Jumamosi, 26 Oktoba 2013

RAIS KIKWETE AITABIRIA MAKUBWA CCM 2015-2020

 
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwahutubia wanachama wa chama hicho kwenye moja ya mikutano, Kilosa mjini mkoani Morogoro.  

Dodoma. Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete amesema kama rushwa haitakomeshwa ndani ya chama hicho, katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka 2015 kitaanguka vibaya na iwapo kitanusurika hakitapita kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.
Katika hatua nyingine, Rais Kikwete amempa jukumu la kushughulikia viongozi wa CCM wanaokula rushwa, Makamu Mwenyekiti wa CCM, Philipo Mangula.
Rais Kikwete, alitoa onyo hilo juzi usiku, alipokuwa akifunga mafunzo maalumu ya siku nne kwa makatibu wa mikoa, makatibu na wenyeviti wa wilaya wa chama hicho nchini.
“Kama hatutabadilika katika suala la rushwa mwaka 2015 tutakuwa na wakati mgumu sana na kama mwaka huo tutafanikiwa kuishika Serikali, basi mwaka 2020 hatutarudi tena madarakani.

IFIKE MAHALI WATU TUNATAKIWA KUENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA...USAFIRI WA HARAKA NI KITU MOJAWAPO

NEWS ALERT, PICHA: NDEGE YA FASTJET YAFANYA (SURVEY) KATIKA ANGA YA UWANJA WA KIMATAIFA WA NDEGE SONGWE JIJINI MBEYA.

Ndege kubwa ya Fastjet ikiwa inaonekana angani wakati ikifanya survey juu ya uwanja wa kimataifa wa Songwe Mbeya
Hizi ni  Ngazi maalum kabisa ambazo zinatarajiwa kutumika wakati ndege ya Fastjet itakapo anza safari zake mkoani Mbeya.
 Wanaosalimiana ni Watumishi wa Eneo la uwanja wa Ndege na Aliye vaa Nguo za Blue pamoja ni Bwana Mwaipopo mdau mkubwa wa Mbeya yetu Blog.
 Huyu Bwana mdogo anaitwa Eric Mwaisango nae alikuwepo kushuhudia ndege ya Fastjet 
 Hili ni eneo la Nje ya la Uwanja wa kimataifa wa Songwe Mbeya 

****
Leo asubuhi majira ya saa Mbili na nusu Ndege ya Fastjet kwa Mara ya kwanza kabisa ilishuhudiwa na watu wachache katika Uwanja wa wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe ambapo ilikuwa ikifanya Survey angani bila kutua.

Ndege hiyo ambayo ilipita jirani kabisa na uwanja huo kwa Takribani ya zaidi ya mara tatu , ilifanya hivyo kwa sababu za kitaalam, hata hivyo hiyo ilikuwa ni amsha amsha huku siku chache zijazo ndege hiyo itatua kwa mara ya kwanza na Rasmi Jijini Mbeya katika uwanja wa Ndege wa Songwe.

Kwa nyakati Tofauti Baadhi ya Abiria waliokuwa wakijiandaa na kusafiri katika uwanja huo na Ndege zengine walionekana kuwa na furaha na kuzungumza mambo tofauti ikiwa na pamoja na kufurahishwa na hatua ya Ndege ya fastjet kuanza safari zake mkoani Mbeya na kusisitiza kwamba itakuwa ni Mkombozi mkubwa kutokana na bei zao kuwa chini na safari za uhakika.

Timu nzima ya Mbeya yetu Blog ilifika uwanjani mapema na kushuhudia kile kilicho onekana uwanjani hapo, na mpaka wanaondoka uwanjani hapo ndege hiyo ilikuwa tayari imesha anza safari za kurejea jijini Dar es salaam.

Je Mwananchi na Mkazi wa Mbeya na Mikoa ya Jirani unasemaje kuhusiana na Fastjet kuanza safari za kuja Mbeya hivi karibuni???

HIVI BINADAMU ATAISHI KWA UHURU LINI?

ONA WALINZI KADHAA WAUAWA MPAKANI MWA IRAQ
Msafara wa magari Saravan, Iran 
Shirika la habari la taifa la Iran, IRNA, limearifu kuwa walinzi 17 wa mpaka wameuwawa katika mapambano na watu waliokuwa na silaha, kwenye mpaka wa Iran na Pakistan.
IRNA imeeleza kuwa baada ya shambulio hilo watu 16 wamenyongwa - watu wenye uhusiano na makundi yenye uhasama na serikali.
Kisa hicho cha mpakani kimetokea kwenye eneo la milima nje ya mji wa Saravan.
Washambuliaji hawajulikani, lakini mjumbe mmoja wa bunge la Saravan, Hedayatollah Mirmoradzehi, aliwaeleza hao kuwa magaidi wanaopinga mapinduzi.
Mpaka wa Iran na Pakistan huwa na machafuko na eneo hilo ni njia inayotumiwa na wafanya magendo ya mihadarati.