Jumatatu, 23 Septemba 2013

hali bado ni mbaya sana huko Kenya


Jengo la Wastgate likifuka moshi
 
vikosi vya usalama vyaingia

JAMAA WANAOITIKISA KENYA NDIYO HAWA HAPA


 Wapiganaji wa Al Shabaab 
Hizi ni silaha za Al Shabaab walizonasa wanajeshi wa AU
Kundi la wapiganaji wa kisomali la al-Shabaab,limevamia jumba la kifahari lenye maduka na mikahawa nchini Kenya. Al Shabaab lenya mizizi yake nchini Somalia, limeweza kuondolewa kutoka miji mikubwa ya Somalia ikiwemo Mogadishu na sehemu zengine za Somalia , ingawa bado linasalia kuwa tisho kubwa kwa kanda nzima.

Raisi wa Kenya Uhuru Kenyata amewaomba wakenya kuwa watulivu

Raisi wa Kenya uhuru kenyata amewaomba wakenya kuwa watulivu wakati Huu   ambapo vikosi vya usalama vinafanya jitihada kuhakikisha watu waliobaki kaitka jengo la WEST GATE wanaokolewa huku akisisitiza kuwa serikli yake itapambana na magaidi popote pale walipo.
Rais Kenyatta ametoa kauli hiyo  wakati akihutubia taifa jana  juu ya tukio la kuuwawa kwa watu wapatao 68 na wengine zaidi ya 200 kujeruhiwa,ambapo alitoa hotuba hiyo  mbele ya ya viongozi mbalimbali  wa kisiasa akiwemo aliekuwa waziri mkuu wan chi hiyo  raila odinga. Aidha rais uhuru kenyatta amesema vita hii  haihusu dini yoyote wala kabila lolote bali ni vita ya ugaidi.
Tukio hilo limetokea tangu jumamosi sept 21 ambapo mpaka sasa bado kuna watu wameshikiliwa na wavamizi hao ndani ya jengo hilo la WEST GATE MALL lakini serikali ya kenya imewahakikishia wananchi kuwa inafanya jitihada zote kuwaokoa watu walioko ndani ya jengo hilo.
 
Askari wa Kenya wakiwa katika harakati za uokoaji

KENYA BADO HALI NI MBAYA MAUAJI BADO YANAENDELEA


 


Jeshi la Kenya linasema kuwa limedhibiti jengo hilo ingawa hali bado ni mbaya
 
Wakenya waliofanikiwa kuondoka katika jengo la Westgate kwa usaidizi wa polisi

Huku hali ya mshikemshike ikiendelea kushuhudiwa katika jengo la Westgate lenye maduka, ufyatulianaji risasi umesikika ndani ya jengo hilo lenye maduka na mikahawa zaidi ya themanini.
Wapiganaji wa Al shabaab wamewateka nyara raia ambao idadi yao haijulikani. Walikuwemo ndani ya jengo wakiendelea na shughuli zao kuanzia Jumamosi mchana wakati wapiganaji wa Al shabaab walipowavamia na kuanza kufyatua risasi kiholela.