Jumatatu, 9 Septemba 2013

CUF: Ndugai anahujumu


 Mwenyekiti Taifa wa Chama Cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahimu Lipumba akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, wakati akitoa tamko la kulaani kitendo cha Naibu Spika wa Bunge la Muungano wa Tanzania, Job Ndugai kuwanyanyasa na kuwadhalilisha wabunge wa upinzani akiwamo Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, Freeman Mbowe
Chama cha Wananchi (Cuf), kimesema kitendo cha Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai kukataa kumpa nafasi Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe na kuamuru askari wa Bunge wamtoe nje ya ukumbi huo ni kumhujumu Rais Kikwete kwenye azma yake ya kupata Katiba Mpya.
Pia, chama hicho kimesema kinafanya juhudi za kuwasiliana na viongozi wa vyama vingine ili kuweka mkakati wa pamoja wa kukabiliana na hujuma dhidi ya mchakato wa kupata Katiba Mpya na kuimarisha umoja wa kitaifa  kwenye kipindi hiki cha kukabiliana na changamoto za nchi jirani.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahimu Lipumba alisema,

Serena Williams ashinda US Open tena kwa mara ya 17


 Serena Williams 

Bingwa wa dunia wa Tenis kwa wanawake, ameshinda kwa mara ya kumi na saba shindano la US Open, katika fainali lliyokuwa yenye mbwembwe dhidi ya Victoria Azarenka katika uwanja wa Flushing Meadows.
Serena mwenye umri wa miaka 31, aliweza kuibuka mshindi dhidi ya

Cameroon yailaza Libya bao 1-0

Timu ya soka ya Cameroon
Cameroon imejipatia nafasi ya kushiriki michuano ya mwisho ya kufuzu michuano ya kombe la Dunia kwa nchi za Afrika mwaka 2014 nchini Brazil.
Indomitable Lions waliicharaza Libya bao moja bila kwenye mechi ambayo ilichezwa mjini Yaounde Jumapili.
Cameroon walijitosa uwanjani wakijua fika kuwa hata ikiwa wangeenda Sare na Libya matokeo hayo hayangeathiri nafasi yao kushiriki, na haya yote ni kutokana na timu ya Togo kutumia mchezaji aliyeharamishwa Alexis Romao kucheza wakati wa

MATUKIO KATIKA PICHA-AFRIKA

  • Mwenyeji wa mji wa Cape Town nchini Afrika Kusini akifanya mazoezi yake katika moja ya kumbi za mazoezi mnamo Jumatatu , baada ya msimu wa baridi ambao uliacha eneo hilo likuwa limejaa theluji. 
     
  • Wakati mjini Mogadishu siku ya Jumanne , polisi anatoroka eneo kulikotokea mlipuko wa bomu katika kiwanda kimoja cha Petroli katika uliokuwa ubalozi wa Marekani. Marekani ilifunga ubalozi wake mjini Mogadishu zaidi ya miaka ishirini iliyopita baada ya nchi kutumbukia kwenye vita
     
  • Hapa, mwanariadha maarufu wa Ethiopia, Kenenisa Bekele, 31, anaonekana akifanya mazoezi nje ya kambi ya mazoezi mjini Addis Ababa mnamo Jumapili. Mwanariadha huyo wa mbio za masafa marefu, anayeshikilia rekodi ya dunia katika mbio za mita 5,000 na 10,000 anasema bado hajatafakari kuhusu kusalimu amri katika riadha anajianda kwa michezo ya olimpiki itakayofanyika Rio mwaka 2014. 
     
  • Bango hili lilitolewa siku ya Jumatatu kutangaza mchuano kati ya wanamasumbwi, Catherine Phiri Kushoto, kutoka Zambia na Toma Hawa Babirye kutoka Uganda. Mchuano utafanyika mjini Lusaka Zambia.Phiri, mwenye umri wa miaka 19 mwanafunzi wa shule anatarajiwa na wengi kushinda.
     
  • Wasichana wanasarakasi kutoka Angola wakishiriki mashindano ya kimataifa ya sarakasi nchini Urusi
     
  • Watu wanaoenakana hapa wakiokota karatasi na plastiki katika jaa la taka nchini Ivory Coast . Hutumika kwa kutengeza chupa na karatasi za plastiki
     
  • Mjini Johannesburg, mtu huyo ametoa chupa kuu kuu kwenye jaa la taka kupeleka viwandani ambako chupa nyengine mpya hutengezwa
     
  • Watoto hawa wanigeria ni mapacha ambao viungo vyao vimeshikana , hapa ni baada ya kufanyiwa upasuaji nchini India 
     
  • Mwanamalkia wa Denmar Mary wakati wa ziara yake nchini Morocco

18 wauawa kwenye makabiliano na Boko Haram

Makundi ya vijana yanasaidia jeshi kutoa ulinzi kwa raia Nigeria

Takriban watu 18 wamefariki kwenye makabiliano makali kati ya kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Boko Haram na kundi la kijamii la kutoa ulinzi kwa raia, katika jimbo la Borno Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Wengi wa wale waliouawa waliaminika kuwa vijana wanaotoa ulinzi kwa wanavijiji waliokuwa wanatoa ulinzi kwa mji wa Benisheik dhidi ya wapiganaji wa kiisilamu.
Makabiliano hayo yametokea siku chache baada ya

William Ruto aelekea ICC kwa kesi

Naibu rais William Ruto 

Naibu rais wa Kenya William Ruto, ameondoka kuelekea Hague Uholanzi ambako anakabiliwa na kesi ya uhalifu dhidi ya binadamau katika mahakama ya ICC. Kesi yake inatarajiwa kuanza siku ya Jumanne.
Maafisa wakuu wa serikali walimuaga Ruto katika uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta mjini Nairobi.
Bwana Ruto na rais Uhuru Kenyatta, wameshtakiwa kwa kesi ya uhalifu dhidi ya binadamu, ingawa wanakana kuhusika na mauaji yaliyotokea kufuatia ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007-2008.
Mnamo siku ya Jumapili, Rais Kenyatta alisema kuwa ICC

Waliomteka nyara Askofu wasakwa Nigeria

Askofu Ignatius Kattey

Polisi nchini Nigeria wanawasaka wanaume waliomteka nyara kiongozi wa ngazi ya pili wa kanisa la kianglikana nchini Nigeria Askofu mkuu Ignatius Kattey.
Askofu Ignatius ni mkuu wa kanisa la kianglikana tawi la jimbo la Niger Delta.
Alitekwa nyara Ijumaa jioni akiwa na mkewe Beatrice, karibu na makao yao mjini Port Harcourt, Kusini mwa nchi.
Katika miaka ya hivi karibuni, visa vya watu kuteka nyara wakati wakidai kulipwa kikombozi vimekuwa jambo la kawaida katika jimbo lenye utajiri wa mafuta la Niger Delta linalozingira Port Harcourt
Mwaka jana mamake waziri wa fedha, Ngozi Okonjo-Iweala alitekwa nyara na kuzuiliwa kwa siku tano.
Hakuna kundi lolote limedai kumkamta Askofu huyo akiwa na mkewe.
Makundi mengi ya magenge ya watu waliojihami, huendesha shughuli zao katika eneo hilo kutokana na miaka mingi ya migogoro katika eneo hilo dhidi ya sekta ya mafuta.

Wanafunzi 868,030 kuhitimu Darasa la Saba


Ni kwa nchi nzima, ambapo mwaka huu matokeo hayo ni muhimu kwa taifa kujipima kuhusu mpango wake mpya wa matokeo makubwa sasa.

Wanafunzi 868,030 wa Darasa la Saba wanatarajiwa kufanya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi Jumatano na Alhamisi wiki hii, ikiwa ni mwanzo wa mpango wa Serikali wa Matokeo Makubwa Sasa utakaotekelezwa kwa kuanzia katika mitihani hiyo.
  Taarifa ya Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), inaonyesha kuwa wanafunzi hao wanatoka kwenye shule 15,677 zikiwamo za umma na binafsi.
  Inaeleza taarifa hiyo kuwa, wanafunzi wanaotarajiwa kufanya mtihani wa lugha ya Kiswahili ni 844,810  kati yao wasichana wakiwa 444,475 na wavulana 400,335.    Kati ya wanafunzi hao, wasioona ni 88 wavulana wakiwa ni 56 na wasichana 32 huku

RUTO AENDA ICC

NAIROBI, Kenya - Photo shows Kenyan Deputy President William Ruto in Nairobi in March 2013. Ruto, facing charges of crimes against humanity, will visit Japan to attend an international conference on development in Africa, Japanese government and other sources said May 27. (Kyodo)
Makamu wa Rais wa Kenya William Ruto anakwenda The Hague, Uholanzi, leo ikiwa ni siku moja kabla ya kuanza kesi inayomkabili katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu dhidi ya 
 Binaadamu (ICC) mjini humo. 
Ruto mwenye umri wa miaka 46 anakabiliwa na mashitaka ya kuandaa machafuko ya baada ya uchaguzi mkuu wa 2007 ambapo mamia ya watu waliuwawa.
Kiongozi huyo ni mwanasiasa wa ngazi ya juu kabisa aliye madarakani kuwahi kufika mbele ya mahakama hiyo ahadi sasa na kesi hiyo itaanza siku chache tu baada ya wabunge nchini Kenya kupiga kura kujitoa katika mahakama na kuwa nchi ya kwanza kuchukua hatua hiyo.
Wakati akiondojka kwenye uwanja wa ndege wa Nairobi, Makamu huyo wa rais aliupungia mkono umati uliokuweko uwanjani, lakini alikataa kusema chochote.
Ruto anatuhumiwa kupanga baadhi ya machafuko yaliozuka baada ya uchaguzi 2007-2008 ambapo watu wapatao 1,100 waliuwawa na zaidi ya 600,000 kupoteza makaazi yao.
Mshitakiwa mwenzake, mtangazaji wa kituo kimoja cha Redio Joshua arap Sang anayetuhumiwa kuratibu mashambulizi hayo, tayari yuko The Hague, ambako aliwasili mwishoni mwa juma. Wopte wamesema watakana mashtaka yanayowakabili.
Jumapili Ruto alishiriki katika sala ya maombi kanisani akiwa pamoja na Rais Uhuru Kenyatta ambaye pia anatuhumiwa kuandaa kampeni ya mauaji, ubakaji na kuwahamisha watu. Kesi dhidi yake itaanza Novemba 12 
Kenyatta asema hatakwenda The Hague kama Ruto hajarejea
  Hata hivyo Rais Kenyatta amesema hatokubali yeye na naibu wake wawe nje ya Kenya kwa wakati mmoja.
"Tutashirikiana na mahakama ya ICC na wakati wote tumekuwa tukiahidi kufanya hivyo," aliuambia mkutano wa hadhara wa wafuasi wake kwamba lazima ifahamike lakini kwamba Kenya ina katiba na kwamba Ruto na yeye hawatokuwa nje ya nchi wakati mmoja.
Kenyatta ambaye pia atayakana mashtaka yanayomkabili amesema ni ya uwongo na yatafutwa, akiongeza kwamba wapangaji wa njama hizo watatajwa na kuaibishwa. Huku akishangiriwa na umati uliokuwa ukimsikiliza, Kenyatta alisema,"shindi hautokuwa wa Ruto, Sanga au wangu , bali kwa Kenya."
Uchaguzi wa 2007 nchini Kenya uliangamwa na madai ya wizi wa kura na mizengwe, lakini kile kilichoanza ghasia za kisiasa kikageuka kuwa wimbi la mauaji ya kikabila na mashambulizi ya kulipiziana kisasi, yakiwa machafuko mabaya kabisa tangu huru wa nchi hiyo 1963
Mwaandsishi: Mohammed Abdul-Rahman/AFP
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta (kulia) na Makamu wake, William Ruto.
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta (kulia) na Makamu wake, William Ruto.
Mhariri: Josephat Charo