Mchali akionyesha mkono aliokatwa
Baada ya kuwa katika mapenzi na mwanaume huyo kwa zaidi ya miaka 17,
wakipendana na kuitana majina yote mazuri unayoyajua yakiwamo kuambiwa
‘mpenzi wangu nakupenda, nikinywa maji nakuona kwenye glasi’…leo mapenzi
yamegeuka shubiri.
Mkasa wa mwanamke kukatwa mkono
Ilikuwa Agosti 7, mwaka huu, saa mbili usiku.
Ilikuwa ni siku iliyobadili historia ya maisha yake. Baada ya kuwa
katika mapenzi na mwanaume huyo kwa zaidi ya miaka 17, wakipendana na
kuitana majina yote mazuri unayoyajua yakiwamo kuambiwa ‘mpenzi wangu
nakupenda, nikinywa maji nakuona kwenye glasi’…leo mapenzi yamegeuka
shubiri.
Mwanamke huyo, Mchali Kihiyo (35), mama wa watoto
sita, aliyepoteza viungo vyake kutokana na ukatili wa kijinsia
uliofanywa na mwanaume ambaye wamekuwa na uhusiano nae (jina
limehifadhiwa).
“Uhusiano wetu ulikuwa mzuri, hata hivyo kwa sasa
naona mambo yamekuwa magumu kwangu, leo hii mimi sina mkono wa kushoto
na nimeondolewa sehemu ya viungo vyangu vya upande mmoja,”anasema
Mchali,akibubujikwa machozi kutokana na ulemavu alioupata.
Chanzo cha ulemavu
Anasema maisha yao ya uhusiano yalikuwa ya furaha
kwa kipindi chote lakini