Wapiganaji wa kiisilamu al shabaab
Takriban viongozi 160 wa kidini nchini Somalia
wametoa kauli au Fatwa inayolaani kundi la al-Shabab, wakisema kuwa
kundi hilo haliruhusiwi kabisa katika dini ya kiisilamu.
Wadadisi wanasema kuwa ni mara ya kwanza kwa
viongozi wa kidini nchini Somalia kutoa Fatwa aina hiyokulaani kundi
hilo ambalo linadhibiti maeneo mengi ya vijijini na mijini.