Melfu ya watu nchini Afrika Kusini walijiunga na zaidi ya viongozi 90 wa dunia kwa ibada maalu ya hayati Nelson Mandela.
Ibada hiyo ilifanyika katika uwanja wa michezo wa FNB mjini Johannesburg
Rais wa Marekani Barack Obama alisema kuwa Mandela ameifunza dunia
umuhimu wa kutenda badala ya kusema sana pamoja na umuhimu kwa kuwa na
mawazo mazuri ingawa ya kutenda.
Alipoondoka ukumbini, Rais Obama aliamkuana na Rais wa Cuba, Raul Castro
ishara kubwa sana kati ya marais wa nchi hizo mbili ambazo zimekuwa
zikizozana kwa zaidi ya nusu karne
Mandela alifariki Alhamisi iliyopita, akiwa na umri wa miaka 95. Nchi
hiyo imeandaa shughuli mbali mbali za kumuenzi Mandela kabla ya kuzikwa
Jumapili.
Aliyekuwa anaendesha hafla hiyo Cyril Ramaphosa alisema kuwa safari ndefu ya Mandela imekamilika na sasa anaweza kupumzika
Askofu mkuu wa Afrika Kusini Desmond Tutu,mmoja wa waliopigana vita
dhidi ya ubaguzi wa rangi, alisema Mandela alikuwa mtu wa kupatanisha
watu pindi alipoondoka gerezani. 'Tumepata afueni kuwa matatizo yake ya
kiafya yamekwisha' alisema Tutu
Ibada hii ilikuwa moja ya mkusanyiko mkubwa wa viongozi wa dunia
kushuhudiwa hivi karibuni. Katika hotuba yake , katibu mkuu wa Umoja wa
mataifa Ban ki Moon, alisema kuna huzuni tele kwa umma kumpoteza Mandela
Kulikuwa na hofu kuwa watu wangeamrishwa kurejea nyumbani , lakini mvua kubwa ilisababisha sehemu za uwanja kuwa bila watu
Mjane wa Mandela Graca Machel, alishangiliwa sana alipoonyeshwa kwenye skirini kubwa akiingia uwanjani
Pia kulikuwa na shangwe na vigelegele huku watu wakiimba Winnie Winnie
Madikizela Mandela aliyekuwa mkewe Mandela. Alimpa pambaja na kumbusu
Graca
Hata hivyo Rais Jacob Zuma alizomewa mara kwa mara ilipokuwa zamu yake kuhutubia wananchi.
Tangu kifo cha Mandela mji wa Johannesburg umekuwa ukishuhudia mvua
lakini hiyo haikuwakatiza tamaa wananchi waliofurika uwanja wa michezo
wa FNB
Umati wa watu uliimba na kucheza kama ishara ya kuenzi maisha ya Mandela
Ambao hawakuweza kufika uwanjani waliiona ibada hiyo kwenye televisheini zao nyumbani kote nchini Afrika Kusini
Mandela atazikwa siku ya Jumapili tarehe 15
Zaidi ya maraisa tisini
wameungana na wananchi wa Afrika Kusini katika misa ya wafu ya Nelson
Mandela na kusimulia kumbukumbu zao kwa Shujaa huyo wa Afrika.
Akiongea kwenye mkusanyiko huo mjini Soweto,
Rais wa Marekani Barack Obama alimtaja Mandela kuwa shujaa na mkombozi
wa Afrika na shujaa shupavu kuwahi kuonekana katika karne ya ishirini.Alisema maisha ya Mandela lazima yawe mfano mzuri kwa dunia nzima hasa vita alivyopigania kuhakikisha utu wa watu unaheshimiwa.
Jamaa za Mandela wamemtaja baba yao Mandela kama mtu aliyetaka watu kuwa sawa.
Mmoja wa wajukuu wa Mandela alikariri shahiri la kusisitiza mshikimano wa watu. Obama alishangiliwa ingawa Rais Jacob Zuma anayehutubia wananchi alizomewa mara kwa mara.
Uwanja ambako misa hiyo inafanyika, haukujaa watu kutokana na mvbua kubwa iliyonyesha.
Maelfu ya watu wamehudhuria misa hiyo katika uwanja wa FNB.
Afrika Kusini imeandaa shughuli mbali mbali za kumuenzi Mandela kabla ya siku ya kuzikwa kwake nchini Afrika Kusini siku ya Jumapili.
Misa ya leo ni moja ya mikusanyiko mikubwa ya viongozi wa kimataifa iliyoshuhudiwa nchini humo katika miaka ya hivi karibuni.
Viongozi wengine Watakaohudhuria misa ya wafu ya Mandela:
Watu wengi walikaidi hali mbaya ya hewa ambapo mvua kubwa imenyesha huku wakikusanyika uwanjani humo wakisubiri kwa muda mrefu kabla ya misa hiyo kuanza muda mfupi uliopita.
Waliohudhuria misa hiyo wamesemekana kuwa wenye furaha wakiimba nyimbo na kutaja jina la Mandela kwa shangwe unaweza kudhani ni mkutano wa kisiasa.
Misa hiyo itafanyika katika uwanja ambako Nelson Mandela alionekana kwa mara ya mwisho hadharani.
Misa hiyo itaonyeshwa kwenye skrini kubwa nje ya uwanja ili kuzuia msongamano wa watu.
Mandela alifariki akiwa na umri wa miaka 95 na kwa wengi yeye ni shujaa na mkombozi wa Afrika Kusini.