Takriban watu 22 wameripotiwa kufariki katika milipuko miwili ambayo ililenga ubalozi wa Iran mjini Beirut, mji mkuu wa Lebanon
Afisaa mmoja mkuu katika ubalozi huo Ebrahim Ansari alikuwa miongoni mwa
waliofariki. Maafisa wamesema kuwa idadi ya waliofariki huenda
ikaongezeka
Picha nyingi za mashambulizi hayo zilionyesha magari yakiteketea pamoja
na miili ya watu ikiwa imetapakaa kwenye barabara za eneo hilo. Majumba
pia yaliharibiwa vibaya
Iran inaunga mkono kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Hezbollah ambalo
limewapeleka wapiganaji nchini Syria kuunga mkono serikali ya Rais
Bashar al Assad.
Duru zinasema kuwa moja ya milipuko hio, ilisababishwa na mshambuliaji
wa kujitoa mhanga, wakati shambulio la pili lilitokana na bomu
lililokuwa limetegwa ndani ya gari.
Shirika la habari la Reuters linanukuu kituo cha televisheni cha CCTV,
kikionyesha mwanamume mmoja akikimbia kutoka katika ubalozi wa Iran na
kisha kujilipua
Balozi wa Iran nchini Beirut alithibitisha kifo cha bwana Ansari, ingawa
haijulikani ikiwa alikuwa ndani ya ubalozi au katika jengo jirani
Syria imelaani vikali mashambulizi hayo. Mgogoro wa kisiasa nchini Syria
umechochea kuongezeka kwa hali ya wasiwasi nchini Lebanon.
HAYA NI BAADHI TU YA MATUKIO AMBAYO FREE MEDIA TO BLOGS INAJARIBU KUKUHABARISHA
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni