Jumanne, 31 Desemba 2013

MOJA YA MATUKIO YA KUSIKITISHA SANA KWA MWAKA 2013 NI MAUAJI YA NGOME YA HEZBOLLAH

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/19/131119115932_blast_afp-1.jpg 
Takriban watu 22 wameripotiwa kufariki katika milipuko miwili ambayo ililenga ubalozi wa Iran mjini Beirut, mji mkuu wa Lebanon
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/19/131119115934_blast_afp-2.jpg
Afisaa mmoja mkuu katika ubalozi huo Ebrahim Ansari alikuwa miongoni mwa waliofariki. Maafisa wamesema kuwa idadi ya waliofariki huenda ikaongezeka
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/19/131119115936_blast_ap-3.jpg
Picha nyingi za mashambulizi hayo zilionyesha magari yakiteketea pamoja na miili ya watu ikiwa imetapakaa kwenye barabara za eneo hilo. Majumba pia yaliharibiwa vibaya
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/19/131119115938_blast_ap-4.jpg
Iran inaunga mkono kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Hezbollah ambalo limewapeleka wapiganaji nchini Syria kuunga mkono serikali ya Rais Bashar al Assad. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/19/131119115940_blast_afp-5.jpg
Duru zinasema kuwa moja ya milipuko hio, ilisababishwa na mshambuliaji wa kujitoa mhanga, wakati shambulio la pili lilitokana na bomu lililokuwa limetegwa ndani ya gari. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/19/131119115942_blast_reuters-6.jpg
Shirika la habari la Reuters linanukuu kituo cha televisheni cha CCTV, kikionyesha mwanamume mmoja akikimbia kutoka katika ubalozi wa Iran na kisha kujilipua
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/19/131119115944_blast_reuters-7.jpg
Balozi wa Iran nchini Beirut alithibitisha kifo cha bwana Ansari, ingawa haijulikani ikiwa alikuwa ndani ya ubalozi au katika jengo jirani 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/19/131119115946_blast_ap-8.jpg
Syria imelaani vikali mashambulizi hayo. Mgogoro wa kisiasa nchini Syria umechochea kuongezeka kwa hali ya wasiwasi nchini Lebanon. 

HAYA NI BAADHI TU YA MATUKIO AMBAYO FREE MEDIA TO BLOGS INAJARIBU KUKUHABARISHA

Hakuna maoni: