Jumatatu, 11 Novemba 2013

ONA JINSI KIMBUNGA KIVILYOFANYA UHARIBIFU MKUBWA NCHINI UFILIPINO

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/11/131111133731_1_philippines.jpg 
Raia wa Ufilipino wangali wanahisi athari za Kimbunga Haiyan, kinachojulikana na wenyeji kama Yolanda. Kimbunga hicho kilifanya uharibifu mkubwa sana baada ya kupiga eneo la Kati mwa Ufilipino Ijumaa na Jumamosi. Inahofiwa maelfu ya watu wamefariki kutokana na Kimbunga hicho.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/11/131111133733_2_philippines.jpg
Picha zaidi zilizopigwa kutoka angani, katika mji wa Tacloban moja ya maeneo yaliyoathriwa zaidi -lakini waokozi wangali kufika katika baadhi ya maeneo yaliyoathirika ambako inahofiwa uharibifu mkubwa zaidi ulifanyika.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/11/131111133735_3_philippines_ap.jpg
Siku tatu baada ya Kimbunga hicho kinachosemekana kuwa kibaya zaidi kushuhudiwa katika historia ya nchi hiyo , waathiriwa wako katika hali mbaya.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/11/131111133737_4_philippines_ap.jpg 
Wakaazi wengi walijaribu kujiokoa lakini wakajipata katika vituo vya kuwanusuru watu ambavyo navyo vilishindwa kuhimili mawimbi ya kimbunga hicho. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/11/131111133739_5_philippines_reuters.jpg
Kuna afueni kwa wachache waliofika katika mkoa huu wa Lloilo, huku helikopta zikiwasili na msaada zaidi
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/11/131111133741_6_philippines_afp.jpg
Hapa katika mji wa Guiuan , mkoa wa Samar, wakaazi wanajisaidia kadri ya uwezo wao , wakichukua chakula na hata kufanya msako katika moja ya majumba yaliyosalia kusimama baada ya kimbunga
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/11/11/131111133743_7_philippinesap.jpg
Nchi kadhaa zimeahidi kutoa msaada zaidi, lakini huku barabara zikiwa zimezibwa na viwanja vya ndege kuharibiwa, tatizo litakuwa msaada huo kuwafikia watu wanaouhitaji zaidi