Mchali akionyesha mkono aliokatwa
Baada ya kuwa katika mapenzi na mwanaume huyo kwa zaidi ya miaka 17,
wakipendana na kuitana majina yote mazuri unayoyajua yakiwamo kuambiwa
‘mpenzi wangu nakupenda, nikinywa maji nakuona kwenye glasi’…leo mapenzi
yamegeuka shubiri.
Mkasa wa mwanamke kukatwa mkono
Ilikuwa Agosti 7, mwaka huu, saa mbili usiku.
Ilikuwa ni siku iliyobadili historia ya maisha yake. Baada ya kuwa
katika mapenzi na mwanaume huyo kwa zaidi ya miaka 17, wakipendana na
kuitana majina yote mazuri unayoyajua yakiwamo kuambiwa ‘mpenzi wangu
nakupenda, nikinywa maji nakuona kwenye glasi’…leo mapenzi yamegeuka
shubiri.
Mwanamke huyo, Mchali Kihiyo (35), mama wa watoto
sita, aliyepoteza viungo vyake kutokana na ukatili wa kijinsia
uliofanywa na mwanaume ambaye wamekuwa na uhusiano nae (jina
limehifadhiwa).
“Uhusiano wetu ulikuwa mzuri, hata hivyo kwa sasa
naona mambo yamekuwa magumu kwangu, leo hii mimi sina mkono wa kushoto
na nimeondolewa sehemu ya viungo vyangu vya upande mmoja,”anasema
Mchali,akibubujikwa machozi kutokana na ulemavu alioupata.
Chanzo cha ulemavu
Anasema maisha yao ya uhusiano yalikuwa ya furaha
kwa kipindi chote lakini
yamegeuka shubiri baada ya mwanamume wake huyo kuonyesha dalili ya kutompenda kama awali, hali ambayo anaitafsiri kama labda alikuwa na mwanamke mwingine.
yamegeuka shubiri baada ya mwanamume wake huyo kuonyesha dalili ya kutompenda kama awali, hali ambayo anaitafsiri kama labda alikuwa na mwanamke mwingine.
Mchali, anasema mikasa na mateso ilianza miaka
mitatu iliyopita baada ya kuhisi kwamba mwanamume wake huyo amezaa na
mwanamke mwingine. Ubaya zaidi ulimtokea baada ya mtoto wa huyo mwanamke
mwingine, kutumbukia kwenye kisima cha maji na kisha kupoteza maisha.
“Kifo cha mtoto huyo, ndicho kilichozaa tatizo
hili la ukatili dhidi yangu na kunisababishia ulemavu, kwa kuwa huyo
mwanaume wangu na huyo mwanamke aliyezaa nae, walidai kwamba mimi ndiyo
nilimtupia majini marehemu mtoto wao ili afe,”anasema mama huyo.
Vitisho kabla ya ulemavu
Mchali, anasema mara baada ya msiba wa mtoto kumalizika,
mwanamume wake huyo alihamia kwa mke mdogo lakini akawa anarejea
nyumbani na kumtukana huku akitishia kufanya lolote analofikiri linafaa.
Anasema baada ya mateso na vitisho kuzidi aliamua
kuondoka kwa mumewe huyo toka mwezi Aprili mwaka huu na kuamua kurudi
kwa wazazi wake huku akiwaacha watoto wake kwenye nyumba waliyokuwa
wakiishi.
Anasema alilazimika kuwaacha watoto kutokana na
agizo la mumewe, aliyekataa asiwachukue, hivyo akaanza maisha mengine ya
upweke bila watoto huku akiendesha maisha yake kwa biashara ya kuuza
samaki.
Anasema mwanzoni mwa mwezi huu, aliugua malaria na
kukaa nyumbani bila kwenda kwenye biashara zake. Agosti saba mwaka huu,
alipata nafuu na kuamua kwenda kumsalimia kaka yake, anayeishi mbali
kidogo na nyumbani kwao na ndipo yakamkuta yaliyomkuta.
Anaeleza kuwa alikaa kwa kaka yake hadi muda wa
futari wakafuturu na kushangaa simu yake ikiita, kuangalia ni namba ya
mpenzi wake huyo. Alipoipokea, aliulizwa aliko, yeye alimweleza yuko kwa
kaka yake na kumtaka amfuate mnadani akale nyama kitendo ambacho
anasema alipingana nacho.
Anasema baadaye aliamua kurudi nyumbani na
kusindikizwa na wifi yake hadi karibu na nyumba yao ikiwa ni saa mbili
usiku.Walipoagana, ghafla akashangaa kusikia sauti ya mumewe ikimuita,
alipogeuka alimwona, kisha akamuuliza alikotoka na kumwambia alikuwa
kwa kaka yake.
Kipigo na ulemavu
Anasema mara baada ya kumjibu mwanamume huyo
alianza kumpiga na hatimaye alianguka chini na mumewe akatoa panga na
kuanza kumkatakata sehemu mbalimbali za mwili wake.
Hakika hujafa hujaumbika. Mchali amecharangwa kwa
mapanga kuanzia chini ya goti mguu wa kushoto hadi kwenye makalio,
amekatwa sehemu zaidi ya saba mwilini.
Ni kama alitaka kumkata shingo
Anasema kwa namna anavyoona ni kama alidhamiria
kumuua akisema kuwa mara nyingi akiwa na huo upanga alikuwa analenga
kumtenganisha shingo. Alichofanya mama huyo ni kuweka mikono shingoni
kuzuia panga, kitendo kilichosababisha mkono wake wa kushoto kukatwa
kabisa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni