Umoja wa Mataifa umesema robo
tatu ya Wapalestina waliouawa kwa mashambulizi ya ndege yanayoendelea
yanayofanywa na Israel huko Gaza ni raia wa kawaida.
Maafisa wa Palestina wanasema raia mia moja ishirini wameuwawa tangu mashambulio kuanza.
Israel imesema inafanya mashambulio hayo, ili
kujaribu kuwazuia wapiganaji wa Hamas, ambao wamekuwa wakirusha mamia ya
makomborakwenye ardhi ya Israel.
Israel inalaumu wapiganaji wa Hamas kwa kutumia raia kama ngao kwa kuweka vifaa vya kivita kwenye makazi ya watu.
Professor Manuel Hassassian mwakilishi wa
Palestina nchini Uingereza, ameiambia BBC, Israel kwa kuwalenga Hamas
hukutakwepa kuwadhuru raia.
Alisema idadi kubwa ya raia wamekufa siyo sababu Hamas inajificha kati ya raia, yaani inawatumia raia kama kinga.
Gaza, kwa hivo wanapowalenga Hamas
kamawanavosema, wanawalenga wa-Palestina wote. Siyo Gaza peke
yake.Katika Ufukwe wa Magharibi piya, Israil imekuwa ikiwauwa kiholela,
na huko hakuna makombora yaliyolegwa dhidi ya Israil" Alisema
Hassassian.