Alhamisi, 31 Oktoba 2013

MIILI 87 YA WAHAMIAJI YAPATIKANA JANGWANI

 
Jangwa la Sahara
Waokozi nchini Niger wanasema kuwa wamepata miili 87 ya watu waliofariki baada ya magari yao kuharibika walipokuwa wanajaribu kuvuka jangwa la Sahara.
Mmoja wa waliokuwa wanaendesha shughuli ya ukozi Almoustapha Alhacen, alisema kuwa miili yao ilikuwa katika hali mbaya ya kuharibika na kuwa ilikuwa imeliwa sehemu moja na wanyama pori.
Miili hiyo inaaminika kuwa ya wafanyakazi wahamiaji na familia zao. Wengi walikuwa wanawake na watoto.
Niger ni kivukio kikubwa cha wahamiaji wanaokuwa safarini kufika Kusini mwa Jangwa la Sahara kuelekea Ulaya.
Lakini wengi wa wanaofanikiwa kukamilisha safari hiyo huishia kufanya kazi katika mataifa ya Afrika Kaskazini.
Kulingana na Bwana Alhacen, moja ya magari ambayo wahamiaji hao walikuwa wanatumia kwa usafiri, liliharibika walipotoka mji wa Arlit mwishoni mwa mwezi Septemba, au mwanzoni mwa Oktoba.
Maafisa wa usalama pia wamesema kuwa gari la pili liliharibika lilipokuwa njiani kurejea Arlit ili kutengenezwa.
Inaonekana kuwa miongomi mwa wasafiri hao takriban watu 10 walisafari kurejea Arlit na kutoa taarifa ya wenzao kukwama jangwani.
Iliarifiwa kuwa miili mitano ilipatikana.
Mnamo siku ya Jumatano, wafanyakazi wa kujitolea pamoja na wanajeshi, walipokuwa wanawatafuta wahamiaji hao, wakafanikiwa kupata maiti zaidi umbali wa kilomita 10 kutoka katika mpaka wa Algeria.
Kati ya maiti 48 waliopatikana, kulikuwa na miiili ya watoto na vijana na Alhacen alisema kuwa walikuwa wanaelekea nchini Algeria kutafuta vibarua vya mishahara midogo sana.
Akizungumza kutoka katika kiwanda cha kuchimba madini ya Uranium, Kaskazini mwa Agadez, aliambia BBC kuwa hiyo ndiyo iliuwa siku mbaya kwake baada maishani mwake baada ya kupata miili hiyo.

Jumatano, 30 Oktoba 2013

11 WAFARIKI KWENYE AJALI YA TRENI NAIROBI HIVI PUNDE

 
Watu 11 wamethibitishwa kufariki katika ajali iliyohusisha treni na basi iliyokuwa imewabeba watu wakielekea kazini katika mtaa wa Umoja viungani mwa mji wa Nairobi.

Basi hiyo inayoaminika kuwa na watu 34 iligongwa na treni kwenye njia ya reli kuelekea mjini. Kwa mujibu wa shirika la Red Cross, idadi ya majeruhi imefika 34 na wamepelekwa katika hospitali kuu ya Kenyatta.

Baadhi ya waliojeruhiwa wanasemekana kuwa katika hali mbaya.

Walioshuhudia ajali hiyo wanasema kuwa basi hilo lilisukumwa umbali wa mita hamsini baada ya kugongwa kwa upande.

Inaarifiwa watu sita walifariki papo hapo na wengine wawili kufariki baadaye kutokana na majeraha waliyoyapata.

Wengine wengi wamejeruhiwa kwa mujibu wa shirika la msalaba mwekundu.

Mwandishi wa habari wa shirika la habari la AFP aliyeshuhudia ajali hiyo alisema kuwa basi iliharibiwa vibaya baada ya kugongwa kwa upande na treni ihiyo ilikuwa inasafiri kwa kasi kubwa.

Ajali hiyo imetokea asubuhi wakati wa msongamano wa watu na magari huku watu wengi wakiwa katika haraka kuu kuelekea kazini

UTANI WA SIMBA NA YANGA SASA WAHAMIA MBEYA CITY NA TANZANIA PRISON...! ONA JINSI UWANJA WA SOKOINE MBEYA ULIVYCHAFUKA HAPO JANA TAR.29/10/2013

 JUKWAA LA MASHABIKI NA WAPENZI WA MBEYA CITY













 WACHEZAJI WAKISHANGILIA GOLI LAO LA KWANZA







 ANGALIA PENALTY HIYO INAPIGWA NA DEOGRATIUS JULIUS
















MASHABIKI WA MBEYA CITY WAKIWA WAMEBEBA JENEZA







 KAMA KAWAIDA YA TIMU HII MWISHO WA MCHEZO HUWA INAPENDA KUTOA SHUKRANI KWA MASHABIKI WAO







 HADI MWISHO WA MCHEZO MBEYA CITY 2-O PRISON

PICHA ZOTE NA FREE MEDIA TO BLOGS