Ijumaa, 5 Desemba 2014

NAWEZA KUSEMA SIKU ZA KUFUNGA MWAKA HUWA NA MAMBO MENGI....HII NI AJALI ILIYOTEKEA HIVI PUNDE ENEO LA MLIMA NYOKA HAPA MKOANI MBEYA

Lori la Mafuta lenye namba za Usajiri T332 AGA ambalo Dereva wake Godfrey Lyimo (33) alikuwa amejeruhiwa vibaya na kukimbizwa hospitali kwa matibabu zaidi, Hapa Lori hilo la mafuta liliwa Limepinduka.

Basi la Mbukio Missio muda mfupi baada ya kupata ajali ambayo ilisababishwa na Dereva wa Basi hilo, Hapa vijana wakiwa wamechukua magazeti wakificha jina la Basi hilo lisitambulike kwa wale wanaokuja kushuhudia ajali hiyo, Nia na lengo la kufanya hivyo haijafahamika mpaka sasa.
Baadhi ya Abiria , Washuhudiaji pamoja na Askari wakiwa eneo la Mlima Nyoka ambapo ajali ilipo tokea
Watu 50 wamenusurika kifo baada ya basi la Mbukio Mission waliokuwa wakisafiria kugongana na lori la mafuta katika eneo la Mlima Nyoka hapa mkoani Mbeya hivi karibuni...
Chanzo na ITV Tanzania