Brazil ni nchi yenye urathi mkubwa wa kiafrika , na ni kwa sababu ya
historia biashara ya utumwa. Mamilioni ya watu nchii Brazil wana asili
ya kiafrika. Lakini je maisha yako vipi kwa waafrika waliohamia nchini
humo aidha kufanya kazi au kusoma? Mwandishi wa BBC Manuel Toledo
alikuwa nchini Brazil na alikutana na baadhi yao.
Victor Macaia (katikati) na mkewe Melanito Biyouha, wanatoka nchini
Cameroon. Walifungua mgahawa wao wa chakula cha kiafrika mjini Sao Paulo
miaka sita iliyopita. "mwanzoni asilimia 80 ya wateja wetu walikuwa
waafrika, lakini sasa asilimia 90 ni wageni na wenyeji wa-Brazil.
Chakula chetu chote ni cha kiafrika,'' alisema mwanamume huyo.
ilikuwa vigumu sana kwetu kaunza biashara hii. Wakati mwingine huna
nyaraka zinazotakikana, pesa na gharama au hata uzoefu wa kazi.
Inachukua muda, kufanya kazi muda wa kupitia masaibu na pia muda wa
kupata faida. Lakini sasa tuko vizuri sana,'' Bwana Macaia aliongeza
kusema.
Ale Fall Sow, kutoka Senegal ni mhadhiri katika chuo kikuu Brasilia. ''
Nimeishi nchini Brazil kwa miaka 26. Nilikuja hapa kwa mara ya kwanza
kama mwanafunzi. Mke wangu na watoto wangu ni wa-Brazil. Wanapenda
Afrika na wao huenda huko kwa likizo mara kwa mara.
Nchini Brazil kuna asili mbali mbali. Kwa sababu za kihistoria, kuna
watu weusi Kaskazini mwa nchi,'' asema mwanafunzi Tresor Mukendi Muteba,
kutoka Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo. Nahisi kama niko nyumbani
hapa. Utamaduni wa Brazil unafanana na utamaduni wa Afrika. Kwa sababu
ya hilo, wakati mwingi mimi huhisi kama niko Afrika. ''
"nimekuwa nchini Brazil, kwa miezi mitatu au minne, asema Uju Juliana
kutoka Nigeria. "Brazil ni mahala pazuri sana. Wanawake wa kiafrika sisi
huhisi kama tuko tu nyumbani. Ningesema kwamba hapa Brazil watu
huheshimu wanawake zaidi hata kuliko nchini mwangu. ''
Lacine Sanogo kutoka Ivory Coast anasema: "nilikuja hapa kucheza soka.
Lakini maisha hapa ni magumu hasa kwetu raia wa kigeni. Hatupewi nafasi
za kutosha, Nimekuwa nikicheza katika ligi ya daraja ya pili lakini hivi
karibuni nilipata jeraha la goti. Ambavyo soka inachezwa Afrika ni
tofauti sana na inavyochezwa hapa. Nimejifunza mambo mengi. ''
El Hadji Omar, kutoka Senegal anauza mali yake barabarani. "nilikuja
Brazil miezi miwili iliyopita kutafuta kazi. Sijui nitakuwa hapa kwa
muda gani lakini naipenda nchi hii. Kama katika sehemu nyingine yoyote
duniani, kuna watu wazuri na wabaya. Lakini watu nchini Brazil ni kama
tu sisi waafrika. ''
nimekuwa hapa kwa miezi minne,'' asema Yussif Muhktar kutoka Ghana.
"nilikuja hapa kufanya kazi. Wa-Brazil ni watu wazuri sana na wanapenda
kila mtu na ninashukuru kwa hilo. ''
Serge Tchieguen kutoka Cameroon anasema: "ninafanya kazi ya usimamizi wa
michezo, na hiyo ni sekta ambayo imekomaa sana hapa Brazil. Nimejifunza
mengi. Nadhani nimebadilika na kuwa bora zaidi tangu kuja hapa miaka
minne iliyopita kwa namna ambavyo nafikiria na pia kufanya kazi. ''
Ifeanyi Okafor, kutoka Nigeria, ni mhandisi katika kampuni ya kuchimba
mafuta. "ninaishi eneo linaljulikana kama Macae karibu na Rio de
Janeiro. Nimeishi hapo kwa miaka miwili. Ni mara ya kwanza kwangu
kufanya kazi nje ya Afrika. Nimefurahi sana na nina marafiki wengi sana
hapa Brazil.''
endelea kufuatilia matukio mbalimblia kupitia blog yako ya kijanja