Jumanne, 12 Novemba 2013

MJADALA WA USAWA WA KIJINSIA KWA PICHA ULIOFANYIKA KENYA KUPITIA PROGRAMU YA SEMA KENYA

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/10/131110121041_skwomenshow_pict5_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Kwa mara ya kwanza kabisa tangu Kenya kujipatia uhuru, idadi ya wanawake imeongezeka kwa kiwango kikubwa katika bunge.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/10/131110120053_skwomenshow_pict2_976x549_bbc_nocredit.jpg
Katiba mpya inapiga marufuku ubaguzi wa aina yoyote dhidi ya wanawake. Hivi nafasi ya wanawake ya kuongoza, kumiliki mali na kuendeleza jamii katika njia ya kipekee, inalindwa katika katiba.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/10/131110115917_skwomenshow_pict_1_976x549_bbc_nocredit.jpg
Kwa mara ya kwanza kwa miaka hamsini ya kuwa jamhuri, Kenya imewapa wanawake uongozi katika wizara kuu kama vile wizara ya mambo ya kigeni na wizara ya ulinzi.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/10/131110120640_skwomenshow_pict4_976x549_bbc_nocredit.jpg
Taasisi kama mahakama ya juu na tume ya umma pia zinafuata katiba katika kuwapa wanawake nafasi za kipekee.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/10/131110120243_skwomenshow_pict3_976x549_bbc_nocredit.jpg
Mjadala huu ulijadili iwapo sera hizi zimefanikiwa katika mfumo wa serikali za ugatuzi.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/10/131110121805_skwomenshow_pict7_976x549_bbc_nocredit.jpg
Wanawake walio uongozini walielezea changamoto wanayoyapata kazini na kujibu maswali kuhusiana na mchango wao.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/10/131110121556_skwomenshow_pict6_976x549_bbc_nocredit.jpg
Joan Birika, Bobby Mkangi, Emma Mburu na Priscilla Nyokabi walikuwa kwenye jopo. Edwin Saka ni mojawapo wa wageni maalum walioalikwa. Msimulizi ni Joseph Warungu.
 
Katiba mpya ya Kenya inatilia maanani usawa wa wanawake katika vitengo tofauti ya maisha. Mjadala huu ulimulika mchango wa wanawake viongozi na kuchambua jinsi sera za katiba mpya zinafanikiwa kuendeleza usawa wa kijinsia.