Wafanyakazi wa Marikana waligoma wakidai nyongeza ya mishahara na mazingira bora ya kazi
Polisi nchini Afrika Kusini wameikosoa tume
inayochunguza mauaji ya wafanyakazi thelathini na nne katika mgodi wa
madini ya platinum huko Marikana Agosti mwaka uliopita kusema kuwa
walidangaya.
Katika taarifa idara ya polisi imesema kuwa madai dhidi yao ni ya kuudhi na hayana msingi.Wamesisitiza kuwa walitumia risasi kujilinda walipokuwa wakijaribu kuwatawanya na kuwapokonya silaha wafanyikazi hao waliokuwa wakigoma.