Alhamisi, 26 Septemba 2013

WATAALAM WAKITAFUTA MIILI YA WATU WALIOPOTEZA MAISHA WASTGATE



Jengo la Westgate ambalo ghorofa zake tatu ziliporomoka

Vikundi vya maafisa wa uchunguzi wa mauaji vinatafuta miili ya mateka waliouawa ndani ya jengo la Westgate ambao idadi yao haijulikani.

Mateka walizuiliwa na magaidi kwa siku nne kabla ya serikali kutangaza kumalizika rasmi kwa shambulizi hilo
Zaidi ya watu 65 waliuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa.

Waziri wa usalama Joseph Ole Lenku amesema kuwa hatarajii kuwa idadi ya waliofariki itaongezeka na kusema kuwa miili ya magaidi pakee ndio itapatikana ndani ya vifusi.

Hii ni baada ya sehemu ya jengo hilo kuporomoka wakati shughuli za uokozi zilikuwa zinaendelea .
Lakini kwa mujibu wa shirika la Red Cross, watu 61 wangali hawajulikani waliko.

Wakati huohuo, Kenya inaendelea na siku tatu za maombolezi ya vifo vya raia na baadhi ya maafisa wa usalama waliofariki katika shambulizi hilo.

Mazishi ya mtangazaji mmoja wa Televisheni na Redio, Ruhila Adatia yalifanyika siku ya Alhamisi.

Bendera zingali zinapeperushwa nusu mlingoti kwa heshima ya wale waliofariki.
Walinzi walionekana wakichunguza abiria kabla ya kuabiri magari ya usafiri.

Huku wasiwasi ukiongezeka miongoni mwa wakenya kuhusu hali ya kujiandaa kwa maafisa wa usalama kuhusiana na mashambulizi kama haya, taarifa zinasema kuwa serikali inajiandaa kudurusu mikakati yake ya kupigana dhidi ya ugaidi na majanga mengine.

Kundi la kigaidi la Al Shabaab linasema limeshambuli Kenya kutokana na nchi hiyo kujihusisha na vita dhidi ya kundi hilo nchini Somalia

UGANDA YAPATA NEEMA KUTOKA CHINA

Uchimbaji mafuta ukifanywa na kampuni ya (CNOOC)

Kampuni ya kitaifa inayomilikiwa na China ya Offshore Oil, (CNOOC) imeshinda kandarasi yenye thamani ya dola bilioni 2 kujenga kiwanda cha mafuta nchini Uganda.

Kiwanda hicho kinaaminika kuwa na uwezo wa kuzalisha mitungi milioni 635 za mafuta.
Hatua hii ni ya uwekezaji ya hivi karubini kuchukuliwa na makampuni ya China katika sekta kigeni ya mafuta na gesi.

Makampuni ya China, yamekuwa yakitaka kuekeza katika sekta ya kawi ili kukidhi mahitaji yake ya kiuchumi.

Kampuni hiyo itajenga kiwanda hicho kwa kipindi cha miaka minne.
Aidha kiwanda hicho kina uwezo wa kuzalisha kati ya mitungi 30,000 hadi 40,000 ya mafuta kila siku.

Ukuwaji wa haraka wa uchumi wa China katika miaka ya hivi karibuni, imesababisha kuongezeka kwa mahitaji ya mafuta , na kuifanya kuwa nchi inayotumia mafuta kwa wingi duniani.

Mahitaji hayo yanatarajiwa kuongezeka hata zaidi huku uchumi wake ukiendelea kukuwa.
Lakini China inategemea sana bidhaa za kutoka nje kuweza kukidhi mahitaji yake.

Kutokana na hilo, makampuni ya China yanatafuta sana kuekeza katika sekta ya gesi na mafuta.
Mwaka jana kampuni hiyo ilikubali kulipa dola bilioni 15.1 katika kununua kampuni ya mafuta ya Nexen nchini Canada.

MTOTO WA MIAKA MINNE AWAAMBIA MAGAIDI WA WESTGATE KUWA NI WABAYA

Mtoto wa miaka minne ambaye ni raia wa Uingereza, Elliott Prior ameonyesha ushujaa wa hali ya juu baada ya kuweza kuwatolea maneno makali na ya kugusa magaidi waliovamia jengo la maduka la Westgate.

MATOKEO YA KOMBE LA CAPITAL ONE ROUND YA TATU 25/09/2013


MANCHESTER UNITED 1-O LIVERPOOL
Birmingham: Celebrate Dan Burn's opener against Swansea 
BIRMINGHAM 3-1 SWANSEA
Papiss Cisse: Scored his first goal in 14 games during the first half against Leeds United 
NEWCASTLE 2-O LEEDS
Stephen Ireland: On target in Stoke's win at Tranmere 
TRANMERE O-2 STOKE CITY
Youssouf Mulumbu: Had a half-volley saved by Fabianski 
WEST BROM 1-1 ARSENAL

WAZIRI PINDA APOKELEWA KWA MABANGO KWA BABU LOLIONDO


“Wananchi wanataka amani kwani migogoro imeshasababisha vifo na mali nyingi kupotea sasa tunataka amani,"
Wakazi wa Kata ya Samunge, wilayani Ngorongoro Mkoa wa Arusha, jana walimpokea Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwa mabango wakiomba Serikali iligawe Jimbo la Ngorongoro na ikomeshe mapigano ya kikabila.