Alhamisi, 10 Julai 2014

HII NI ZAIDI YA MVUA YA MAGOLI: KICHAPO KWA TIMU YA BRAZIL

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/07/09/140709084904_bra_v_ger_1.jpg 
Bao la kwanza la Ujerumani lilipokewa kwa vifijo na nderemo na mashabiki waliokuwa wamejaa pomoni kushuhudia timu yao ikimenyena na mabingwa mara sita wa kombe la dunia Brazil  
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/07/08/140708203553_thomas_mueller_976x549_reuters.jpg 
Mechi hii ilikua ya kwanza ya nusu fainali katika kombe la dunia mwaka 2014 nchini Brazil  
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/07/08/140708204203_toni_kroos_976x549_afp.jpg 
Wengi wamesema wachezaji wa Ujerumani walikuwa 'balaa' yaani walikuwa wakali katika mechi hiyo
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/07/08/140708225505_brazil_defeat_976x549_ap.jpg
Kipa wa Ujerumani hakuwa na chochote cha kufanya kwani hali ilikuwa ngumu kweli.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/07/09/140709084918_bra_v_ger_8.jpg
Ilikuwa sherehe kila pembe ya dunia kutoka kwa mashabiki wa Ujerumani na hata nyumbani baada ya timu yao kuingiza mabao matano katika dakika za kwanza 29 za mechi hiyo 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/07/08/140708203937_toni_kroos_976x549_reuters.jpg
Mabao yaliendelea kuingizwa hadi yakafika saba mwishoni mwa mechi. Brazil hata hivyo walikomboa bao moja la kupanguzia machozi, ila halikutosha kuondoa aibu waliyoipata katika mchuano huu ambao umewaacha wengi vinywa wazi
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/07/09/140709084910_bra_v_ger_4.jpg
Mashabiki wa Brazil walikuwa wanajionea giza uwanjani magoli yakiingizwa na Ujerumai kutoka pembe zote za uwanja
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/07/08/140708203223_thomas_mueller_976x549_ap.jpg
Ujerumani sasa watajiandaa kumenyana na mshindi wa mechi kati ya Uholanzi na Argentina Brazil itasalia kupigania nafasi ya tatu 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/07/09/140709084914_bra_v_ger_6.jpg
Huzuni ulitanda Brazil na kote duniani kwa mashabiki wa Brazil 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/07/09/140709081157_david_luiz_brazil_football_worldcup_semi_final_976x549_reuters_nocredit.jpg
Lakini nahodha wa muda wa Brazil David Luiz amewataka mashabiki wa timu hiyo kote duniani kuwasamehe wachezaji waliokuwa uwanjani Selecao,walipoadhibiwa kichapo cha mabao 7-1 na Ujerumani katika mechi ya kwanza ya nusu fainali ya kombe la dunia huko Brazil.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/07/08/140708205601_germany_976x549_afp.jpg
Kwa sasa hadi fainali za kombe la dunia ni sherehe kote kote nchini Ujerumani 

ENDELEA KUFUATILIA MATUKIO ZAIDI YA KOMBE LA DUNIA KUPITIA HAPAHAPA BLOG YA KIJANJA
NITAWALETEA TENA MATUKIO YA BRAZIL KUTAFUTA NAFASI YA TATU AMA YA NNE!