Jumatatu, 14 Oktoba 2013

ZIJUE TIMU ZA AFRIKA ZITAKAZOKWENDA KUTIKISA KOMBE LA DUNIA BRAZIL

Nigeria Super Eagles
Nigeria Super Eagles

Ushindi wa Super Eagles ya Nigeria ugenini dhidi ya Ethiopia umeipa matumaini ya kushiriki kombe lijalo la dunia.
Ethiopia ilipata goli la kuongoza kunako dakika ya 56 kupitia mchezaji Asefa.
Bao hilo halikukaa kwa muda mrefu.kunako dakika ya 67 mkwaju uliopigwa na Emanuel Emenike uliishia langoni na kuwa 1-1.
Ethiopia watajilaumu wenyewe kwa kushindwa kutumia nafasi kadhaa walizopata na pengine waliponea chupuchupu kunako dakika 77 ambapo mkwaju wa Nigeria ulirudishwa na mlingoti wa lango.
Goli la ushindi la Nigeria limepatikana kwenye dakika ya mwisho kwa njia ya penalty iliyofungwa kimiani na Emmanuel Emenike na kupalilia njia kwa bingwa hao wa Afrika ya kwenda Brazil.
Didier Drogba
Didier Drogba(kulia)

Ushindi wa Ivory Coast dhidi ya Senegal umekuwa hatua muhimu ya kuelekea katika fainali za kombe la dunia.
Mabao 3 yaliyofungwa na washambuliaji Didier Drogba, Gervinho na Salomon Kalou yametosha kuiongezea matumaini Ivory Coast ya kushiriki fanali za kombe la dunia mwaka ujao nchini Brazil.
Goli la kufutia machozi upande wa Senegal lilifungwa kimiani na mshambuliaji wa NewCastle Papiss Demba Cisse.
Mechi ya mkondo wa pili itachezwa mwezi ujao nchini Morocco kwa sababu Senegal inatumikia adhabu ya kutochezea kwenye uwanja wa nyumbani.

Burkinafaso 3 Algeria 2

Penalti ya dakika za mwisho iliyopewa Burkinafaso katika mazingira ya kutatanisha iliiwezesha timu hiyo kupata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Algeria.
Hadi dakika ya 85 matokeo yalikuwa magoli 2-2 kabla ya Burkinafaso kupata penalti iliyowawezesha kuondoka na ushindi mdogo.

Hakuna maoni: