Jeshi la Kenya linasema kuwa limedhibiti jengo hilo ingawa hali bado ni mbaya
Wakenya waliofanikiwa kuondoka katika jengo la Westgate kwa usaidizi wa polisi
Huku hali ya mshikemshike ikiendelea kushuhudiwa
katika jengo la Westgate lenye maduka, ufyatulianaji risasi umesikika
ndani ya jengo hilo lenye maduka na mikahawa zaidi ya themanini.
Wapiganaji wa Al shabaab wamewateka nyara raia
ambao idadi yao haijulikani. Walikuwemo ndani ya jengo wakiendelea na
shughuli zao kuanzia Jumamosi mchana wakati wapiganaji wa Al shabaab
walipowavamia na kuanza kufyatua risasi kiholela.