Jumatano, 27 Novemba 2013
AFRIKA KATIKA PICHA
Shabiki wa Tunisia aliyejipaka rangi ashauriana na mtani wake wa Cameroon baada ya mechi jijini Younde huko Cameroon.
Ilikua ni mechi ya marudiano ya kufuzu kwa kombe la dunia ambapo timu ya
“the Lions” walishinda kwa mabao 4-1 na kujikatia tikiti ya kushiriki
kombe la dunia mwaka ujao nchini Brazil. Kulikua na karamu na sherehe
baadaye mjini Younde.
Algeria pia walijikatia tikiti kucheza Brazil baada ya kucheza mechi ya
marudiano, awamu ya pili siku ya jumanne kwa kuilaza Burkina Faso bao
1-0 ,ambayo ilikua furaha kwa mashabiki katika mji mkuu wa Algiers.
Kulikua na mvua mkubwa Afrika Kusini Magharibi mwa mkoa wa Cape wikendi
na kusababisha mafuriko sehemu kadhaa. Matofali yaliyotengenezwa
yanavunjika pakiwa na maji mengi
Maonyesho ya kudumu ya nyaraka kuhusu maisha ya Nelson Mandela
yalifunguliwa siku ya jumatatu katika kituo cha makumbusho cha Nelson
Mandela jijini Johannesberg. Hivi ni vitabu vya Nelson Mandela
alivyokuwa navyo gerezani katika kisiwa cha Robben alikokua amefungwa
kwa juhudi zake za kupinga ubaguzi wa rangi. Aliachiliwa baada ya miaka
27, mwaka wa 1990 na kuwa rais wa kwanza wa nchi hiyo kuchaguliwa kwa
miaka nne kupitia democrasia
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe na mkewe Grace wahudhuria sherehe ya
mahafali ya binti wao Bona katika chuo kuku huko Singapore Jumamosi.
Pia Jumanne,kijana mmoja katika soko la Gorongosa katikati mwa Msumbiji anajikinga kwa kutumia mwavuli.
Siku iliyopita, mwandamanaji nchini Tunisia avaa bereti na beji
inayoonyesha picha ya aliyekuwa kiongozi wa Iraq Saddam Hussein,wakati
wa maandamano dhidi ya muungano wa kiislamu unaoongozwa na chama tawala
cha muungano katika mji mkuu Tunis.
Siku hio,vijana wawili wadogo wanalima shamba lililoko kando ya barabara
kuu inayounganisha jiji kuu la Mogadishu na Baido lililo karibu na
shamba lenye rotuba karibu na Afgoye inayojulikana kwa mavuno bora
nchini Somali
Walinzi wa Somal, wakishika doria katika fuo za bahari mjini Bosasso, katika eneo lililojitenga na Somalia la Puntland
Katika kijiji kimoja Kaskazini mwa Kenya ,kijana asimama kando kando na
fahali aliyenona kabla ya kuwasilishwa kwa kamishna mkuu wa Uingereza
kutoka kwa jamii ya Wasamburu ya Nanuyak kama zawadi ili kusheherekea
kuzaliwa kwa mwana mfalme George Mwakani.
Mji mkuu wa Kenya Nairobi uliandaa maonyesho ya magari siku ya
Jumapili,huku gari aina ya Peugeot 203 ya mwaka 1959 ikiwemo kati ya ya
magari 70 kwenye maonyesho katika uwanja wa mashindano wa Ngong.
Kijana mmoja katika jiji kuu la Mali Bamako,ajaribu kuyagonga mapera
kutoka kwa mti siku ya jumatano. Uchaguzi wa kiubunge utafanyika nchini
humo jumapili.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)