Jumanne, 24 Septemba 2013

TAZAMA JINSI AFRIKA MASHARIKI INAVYOANDAMWA NA MATUKIO YA KIGAIDI

Haya ni miongoni mwa mashambulizi makubwa ya kigaidi ambayo yamewahi kutekelezwa katika kanda ya Afrika Mashariki.
Septemba. 21, 2013: Magaidi walitumia maguruneti na bunduki kushambulia jengo la kifahari la Westgate mjini Nairobi, Kenya lenye maduka na mikahawa themanini na kuwaua watu zaidi ya sitini huku zaidi ya 175 wakijeruhiwa.Kundi la kigaidi la Al-Shabab lilikiri kufanya shambulizi hilo.

Oktoba 2011-Machi 2013: Al Shabaab na wapiganaji wake walifanya mashambilizi kadhaa nchini Kenya na kuwaua zaidi ya watu sitini wakilipiza kisasi kile walichosema ni hatua ya Kenya kupeleka majeshi yake nchini huo kupigana dhidi yao. Serikali ya Kenya ilituma vikosi vyake nchini Somalia baada ya al-Shabab kufanya mashambulizi kadhaa katika maeneo ya mipakani pamoja na kuwateka nyara watalii wa kigeni.

Mnamo mwezi Julai tarehe 11,mwaka 2010: Wanamgambo wa Al Shabaab walilipua misururu ya mabomu katika mji mkuu wa Uganda Kampala, katika mkahawa ambako mashabiki wa soka walikuwa wanatizama fainali ya michuano ya kombe la dunia, kwenye skrini kubwa. Takriban watu 76 waliuawa. Kundi la Al-Shabab lilisema kuwa mashambulizi hayo yalikuwa ya kulipiza kisasi kwa Uganda kujihusisha na vita dhidi ya kundi hilo Somalia.

Tarehe 28 mwezi Novemba, mwaka 2002: Kundi hilo la kigaidi lilishambulia hoteli ya kifahari iliyokuwa inamilikiwa na waisraeli, katika eneo la Kikambala karibu na mji wa Mombasa na kuwaua watu 13. Dakika chache kabla ya shambulii hilo, magaidi hao waliifyatulia makombora ndege ya kiisiralei iliyokuwa inaruka katika uwanja wa kimataifa wa Mombasa, lakini waliikosa.

Mnamo tarehe saba Agosti, 7 mwaka 1998: Kundi lengine la kigaidi la Al-Qaida ilishambulia balozi za Marekani mjini Nairobi na Dar es Salam. Mashambulizi hayo yaliwaua watu 224 , wengi wakiwa wakenya . Raia 123 wa Marekani pia waliuawa. Wengine wengi pia walifuawa nchini Tanzaia.

Jumatatu, 23 Septemba 2013

hali bado ni mbaya sana huko Kenya


Jengo la Wastgate likifuka moshi
 
vikosi vya usalama vyaingia

JAMAA WANAOITIKISA KENYA NDIYO HAWA HAPA


 Wapiganaji wa Al Shabaab 
Hizi ni silaha za Al Shabaab walizonasa wanajeshi wa AU
Kundi la wapiganaji wa kisomali la al-Shabaab,limevamia jumba la kifahari lenye maduka na mikahawa nchini Kenya. Al Shabaab lenya mizizi yake nchini Somalia, limeweza kuondolewa kutoka miji mikubwa ya Somalia ikiwemo Mogadishu na sehemu zengine za Somalia , ingawa bado linasalia kuwa tisho kubwa kwa kanda nzima.

Raisi wa Kenya Uhuru Kenyata amewaomba wakenya kuwa watulivu

Raisi wa Kenya uhuru kenyata amewaomba wakenya kuwa watulivu wakati Huu   ambapo vikosi vya usalama vinafanya jitihada kuhakikisha watu waliobaki kaitka jengo la WEST GATE wanaokolewa huku akisisitiza kuwa serikli yake itapambana na magaidi popote pale walipo.
Rais Kenyatta ametoa kauli hiyo  wakati akihutubia taifa jana  juu ya tukio la kuuwawa kwa watu wapatao 68 na wengine zaidi ya 200 kujeruhiwa,ambapo alitoa hotuba hiyo  mbele ya ya viongozi mbalimbali  wa kisiasa akiwemo aliekuwa waziri mkuu wan chi hiyo  raila odinga. Aidha rais uhuru kenyatta amesema vita hii  haihusu dini yoyote wala kabila lolote bali ni vita ya ugaidi.
Tukio hilo limetokea tangu jumamosi sept 21 ambapo mpaka sasa bado kuna watu wameshikiliwa na wavamizi hao ndani ya jengo hilo la WEST GATE MALL lakini serikali ya kenya imewahakikishia wananchi kuwa inafanya jitihada zote kuwaokoa watu walioko ndani ya jengo hilo.
 
Askari wa Kenya wakiwa katika harakati za uokoaji

KENYA BADO HALI NI MBAYA MAUAJI BADO YANAENDELEA


 


Jeshi la Kenya linasema kuwa limedhibiti jengo hilo ingawa hali bado ni mbaya
 
Wakenya waliofanikiwa kuondoka katika jengo la Westgate kwa usaidizi wa polisi

Huku hali ya mshikemshike ikiendelea kushuhudiwa katika jengo la Westgate lenye maduka, ufyatulianaji risasi umesikika ndani ya jengo hilo lenye maduka na mikahawa zaidi ya themanini.
Wapiganaji wa Al shabaab wamewateka nyara raia ambao idadi yao haijulikani. Walikuwemo ndani ya jengo wakiendelea na shughuli zao kuanzia Jumamosi mchana wakati wapiganaji wa Al shabaab walipowavamia na kuanza kufyatua risasi kiholela.