Mwenyekiti Taifa wa Chama Cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahimu Lipumba
akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, wakati akitoa
tamko la kulaani kitendo cha Naibu Spika wa Bunge la Muungano wa
Tanzania, Job Ndugai kuwanyanyasa na kuwadhalilisha wabunge wa upinzani
akiwamo Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, Freeman Mbowe
Chama cha Wananchi (Cuf), kimesema kitendo cha Naibu Spika wa
Bunge, Job Ndugai kukataa kumpa nafasi Kiongozi wa Kambi ya Upinzani
Bungeni, Freeman Mbowe na kuamuru askari wa Bunge wamtoe nje ya ukumbi
huo ni kumhujumu Rais Kikwete kwenye azma yake ya kupata Katiba Mpya.
Pia, chama hicho kimesema kinafanya juhudi za
kuwasiliana na viongozi wa vyama vingine ili kuweka mkakati wa pamoja wa
kukabiliana na hujuma dhidi ya mchakato wa kupata Katiba Mpya na
kuimarisha umoja wa kitaifa kwenye kipindi hiki cha kukabiliana na
changamoto za nchi jirani.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa
chama hicho, Profesa Ibrahimu Lipumba alisema,
Cuf inalaani vitendo vya kuwanyanyasa na kuwadhalilisha wabunge wa upinzani akiwamo Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na kudai kuwa inaonyesha wazi CCM wanampango wa kutengeneza katiba ya upande mmoja.
Cuf inalaani vitendo vya kuwanyanyasa na kuwadhalilisha wabunge wa upinzani akiwamo Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na kudai kuwa inaonyesha wazi CCM wanampango wa kutengeneza katiba ya upande mmoja.
“Kwa mfumo wa mabunge ya Jumuiya ya Madola, kwa
Tanzania Waziri Mkuu na kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni
ndiyo wanawakilisha pande mbili ndani ya Bunge, hivyo kumnyima Mbowe
fursa ya kuzungumza ni unyanyasaji na udhalilishaji na kwamba kitendo
hicho hakikubaliki,” alisema.
Profesa Lipumba alisisitiza muswada uliokuwa
unajadiliwa ulikuwa na utata, Serikali imeubadili kwa nguvu na kuondoa
maoni muhimu ya wadau.
Chanzo:gazeti la Mwananchi
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni