Jumatano, 30 Oktoba 2013

11 WAFARIKI KWENYE AJALI YA TRENI NAIROBI HIVI PUNDE

 
Watu 11 wamethibitishwa kufariki katika ajali iliyohusisha treni na basi iliyokuwa imewabeba watu wakielekea kazini katika mtaa wa Umoja viungani mwa mji wa Nairobi.

Basi hiyo inayoaminika kuwa na watu 34 iligongwa na treni kwenye njia ya reli kuelekea mjini. Kwa mujibu wa shirika la Red Cross, idadi ya majeruhi imefika 34 na wamepelekwa katika hospitali kuu ya Kenyatta.

Baadhi ya waliojeruhiwa wanasemekana kuwa katika hali mbaya.

Walioshuhudia ajali hiyo wanasema kuwa basi hilo lilisukumwa umbali wa mita hamsini baada ya kugongwa kwa upande.

Inaarifiwa watu sita walifariki papo hapo na wengine wawili kufariki baadaye kutokana na majeraha waliyoyapata.

Wengine wengi wamejeruhiwa kwa mujibu wa shirika la msalaba mwekundu.

Mwandishi wa habari wa shirika la habari la AFP aliyeshuhudia ajali hiyo alisema kuwa basi iliharibiwa vibaya baada ya kugongwa kwa upande na treni ihiyo ilikuwa inasafiri kwa kasi kubwa.

Ajali hiyo imetokea asubuhi wakati wa msongamano wa watu na magari huku watu wengi wakiwa katika haraka kuu kuelekea kazini

UTANI WA SIMBA NA YANGA SASA WAHAMIA MBEYA CITY NA TANZANIA PRISON...! ONA JINSI UWANJA WA SOKOINE MBEYA ULIVYCHAFUKA HAPO JANA TAR.29/10/2013

 JUKWAA LA MASHABIKI NA WAPENZI WA MBEYA CITY













 WACHEZAJI WAKISHANGILIA GOLI LAO LA KWANZA







 ANGALIA PENALTY HIYO INAPIGWA NA DEOGRATIUS JULIUS
















MASHABIKI WA MBEYA CITY WAKIWA WAMEBEBA JENEZA







 KAMA KAWAIDA YA TIMU HII MWISHO WA MCHEZO HUWA INAPENDA KUTOA SHUKRANI KWA MASHABIKI WAO







 HADI MWISHO WA MCHEZO MBEYA CITY 2-O PRISON

PICHA ZOTE NA FREE MEDIA TO BLOGS