Jumapili, 13 Julai 2014
HII NI ZAIDI YA UJUAVYO....UGONJWA WA EBOLA NI JANGA KWA AFRIKA HASA MAGHARIBI
Shirika la Afya Duniani (WHO) limetaka "hatua za dharura" zichukuliwe
ili kudhibiti kuzuka kwa ugonjwa wa Ebola Africa magharibi, ambao
umewauwa zaidi ya watu 400. Ugonjwa huu ndio mkubwa zaidi duniani kuzuka
kutokana na visa vyake, vifo na kusambaa katika maeneo.
Kumekuwepo na visa visivyopungua 600 nchini Guinea - ambapo ugonjwa huo
ulianza kuzuka miezi minne iliyopita mjini Guekedou, ambao ulikuwa kituo
kikubwa cha biashara, kilichowavutia wauzaji na wanunuzi kutoka mataifa
kadhaa.
Shirika la misaada la Medecins Sans Frontieres (MSF) tayari limeonya
kuwa kusambaa kwa ebola hakuwezi kudhibitiwa. Shirika hilo lina
wafanyikazi 300 wa kimataifa na vile vile wa kitaifa wanaofanya kazi
nchini Guinea, Sierra Leone pamoja na Liberia, ambako ugonjwa huo
unaenea kwa kasi. Mataifa mengine yako
macho iwapo ugonjwa huo utasambaa
Zaidi.
Kwa mujibu wa shirika la afya duniani, Ebola ni ugonjwa unaosababishwa
na virusi na ambao dalili zake za mwanzo huweza kuwa kushikwa na homa,
kuwa dhaifu, kuumwa na misuli na kuumwa na koo. Na huo ni mwanzo tu:
kile kinachofuata ni kutapika, kuendesha na -wakati mwingine- kuvuja
damu.
Virusi hivyo huenea kwa haraka sana, na hadi sasa hakuna dawa
inayotambulika kuweza kuvitibu, kwa hivyo wanaotoa huduma za matibabu
huvalia mavazi yanayowakinga kutokana na kuambukizwa kwa ugonjwa huo.
Kulingana na uzito wa athari za ugonjwa huo, hadi kufikia asilimia 90 ya
walioambukizwa huaga dunia. Anayehakikisha usafi anawakaribia wagonjwa
wanaosubiri matokeo baada ya kupimwa damu.
Vipimo vya maabara vitaonyesha kwa saa kadhaa iwapo sampuli ya damu inayopimwa ina virusi vya Ebola au la.
Baada ya kukumbana na virusi hivyo katika sehemu iliyotengwa, mavazi na viatu husafishwa kwa Chlorine.
Kando na kutoa huduma za kliniki, kikundi hicho hutoa hamasisho kuhusu
ugonjwa huo. Hapa Touloubengo, familia tano ambazo nyumba zao zilikuwa
zimesafishwa siku kadhaa zilizopita kutokana na kuaga dunia kwa mmoja
wao wanakabidhiwa magodoro.
Sio kila mtu aliye salama. Hapa familia ya Kinda Marie Kamano, akiwemo
dadake (katikati), pamoja na wanajamii wengine wanahuzunika katika
mazishi yake karibu na nyumba yake.
Takriban watu 600 wamefariki kutokana na homa ya Ebola Afrika Magharibi
Endelea kufuatilia
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)