Ijumaa, 27 Septemba 2013

WAKUU WA USALAMA KUHOJIWA KENYA


Maafisa wakuu wa ujasusi wametakiwa kufika mbele ya kamati ya ulinzi ya bunge ili kuhojiwa kuhusu mashambulizi ya kigaidi dhidi ya jumba la Westgate mjini Nairobi.

Taarifa kwenye vyombo vya habari nchini humo zinaonyesha kuwa hali ya kulaumiana imeanza kuibuka huku mashirika ya usalama yakinyosheana kidole.

TANZANIA NA MATUKIO YA WIKI

RAIS JAKAYA M. KIKWETE NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA OMAN NDUGU YOUSEF BIN ALAWI ABUDULLAH WAKIBADILISHANA MAWAZO HUKO NEW YORK MAREKANI SEP 26/2013
WAZIRI MKUU MIZENGO AKISALIMIANA NA WANAKIJIJI CHA ENGOSERO KATIKA WILAYA YA NGORONGORO SEP.26.2013
WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI JANGWANI WAKIWA KATIKA MAZOEZI
SIKU YA UZINDUZI WA WIKI YA NENDA KWA USALAMA ZILIZOFANYIKA MITAA YA MWEMBEYANGA WILAYA YA TEMEKE JIJINI DAR ES SALAAM SEP.23.2013
 YANGA 2-3 AZAM
BEKI WA AZAM ERASTO NYONI (KUSHOTO) NA KIUNGO WA YANGA  HARUNA NIYONZIMA LIGI KUU TANZANIA JUMAPILI
WAFANYAKAZI WA MANISPAA YA ILALA WAKITIMIZA MAJUKUM YAO JIJINI DAR ES SALAAM

HII IMENIFURAHISHA SANA NA NINA HAKIKA UJUMBE UMEFIKA

UKITAKA KUUNGANISHA UMEME TANZANIA JIANDAE KISAIKOLOJIA

Ukitaka kuunganishiwa umeme nchini Tanzania ni lazima uache kazi ufanye kazi  ya kuunganishiwa huduma hiyo. Hii inatokana na ukweli kwamba kama unataka umeme, huna budi kuacha unachofanya na kutumia muda mwingi kukamilisha huduma hiyo tena  kwa gharama kubwa.

SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA INA MAPUNGUFU "WARIOBA"


Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu, Joseph Warioba akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Makamu wake, Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino Ramadhani 
 
Jaji Warioba

Wakati wananchi wa kada mbalimbali wakishinikiza Rais Jakaya Kikwete kutokusaini Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba 2013, kwa maelezo kuwa una kasoro, Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba naye amesema sheria ina upungufu.

KWA UFUPI

KENYA YAMSAKA SAMANTHA LEWTHWAITE

Polisi wa kimataifa Interpol, wamemuweka mwanamke aliyeshukiwa kuongoza mashabulizi ya kigaidi nchini Kenya raia Muingereza Samantha Lewthwaite, kwenye orodha ya watu wanaosakwa
 sana duniani.

UN YAJADILI AZIMIO KUHUSU SYRIA
 
 Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa linajadili rasimu ya azimio kuhusu silaha za kemikali za Syria baada ya Marekani na Urusi kukubali mapendekezo ya azimio hilo.

AFUNGWA MIEZI SITA JELA KWA WIMBO WA MATUSI TUNISIA
 
Msanii wa kizazi kipya nchini Tunisia, Ahmed Ben Ahmed, anayejulikana kwa jina la kiusanii, Klay BBJ, amehukumiwa jela kwa miezi sita kwa kuwatusi maafisa wakuu kupitia kwa  
muziki wake.