Ndege iliyokuwa imewabeba watu 27 imeanguka baada ya
kukumbwa na hitilafu ya injini, muda mfupi baada ya kuruka kutoka uwanja
wa ndege mjini Lagos.
Duru zinasema kuwa watu 5 wamefariki huku
shughuli ya uokozi ikendelea na mtu mmoja akipata matibabu kwa majeraha
mabaya aliyopata.
Ndege hiyo ya shirika la ndege la Associated
Airlines, iliyokuwa na uwezo wa kubeba watu 30 ilianguka muda mfupi tu
baada ya kuruka na kulipuka.
Aidha ilikua inaelekea mjini Akure Kusini
Magharibi mwa nchi, kwa mujibu wa msemaji wa shirika la udhibiti wa
safari za angani nchini humo.