Jumapili, 17 Novemba 2013

JE, UNAPENDA SAMATTA AU WANYAMA TUZO ZA MWANASOKA BORA AFRIKA?

 
Mbwana Samatta (kushoto) kutoka Tanzania na Victor Wanyama (kulia) kutoka Kenya
Shirikisho la kandanda barani Afrika CAF limetangaza majina ya wachezaji wa kiafrika watakaowania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa mwaka 2013 na Mchezaji bora wa Afrika anayechezea vilabu vya ndani ya Afrika mwaka 2013.
Katika majina hayo yapo majina mawili ya wachezaji wanaotoka Afrika Mashariki ambao ni Victor Wanyama raia wa Kenya anachezea Southampton FC ya England ambaye ni miongoni mwa wachezaji 25 watakaowania tuzo ya Mchezaji bora wa Afrika, huku Mbwana Samatta raia wa Tanzania anayechezea klabu ya TP Mazembe ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo yeye ameteuliwa kuwania tuzo ya Mchezaji bora wa Afrika anayechezea timu za Afrika.
Wachezaji 25 watawania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika na 21 Mchezaji bora wa Afrika anachezea timu za ndani ya Afrika.
Washindi wa tuzo hizo wanatarajiwa kutangazwa Januari 9, mwaka 2014 mjini Lagos nchini Nigeria.
Orodha kamili ya wachezaji waliotangazwa na CAF na timu wanazotoka hii hapa chini.

Mchezaji wa bora wa CAF Afrika

1. Ahmed Musa - Nigeria - CSKA Moscow
2. Asamoah Gyan - Ghana - Al Ain
3.Dame N'Doye - Senegal - Locomotiv Moscow
4. Didier Drogba - Cote d'Ivoire - Galatasaray
5. Emmanuel Emenike - Nigeria - Fenerbahce
6. Islam Slimani - Algeria - Sporting Lisbon
7. John Mikel Obi - Nigeria - Chelsea
8. Jonathan Pitroipa - Burkina Faso - Stade Rennais
9. Kévin Constant - Guinea - AC Milan
10. Kwadwo Asamoah - Ghana - Juventus
11. Luís Carlos Almada Soares (platini) - Cape Verde - AC Omonia
12. Mehdi Benattia - Morocco - AS Roma
13. Mohamed Aboutrika - Egypt - Al Ahly
14. Mohamed Salah - Egypt - Basel FC
15. Nicolas Nkoulou - Cameroon - Marseille
16. Pierre-Emerick Aubameyang - Gabon - Borussia Dortmund
17. Ryan Isaac Mendes da Graça - Cape Verde - Lille
18. Saladin Said - Ethiopia - Wadi Degla FC
Victor Wanyama
19. Seydou Keita - Mali - Dalian Aerbin F.C
20. Sofiane Feghouli - Algeria - Valencia
21. Sunday Mba - Nigeria - Warri Wolves
22. Victor Wanyama - Kenya - Southampton FC
23. Vincent Enyeama - Nigeria - Lille
24. Yao Kouassi Gervais 'Gervinho' - Cote d'Ivoire - AS Roma
25. Yaya Toure - Cote d'Ivoire - Manchester City

Mchezaji bora Afrika anacheza vilabu ndani ya Afrika

1. Adane Girma - Ethiopia - St George
2.Ahmed Fathi - Egypt - Al Ahly
3. Alexis Yougouda Kada - Cameroon - Coton Sport
4. Ali Machani - Tunisia - CAB
5. Bapidi Fils Jean Jules - Cameroon - Coton Sport
6. Daine Marcelle-Klate - South Africa - Orlando Pirates
7. Fakhreddine Ben Youssef - Tunisia - CSS
8. Getaneh Kebede - Ethiopia - Bidvest Wits
9. Idrissa Kouyate - Cote d'Ivoire - CS Sfaxien
10. Iheb Msakni - Tunisia - Esperance
11. Luyanda Lennox Bacela - South Africa - Orlando Pirates
12. Mbwana Samatta - Tanzania - TP Mazembe

 
Mbwana Samatta
13. Moez Ben Cherifia - Tunisia - EST
14. Mohamed Aboutrika - Egypt - Ahly
15. Rainford Kalaba - Zambia - TP Mazembe
16. Senzo Meyiwa - South Africa - Orlando Pirates
17. Soumbeila Diakite - Mali - Stade Malien
18. Sunday Mba - Nigeria - Warri Wolves
19. Tresor Mputu - DR Congo - TP Mazembe
20. Waleed Soliman - Egypt - Al Ahly
21. Yannick N'djeng - Cameroon - EST

JE UNAJUA KUWA NYOKA NA KONOKONO NI TIBA MBADALA KWENYE MWILI WAKO?

 
Nyoka na konokono wamekuwa tiba mbadala kwa watu wengi katika nchi za Ulaya na Asia, ikiwemo kuondoa uzee
Wakati nyoka akiendelea kuwa adui mkubwa wa binadamu na konokono kuonekana mdudu anayetia kinyaa kwa baadhi ya watu, nchi za China na Japan wanyama hawa wamekuwa wakitumika kama mboga na wakati mwingine wamekuwa ni rafiki wa binadamu kwani wengi wao hufugwa na binadamu.
Lakini Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni, kwani katika nchi za Ulaya miezi kadhaa iliyopita watu mbalimbali wameanza kupokea tiba kutoka kwa wanyama hao ikiwemo huduma ya kukanda na kupodoa uso (facial) inayotolewa na konokono na kusinga (massage) inayotolewa na nyoka.
Facial ya konokono
Kwa wengi wetu konokono ni mdudu mpole zaidi kuliko wadudu wengine wanaopatikana majanini, lakini nchini Japan wataalamu wamegundua kuwa lami (uteute) anaotoa mdudu huyo ni tiba nzuri kwa ngozi ya binadamu, baada ya kutumika kwa miezi kadhaa nchini Japan sasa tiba hiyo imeanza kupendwa barani Ulaya, kama watu wanavyomiminika katika saluni moja iliyopo East Midland nchini Uingereza.
Matibabu hayo yanahusisha konokono kuanzia watatu ambao huwekwa juu ya uso wa binadamu na wao huanza kuzunguka maeneo mbalimbali ya uso huo, yamekuwa yakiongeza uwingi wa watu katika saluni za maeneo mbalimbali ya nchi za Ulaya.