Wanajeshi wa Misri wanashika doria katika baadhi ya miji mikubwa ambapo
maandamano yanafanyika kupinga au kuunga mkono kura ya maoni kuhusu
rasimu ya katiba itakayofanyika siku ya Jumamosi
Wanajeshi wameruhusiwa kuchukua hatua dhidi ya waandamanaji watakaozua rabsha
Katika mji wa Alexandria ambao ni mji wa bandarini , wananchi asubuhi ya
leo walianza kuandamana kuipinga katiba lakini polisi walikuwepo
kuwazuia
Maandamano yalianza baada ya mhubiri mmoja katika msikiti mmoja kuwashauri waumini kupigia kura ya ndio katiba
Waandamanaji mahasimu hawajachoka tangu mapema wiki hii walipoanza
kuandamana wakipinga katiba ya rais Morsi huku wengine wakiiunga mkono
Waandamanaji wengi wanasema kuwa wataipinga katiba hiyo
Hawakutaka kuondoka hata baada ya jeshi kuamrishwa kuwakamata wale
watakaokiuka sheria, agizo ambalo wengi wamelitafsiri kama Misri kurejea
katika enzi ya kidikteta
Wengi walikesha katika medani ya Tahrir kuelezea kero lao dhidi ya katiba mpya