Alhamisi, 19 Septemba 2013

HABARI ZA HIVI PUNDE:Vikosi vyakabiliana na wapiganaji Misri




Majeshi ya Misri yameraukia kwenye mji wa Kerdasah kuondoa kile wanachosema ni makundi ya kigaidi
Vikosi vya usalama nchini Misri, vimekabiliana na wapiganaji wa kiisilamu baada kuingia katika mji ulioko viungani vya mji mkuu Cairo wa Kerdasah.
Duru zinasema kuwa wanajeshi hao waliingia mjini humo ambako polisi 11 waliuawa mwezi jana kukabiliana na kile walichokiita magaidi.
Mauaji hayo yalitokea wakati aliyekuwa rais Mohammed Morsi alipoondolewa mamlakani na jeshi.

ICC yataka Marekani imkamate Rais Bashir




Bashir ametishia kumfukuza balozi wa Marekani nchini Sudan

Siku mbili baada ya Rais wa Sudan kuiomba Marekani kumpa Visa ya kusafiri nchini humo kuhudhuria mkutano wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York, wito umetolewa kwa taifa hilo kumkamata Bashir na kumkamabidhi kwa mahakama ya ICC.
Mkutano huo utafanyika wiki ijayo.

MATOKEO LIGI YA MABINGWA ULAYA 18/09/2013

Schalke 04 3-0 Steaua

Chelsea 1-2 Basel

 Marseille 1-2 Arsenal

Napoli 2-1 Dortmund

Austria Wien 0-1 Porto

Atletico 3-1 Zenit

Milan 2-0 Celtic

 Barcelona 4-0 Ajax