Mshindi wa mbio za Marathon mjini Berlin, Ujerumani mkenya Wilson
Kipsang mwenye umri wa miaka 31. Hapa anasherehekea ushindi wake.
Alivunja rekodi ya mbio hizo kwa sekunde kumi na tano.
Wachezaji wa mchezo wa Roller Skating mjini Lagos Nigeria wanasherehekea miaka 53 ya uhuru wa Nigeria.
Watoto wa shule pia walisherehekea uhuru wa Nigeria kote nchini humo siku ya Jumanne wiki jana
Wafanyakazi wakibeba mchanga kutoka machimboni mjini Mogadishu,siku ya
Jumanne. Kuna machimbo mengi kama hay ambayo yamekuwa na shughuli nyingi
katika miaka miwili iliyopita tangu al-Shabab kufurushwa na kusababisha
ujenzi mkubwa.
Msichana huyu alikuwa miongoni mwa waliohudhuria maombi maalum kwa watu
waliofariki kutokana na shambulizi la kigaidi dhidi ya jumba la Westgate
mjini Nairobi, Kenya
Raia hawa wa Ghana walihudhuria kongamano la kila mwaka la chama cha Conservative katika mtaa wa Manchester nchini Uingereza
Carranzar Naa Okailey Shooter, (kushoto) aliwakilisha Ghana katika
mashindano ya mwanamke mrembo zaidi duniani. Hapa amesimama na mshindi
wa mashindano hayo (katikati) kutoka Ufilipino.
Wamiliki wa boti za usafiri wanawasubiri abiria kwenye fuo za mto Nile
mjini Cairo. Safari za boti ni jambo la kawaida sana na watu husafiri
kwa boti zaidi nyakati za jioni kujivinjari
Pindi wanapowasili, wavuvi hukimbia sokoni na samaki wao waliowavua kwa siku hiyo kuelekea kuwauza katika soko la Kivukoni
Si Samaki pekee wanaovuliwa bali pia Pweza hawa wanaoaminika kuongeza nguvu za kiume mwilini
Uhaba wa maji nchini Senegal ni tatizo sugu na hii ndiyo dalili yake watu kupanga foleni kununua maji