Jumamosi, 28 Septemba 2013

RAIS OBAMA AZUNGUMZA NA ROUHANI

Rais Rouhani na Obama
Kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka 30, viongozi wa Marekani na Iran wamezungumza moja kwa moja.

Rais Barack Obama na mwenzake wa Iran, Hassan Rouhani, wamezungumza kwa simu kwa muda wa robo saa; na kwa mujibu wa Bwana Obama walieleza azma yao ya kutatua mzozo wa muda mrefu kuhusu mradi wa nuklia wa Iran.

Ujumbe kwenye mtandao wa Twitter kutoka ofisi ya Bwana Rouhani ulionesha hisia kama hizo.
Taarifa kutoka Iran zinaonesha kuwa tukio hilo limefurahiwa nchini humo, hasa kati ya washauri wakuu wa Bwana Rouhani.

BODI YA MIKOPO TANZANIA IMETOA MIKOPO KWA WANAFUNZI 29,754

http://www.dailynews.co.tz/images/HESLBI.jpg
AFISA MAWASILIANO,HABARI NA ELIMU WA BODI YA MIKOPO KWA ELIMU YA JUU 

TANZANIA (HESLB) NDUGU COSMAS MWAISOBWA AKITOA TAARIFA HIYO KWA 

VYOMBO YA HABARI JANA KWA WANAVYUO WALIFANIKIWA KUPATA MKOPO HUO 

MWAKA WA MASOMO WA 2013/2014 JIJINI DAR ES SALAAM

KUTOKANA NA TAARIFA HIYO WANAFUNZI WANAWEZA KUPATA HABARI KAMILI 

KUPITIA WAVUTI YA BODI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU.

http://www.heslb.go.tz/
AKIZUNGUMZA JANA NA VYOMBA VYA HABARI ALISEMA, JUMLA YA WANAFUNZI 

WALIOOMBA WALIKUWA 53,239 WALIODAHIRIWA WALIKUWA 43,032 WALIOKUWA NA 

MATATIZO YA MAOMBI WALIKUWA  3,151 WAKAYASAHIHISHA NA 3.213 

HAWAKUFANYA MASAHIHISHO YA AINA YOYOTE.


MATUKIO KATIKA PICHA

RAIS JAKAYA M. KIKWETE AKISAINI KITABU CHA RAMBIRAMBI CHA WAHANGA WA MLIPUKO WA WASTGATE SIKU YA JANA HUKO NEW YORK MAREKANI.
PEMBENI NI BALOZI WA KENYA NCHINI MAREKANI
AFISA HABARI WA BUNGE LA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NDUGU OWEN MWANDUMBYA AKIONGEA NA MAAFISA HABARI WENGINE WA BUNGE JIJINI DAR ES SALAAM HAPO JANA IJUMAA

WATU 50 WAUAWA KWENYE GHASIA NCHINI SUDAN



Ghasia zilianza Jumatatu serikali ilipoondoa ruzuku kwa mafuta

Maafisa wa usalama nchini Sudan wamewaua watu 50 katika maandamano yaliyofanywa kwa siku kadhaa kupinga hatua ya serikali kuondoa ruzuku ya mafuta. Taarifa hii ni kwa mujibu wa mashirika ya kutetea haki za binadamu nchini humo.