Jumatano, 18 Septemba 2013

MATOKEO YA LIGI KUU TANZANIA BARA HII LEO


AZAM 1-1 ASHANTI

RUVU JKT O- 1 RUVU SHOOTING

MBEYA CITY O-O MTIBWA SUGAR

YANGA 1-1 PRISON

SIMBA 6-O MGAMBO

RINHO RANGERS 1-1 COST UNION

KAGERA SUGAR 1-1 JKT OLJOLO

habari za hivi punde:Jeshi la Nigeria lawaua wapiganaji 150



Wanajeshi 9 wangali hawajulikani waliko baada ya makabiliano makali kuzuka kati ya wapiganaji na wanajeshi hao mjini Borno
Jeshi la Nigeria, linasema kuwa limewaua wapiganaji 150 wa kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Boko Haram wakati wa msako dhidi yao wiki jana.
Makabiliano yalitokea wakati jeshi lilipokuwa linafanya msako dhidi ya wapiganaji hao katika jimbo la Borno Kaskazini Mashariki mwa nchi.
Katika taarifa yake, jeshi lilisema kuwa takriban wanajeshi 16, walifariki wakati walipofanya shambulizi la kwanza dhidi ya kambi ya wanajeshi hao ambako walipata silaha nzito
Wanajeshi wengine wa serikali wanasemekana kutojulikana waliko. Aidha jeshi lilisema pia liliweza kumuua kamanda wa wapiganaji hao Abba Goroma.
Mwandishi wa BBC nchini Nigeria anasema kuwa, jeshi kwa kawaida huongeza chumvi idadi ya wapiganaji waliouawa kwa lengo la kuonyesha kuwa wanajeshi waliouawa kwenye mapigano walikuwa wachache.
Boko Haram ilianza harakati zake mwaka 2009 katika jimbo la Borno ambalo hadi sasa liko chini ya sheria ya hali ya hatari

TCRA WAANZA KUWANOA MA BLOGGERS TANZANIA

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma akiwasilisha mada ya kwanza juu ya Ukubwa wa Sekta ya Mawasiliano hapa nchini wakati wa Warsha ya siku mbili kwa wamililiki wa magazeti tando (Bloggers) hapa nchini,iliyoanza rasmi leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania,Uliopo eneo la Sinza B,jijini Dar es Salaam.


Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Innocent Mungy akifafanua jambo wakati wa Warsha ya siku mbili kwa wamililiki wa magazeti tando (Bloggers) hapa nchini,iliyoanza rasmi leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania,Uliopo eneo la Sinza B,jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Sekta ya Washangiaji na Watoa Huduma wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA),Dkt. Raynold Mfungahema akiwasilisha mada wakati wa Warsha ya siku mbili kwa wamililiki wa magazeti tando (Bloggers) hapa nchini,iliyoanza rasmi leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania,Uliopo eneo la Sinza B,jijini Dar es Salaam.


 Baadhi ya Viongozi na Bloggers wakiwa wanafuatilia kwa umakini Mafunzo
 Sehemu ya Wapiga Picha kutoka Vyombo mbali mbali vya habari wakiendelea na zoezi la kuchukua matukio mbali mbali wakati wa Warsha ya siku mbili kwa wamililiki wa magazeti tando (Blogggers) hapa nchini,iliyoanza rasmi leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania,Uliopo eneo la Sinza B,jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya Bloggers mbali mbali hapa nchini  wakiwa kwenye Warsha hiyo ya siku mbili iliyoanza rasmi leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania,Uliopo eneo la Sinza B,jijini Dar es Salaam.

 Kutoka Kulia ni Mwandishi Mkuu wa Mbeya yetu Blog Joesph Mwaisango akiwa na Blogger Rashid Mkwinda wakifuatilia kwa umakini mafunzo
 Baadhi ya Bloggers wakifuatilia Jambo kwa umakini
 Kutoka kushoto ni Fredy Anthony ambaye anatokea Blogs za Mikoa pamoja na Muwakilishi wa Full Shangwe Blog
 Kutoka kushoto ni Dotto Kahindi kutoka Blog ya Tabia Nchi akiwa na Adela Kavishe

 Mkurugenzi wa Google Africa Joe Mucheru akitoa mada wakati wa Mafunzo kwa Bloggers
 Mmoja ya watoa Maada katika Maswala ya Mitandao ya Kijamii Liz Wachuka akizungumza jambo wakati wa Mafunzo kwa Bloggers.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma akijibu Maswali ambayo yaliulizwa na Bloggers wakati wa semina hiyo
 Meza kuu wakifuatilia Mada kwa umakini
 Liz Wachuka Akijibu maswali yaliyo ulizwa na Bloggers
 Afisa Habari wa TCRA Doris Saivoye  akizungumza Jambo wakati wa Mafunzo kwa Bloggers.

Wabunge wa Nigeria wapigana bungeni


Wabunge wa bunge la waakilishi Nigeria wamerushiana ngumi wakati wa vikao vya Jumanne baada ya kuzuka bungeni suitofahamu kuhusu mrengo wa wabunge waliojitenga na chama tawala. Taarifa hizi ni kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo.
 
Chama tawala cha PDP kimekuwa kikikumbwa na mgogoro wa ndani kwa muda sasa
Kituo kimoja cha kibinafsi cha televisheni, pamoja na vituo vingine vilionyesha picha za mbunge mwanamke akimtosa kidole usoni kwa ghadhabu mbunge mwenzake wakati mbunge mwanamume akionekana akichukua kiti nusura kumgonga mwenzake.
Wabunge wengine walionekana wakipigana ngumi.
Mgogoro inasemekana ulianza baada ya