Jumanne, 2 Desemba 2014

JIONEE MOJA YA VIVUTIO VIKUBWA VYA KITALII KISIWANI PEMBA...HAPA NI PICHA ZA HOTEL YA KISASA KABISA ILIYOPO CHINI YA BAHARI

 


 

 


Kisiwa cha Pemba nchini Tanzania kimekuwa maarufu kwa kilimo cha karafuu visiwani Zanzibar kwa miaka mingi tangu enzi za utawala wa Kiarabu visiwani humo.
Hata hivyo zao hilo limekuwa likikumbwa na changamoto mbalimbali zikiwemo za kushuka kwa bei ya karafuu katika soko la dunia na hivyo kuathiri uchumi wa Zanzibar.
Katika kukabiliana na hali hiyo, serikali ya Zanzibar imekuwa ikitilia umuhimu sekta ya utalii, ambapo huko kisiwani Pemba kumejengwa hoteli ya aina yake, ambayo moja ya vyumba vyake kimejengwa chini ya bahari.
PICHA NA:Mwandishi wa BBC Salim Kikeke alitembelea hoteli hiyo.

Jumatatu, 1 Desemba 2014

JE, INATOSHA TU KUWAWAJIBISHA WAHUSIKA WA SAKATA LA ESCROW? MIMI SIJUI..WATANZANIA WANA MAJIBU ZAIDI!

 
 Waziri mkuu Mh. Mizengo P. Pinda.

Bunge la Tanzania mwishoni mwa wiki limehitimisha mkutano wake wa 17 ambao pamoja na mambo mengine lilijadili taarifa maalum ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali, PAC kuhusu taarifa ya ukaguzi maalum kuhusiana na miamala iliyofanyika katika akaunti ya ESCROW ya TEGETA pamoja na umiliki wa Kampuni ya kufua umeme ya IPTL na kutoa maazimio juu ya sakata hilo.
Miongoni mwa maazimio manane ya Bunge ni kuchukuliwa kwa hatua za kisheria dhidi ya watu wote watakaobainika kuhusika na upotevu wa fedha hizo, kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 300 zilichotwa katika akaunti hiyo iliyokuwa iliyokuwa kwenye Benki Kuu ya Tanzania na ikimilikiwa kwa pamoja na IPTL na Shirika la Umeme Tanzania, TANESCO.
Baadhi ya viongozi na maafisa wa serikali kama vile mawaziri, majaji, wabunge, wenyeviti wa kamati za Bunge, wakuu wa taasisi za umma, viongozi wa dini, mawakili wa kujitegemea na watu binafsi wanatuhumiwa kunufaika na mabilioni ya fedha kutoka akaunti ya Escrow na hivyo hatua stahiki zichukuliwe dhidi yao kwa mujibu wa sheria za nchi.
Pia wabunge wametaka mikataba mibovu ya kuzalisha umeme kati ya TANESCO na makampuni binafsi ya kufua umeme iwasilishwe bungeni au kamati zake kwa lengo la kutekeleza vyema wajibu wake wa kuisimamia na kuishauri serikali.
Kwa miaka mingi TANESCO imekuwa ikilalamika kulipa gharama kubwa za umeme na kusababisha kupanda kwa gharama za matumizi ya nishati hiyo hapa nchini.

Endelea kufuatilia!

Jumamosi, 29 Novemba 2014

LIVE: KUTOKA UWANJA WA NDEGE WA JULIUS NYERERE...MH. RAIS AWASILI SALAMA NCHINI TANZANIA KUTOKA NCHINI MAREKANI KWA MATIBABU

Photo: #HABARI Rais Jakaya Kikwete awasili katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere akitokea nchini Marekani kwa matibabu. Apokelewa na wakazi wa DSM

Anaongea na waandishi wa habari pamoja na wananchi waliopo uwanjani 

@jmkikwete : Waambieni watanzania kuwa nimerudi na afya nzuri ingawa bado najiuguza sehemu niliyochanwa.

@jmkikwete : Nimefanyiwa upasuaji wa tezi dume, Tezi ambayo wanayo wanaume pekee wanawake hawana,si Busha kwa inavyosemekana 

@jmkikwete : Ni kawaida yangu kufanya uchunguzi wa afya, hata mwaka 1984 nilipotoka China, nilifanya ukaguzi wa vyote

@jmkikwete : Ni kawaida yangu kufanya uchunguzi wa afya, hata mwaka 1984 nilipotoka China, nilifanya ukagauzi wa vyote

@jmkikwete : Wasukuma wanaamini kuwa ni ugonjwa ule wa kula madafu, siyo hivyo

@jmkikwete : Tulishauriana na madaktari, tukakubaliana kufanya upasuaji katika hospitali ya Johns Hopkins ambao ni mabingwa

@jmkikwete : Kwa upande wangu hali niliyokuwa nayo ni hatua ya Kwanza ya Saratani ambayo inatibika kwa upasuaji 
 Rais Jakaya Kikwete awasili katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere akitokea nchini Marekani kwa matibabu. Apokelewa na wakazi wa DSM

Anaongea na waandishi wa habari pamoja na wananchi waliopo uwanjani

  • jmkikwete : Waambieni watanzania kuwa nimerudi na afya nzuri ingawa bado najiuguza sehemu niliyochanwa.

  • jmkikwete : Nimefanyiwa upasuaji wa tezi dume, Tezi ambayo wanayo wanaume pekee wanawake hawana,si Busha kwa inavyosemekana

  • jmkikwete : Ni kawaida yangu kufanya uchunguzi wa afya, hata mwaka 1984 nilipotoka China, nilifanya ukaguzi wa vyote

  • jmkikwete : Ni kawaida yangu kufanya uchunguzi wa afya, hata mwaka 1984 nilipotoka China, nilifanya ukagauzi wa vyote

  • jmkikwete : Wasukuma wanaamini kuwa ni ugonjwa ule wa kula madafu, siyo hivyo

  • jmkikwete : Tulishauriana na madaktari, tukakubaliana kufanya upasuaji katika hospitali ya Johns Hopkins ambao ni mabingwa

  • jmkikwete : Kwa upande wangu hali niliyokuwa nayo ni hatua ya Kwanza ya Saratani ambayo inatibika kwa upasuaji

BUNGE LILIGUBIKWA NA UTATA PALE AMBAPO SELIKARI ILISHINDWA KUTOA KAULI ZAKE ZA KUWAWAJIBISHA WASHUTUMIWA WA SAKATA LA ESCROW HAPO JANA..!

Vurugu hizo zilianza saa 04:42 usiku hadi saa 04:49 usiku wakati Spika Anne Makinda alipolazimika kuahirisha Bunge.
Dodoma. Kikao cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jana usiku kilivunjika baada yavurugu kutawala ukumbini humo.
Vurugu hizo zilianza saa 04:42 usiku hadi saa 04:49 usiku wakati Spika Anne Makinda alipolazimika kuahirisha Bunge hadi leo saa tatu asubuhi.
Chanzo cha vurugu ni kutokana na ugumu wa kutokukubaliana na azimio la tisa, lililolenga kumwajibisha moja kwa moja Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
Azimio la PAC lilitaka Waziri Muhongo aadhibiwe kwa kufukuzwa kazi kutokana na tuhuma zilizokuwa zinazomkabili ikiwamo kulidanganya Bunge.
Hata hivyo, baadhi ya wabunge wengi wakiwa wa CCM walitaka waziri huyo asiadhibiwe na Bunge bali achukuliwe hatua na mamlaka iliyomteua.
Wakati ubishani huo ukiendelea, ikiwa imefika saa 4.42 usiku Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alisimama na Spika Makinda alimruhusu kuzungumza.
“Bunge kufikisha saa tano kasoro ni historia, lakini leo (jana) kuna uzito wa kiti na uzito wa wabunge kwa mamlaka ambayo yako ndani yao. Panaonekana kuna maamuzi mengine ya kulinda watu. Kwa nini leo tuna kigugumizi. Tunapata wakati mgumu kuendelea kushiriki kikao cha kulindana. Kwanini mnalinda wezi,” ilikuwa ni kauli ya Mbowe.
Mara baada ya kutoa kauli hiyo, wabunge wote wa upinzani walisimama na kuanza kupiga kelele kwamba wezi waondoke…tunataka fedha zirudi…tunataka fedha zirudi…vijana msilale…vijana msilale.