Arsenal bado inaongoza ligi kuu ya England kufuatia ushindi wao dhidi ya Crystal Palace.
Ushindi wa Arsenal umepatikana katika kipindi
cha pili.Goli la kwanza limefungwa na Mikel Arteta kwa njia ya penalty
kabla ya Olivier Djiroud kufunga kazi dakika chache kabla ya kipenga cha
mwisho kulia.Manchester United yaepuka kichapo.
Katika mechi nyingine zilizochezwa,Manchester United imetoka nyuma na kushinda mechi yake dhidi ya Stoke mabao 3-2 baada ya kufungwa 2-1 katika kipindi cha kwanza.
Matokeo mengine Everton ikichezea ugenini imeifunga Aston Villa magoli 2-0.Norwich imetoka sare na Cardiff bila kufungana.Liverpool ikailima West Bromich mabao 4-1 yakiwemo 3 yaliyotiwa kimiani na Luis Suarez na Southampton ikaifunga Fulham
Kwenye msimamo wa muda wa ligi kuu ya England,Arsenal ni ya kwanza ikiwa na alama 22 ikifuatiwa na Livepool yenye alama 20.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni