Jumanne, 4 Machi 2014

HUYU NDIYO CHATU ALIYEWEZA KUPIGANA NA KUMSHINDA MAMBA NA KUMMEZA KABISA HIKO AUSTRALIA

 
Nyoka huyo alijipinda kwa Mamba na kumbana hadi akafa
Chatu ameshinda vita vikali dhidi ya Mamba Kaskazini mwa mji wa QueensLand, kupigana na Mamba, kumpinda na kisha kumla.
Tukio hilo lilishuhudiwa katika ziwa Moondarra, karibu na mlima Isa na kunaswa kwa kamera na wakazi wa eneo hilo siku ya Jumapili.
Nyoka huyo mwenye urefu wa futi 10, alijipinda kwa Mamba na kuanza kupambana naye majini.
Hatimaye, Nyoka huyo alifanikiwa kumshinda Mamba na kumtoa nje ya maji na kisha kumla.

Nyoka alimvuta Mamba na kumtoa ndani ya Maji

Chatu huyo alianza kumla Mamba na kushangaza wakazi

Baada ya mlo huo mkubwa Nyoka alijiendea zake
Tiffany Corlis,mkazi wa eneo hilo, alishuhudia pambano hilo na kupiga picha hizi.
"lilikuwa jambo la ajabu sana, '' aliambia BBC
"Tulimuona Nyoka akipambana na Mamba , alifanikiwa kumbana mamba hasa katika sehemu ya miguu ili kumdhibiti.''
"Pambano lilianzia ndani ya maji. Mamba alikuwa anajaribu kuweka kichwa chake juu ya maji wakati mmoja ingawa Nyoka alikuwa amembana sana.''
"Baada ya Mamba kufa Nyoka alijikunjua, na kuja mbele ya Mamba huyo na kuanza kumla,'' alisema Tifanny.
Bwana Corlis alisema kuwa ilimchukua nyoka muda wa robo saa kumla mamba huyo.
''Bila shaka Nyoka huyo alishiba vyema, na hatujui alikokwenda, baada ya mlo wake,'' alisema mama huyo ambaye hakutaka kusuburi kumuona Nyoka tena.
Mtu mwingine aliyeshuhudia pambano hilo Alyce Rosenthal, alisema kuwa wanyama hao wawili walipambana kwa karibu saa 5. Hatimaye wote walionekana wachovu.

ENDELEA KUTEMBELEA BLOG HII KWA MATUKIO ZAIDI

Ijumaa, 28 Februari 2014

IJUE AFRIKA KWA MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/02/27/140227135608_trekking_uganda_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Maelfu ya wakimbizi ambao wamekuwa wakitoroka nchi ya Sudan Kusini kutokana na vita nchini humo wamehamia Uganda. Mpigaji Picha, Fredric Noy, anayefaifanyia kazi Idara ya wakimbizi ya Umoja wa mataifa, anatumia picha, kufarisia maisha ya ukimbizi ya Atem Angang na familia yake.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/02/27/140227135641_trekking_uganda_976x549_bbc_nocredit.jpg
Mji wa Bor alimokuwa anaishi Matiop Atem Angang ndilo lililokuwa la kwanza kudhibitiwa na waasi pindi vita vilipozuka Sudan Kusini mnamo Desemba 15. Yeye pamoja na familia yake kubwa ya watu 15, akiwemo mamake wa miaka 95, watoto wake sita pamoja na familia ya dadake walitoroka kutoka nchini humo.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/02/27/140227135715_trekking_uganda_976x549_bbc_nocredit.jpg
 Bor, mji mkuu wa Jimbo la Jonglei, umekuwa chini ya udhibiti ambao umekuwa ukibadilika kati ya waasi, na serikali mara kwa mara, na imewaacha watu wengi wakiwa wamepoteza maisha. Tangu makubaliano ya kusitisha mapigano kuafikiwa Januari, pande hizo mbili zimekuwa zikilaumiana. Familia ya Bw. Angang imesafiri kwa muda wa wiki moja kwa kutumia dau na lori ili kufika Uganda. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/02/27/140227135749_trekking_uganda_976x549_bbc_nocredit.jpg
Mpakani, walipelekwa kwa kituo cha Shirika la Umoja wa Kimataifa linalotetea haki za kibinaadam lililoko Adjumani, kaskazini mwa nchi hiyo. Wananchi wengi wa Sudan Kusini wanatoroka nchi hiyo, na hii imekifanya kituo hicho kujaa wakimbizi wapya kila uchao. Umoja wa mataifa unasema kuwa takriban watu 860,000 wametoroka kutoka Sudan Kusini tangu kuibuka kwa vita nchini humo.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/02/27/140227141622_trekking_uganda_976x549_bbc_nocredit.jpg
Lori linalowasafirisha wakimbizi kutoka Sudan, akiwemo Bw. Angang na familia yake, linavuka daraja kabla ya kufika kituo cha uhamiaji cha Dzaipi. Lori hizo husafiri hadi mara nne kwa siku kati ya mipakani na kituo hicho cha uhamiaji.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/02/27/140227135915_trekking_uganda_976x549_bbc_nocredit.jpg
Maafisa wa Uganda wanajaribu kuondoa vifaa vya vita kutoka makao hayo, huku wakipekua vitu walivyonavyo wakimbizi wanaofika.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/02/27/140227140002_trekking_uganda_976x549_bbc_nocredit.jpg
Mamake Angang’, Apiou Angar, ambaye ni mkongwe, anakutana na rafiki yake wa zamani wakiwa safarini. Bor, mji ambao ulikuwa unajivunia idadi ya watu 25,000, sasa umebaki mtupu.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/02/27/140227140034_trekking_uganda_976x549_bbc_nocredit.jpg
"Hii familia ina bahati sana ikilinganishwa na zile ambazo itabidi zingoje kwa majuma mawili ili ziweze kuhama na kuenda kuanza maisha mapya katika makao mageni,” hii ni kulingana na Shirika la kutetea haki za kibinaadam la Umoja wa mataifa. Bw. Angang amepiga hema (kulia) kutumia vifaa alivyobeba kutoka Bor. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/02/27/140227140549_trekking_uganda_976x549_bbc_nocredit.jpg
Famililia hii haijazoea makali ya baridi nyakati za usiku, ila walivumilia. Asubuhi ilipofika, akisaidiwa na mkalimani, Bw. Angang aliweza kuisajili familia yake na Shirika la msalaba mwekundu la Uganda.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/02/27/140227140826_trekking_uganda_976x549_bbc_nocredit.jpg
Baada ya kulala chini ya hema ambayo haiwezi kuwakinga kutokana na makali ya baridi kwa siku mbili, watoto wake wanakuwa wagonjwa. Katika kituo cha afya kilichoko karibu, wahudumu wa afya nchini humo wamekuwa wakiwahudumia wagonjwa kwa masaa 12 kutokana na uongezekaji wa idadi ya wakimbizi
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/02/27/140227140905_trekking_uganda_976x549_bbc_nocredit.jpg
Mpwa wa Bw. Angang ambaye ana miezi sita, Nyalet Deng, anachunguzwa na daktari wa kiliniki inayopata ufadhili kutoka kwa shirika la Medicines Sans Frontieres (MSF) iwapo anaugua utapiamlo. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/02/27/140227140942_trekking_uganda_976x549_bbc_nocredit.jpg
Baada ya siku tatu katika kituo cha uhamiaji, familia hiyo inawasili katika makao ya Nyumanzi-mahala ambapo watapaita nyumbani pindi watakavyoendelea kuishi Uganda.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/02/27/140227141048_trekking_uganda_976x549_bbc_nocredit.jpg
Wakati ambapo Bw. Angang na familia yake inangoja kando ya barabara kupewa kipande cha ardhi, wanapiga hema itakayowasaidia kujikinga dhidi ya makali ya jua la mchana.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/02/27/140227141126_trekking_uganda_976x549_bbc_nocredit.jpg
Bw. Angang anaugua malaria, na sasa itambidi bintiye wa miaka 18 kuendea chakula cha mwezi cha familia hiyo kutoka kwa Shirika la chakula duniani. Familia nzima ya Bw. Angang inangoja kwa matumaini iwapo majadialiano ya kusitisha vita nchini Sudan Kusini kati ya serikali na waasi mjini Addis Ababa, Ethiopia,yatavuna matunda. 
 

Jumatano, 29 Januari 2014

MSAFARA WA MBITA KWA PICHA NA BBC SEMA KENYA

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/26/140126080434_mbitacover1_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Mbita ni moja wapo wa miji inayozingira Ziwa Victoria.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/26/140126081435_mbita5_976x549_bbc_nocredit.jpg
Timu ya Sema Kenya ilifika huko kuhamasisha wenyeji kujiunga na mijadala ya utawala katika kipindi kila wiki.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/26/140126081215_mbita4_976x549_bbc_nocredit.jpg
Msafara huu uliwafikia wengi.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122112015_mbita_2_976x549_bbc_nocredit.jpg
Wakazi mbalimbali walijitokeza kusikiliza habari.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122111839_mbita_1_976x549_bbc_nocredit.jpg
Walipata nafasi ya kujadili masuala tofauti inayowahusu kama wakazi wa Mbita.
Wakazi wa Mbita walipata burudani na habari kutoka timu ya Sema Kenya walipozuru mji huo katika msafara.

Alhamisi, 23 Januari 2014

UKREINE YAGEUKA UWANJA WA VITA....SIASA MCHEZO MCHAFU

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145158_kiev-protest-1.jpg 
Angalau watu wawili wameuawa katika ghasia kati ya polisi na waandamanaji katika mji mkuu wa Ukraine Kiev.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145200_kiev-protest-2.jpg
Makabiliano hayo ya Jumatano, yalianza baada ya polisi kuanza kuvunja maandamano ya moja ya makundi ya wanaharati 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145202_body-bbc.jpg
Viongozi wa mashitaka walithibitisha kuwa watu wawili walifariki kutokana na majeraha ya risasi. Ni watu wa kwanza kufariki kutokana na vurugu tangu kuanza Novemba mwaka jana kutokana na mapendekezo ya serikali kujiunga na muungano wa Ulaya
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145204_kiev-protest-4.jpg
Makabiliano hayo yanakuja baada ya siku moja ya kubuniwa sheria mpya za kuharamisha maandamano wiki jana. Bunge liliidhinisha sheria hizo wiki jana na kusababisha vurugu mpya
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145206_kiev-protest-5.jpg
Mamia ya watu wamejeruhiwa ingawa baadhi ya vurugu zimelaumiwa kwa kundi moja linalounga siasa kali
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145208_kiev-protest-6.jpg
Ghasia za Jumatano, zilianzia katika sehemu ndogo ya barabara kuelekea katika majengo ya bunge .
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145210_kiev-protest-7.jpg
Muda mfupi baada ya saa mbili asubuhi, baada ya usiku wa amani, polisi walivamia sehemu ambako waandamanaji hao walikuwa wamekita kambi
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145212_kiev-protest-8.jpg
Polisi baadaye walichukua hatua zao, baada ya makabiliano makali na waandamanaji lakini ilipofika mchana na kuvunja vuzuizi
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145213_kiev-protest-9.jpg
Waandamanaji walianza, kuwatupia mabomu ya petroli na mawe wakati polisi wa kupambana na ghasia nao waliwatupia magurunedi na risasi za mipira
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145215_kiev-protest-10.jpg
Moshi mweusi ulifuka kutokana na magurudumu kuteketezwa wakati wa vurugu hizo mjini Kiev, huku picha za magari ya kivita yakitumiwa kupambana na waandamanaji hao.

Jumatatu, 20 Januari 2014

CHAMA CHA AKIBA NA MIKOPO CHA TAZARA MBEYA CHAFANIKIWA KUTOA MKOPO KWA WANACHAMA WAKE WENYE THAMANI YA BILIONI MOJA

MHASIBU WA CHAMA AKICHEKA NA WANACHAMA
 
 
 
 
 
KAMATI YA MIKOPO WAKIWA BUSY NA KUPITISHA MIKOPO
 
 
 
KARANI WA FEDHA AKIWA MAKINI KUHAKIKISHA HESABU HAZIKOSEWI
ENDELEA KUFUATILIA MATUKIO NA FREE MEDIA TO BLOGS