Jumatano, 15 Januari 2014

KATIBA YA WANANCHI WA MISRI IPO MIKONONI MWAO...!

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/14/140114112426_egypt_vote_pic_gal_976x549_e.jpg 
Kwa siku mbili zijazo, Wamisri watajua ikiwa watakuwa na katiba mpya au ikiwa rasimu ya katiba inayopigiwa kura haitaidhinishwa.  
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/14/140114112259_egypt_vote_pic_gal_976x549_getty.jpg 
Nchi hii imekuwa ikikumbwa na hali ngumu ya kisiasa tangu mapinduzi ya kiraia yaliyomwondoa mamlakani Hosni Mubarak.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/14/140114105011_egypt_vote_pic_gal_976x549_reuters.jpg
Baadhi walihisi huo ndio ulikuwa mwisho wa siasa mbaya lakini baadaye rais aliyechaguliwa kihalali Mohammed Morsi, aliondolewa mamlakani na jeshi
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/14/140114112136_egypt_vote_pic_gal_976x549_reuters.jpg
Morsi alikuwa mwanachama wa vuguvugu la Muslim Brotherhood ambalo ikiwa katiba hii itapitishwa ndio itakuwa mwisho wake. Chini ya Katiba mpya Vyama haviwezi kuundwa kwa misingi ya kidini, kabila, jinsia na kijiografia. Bila shaka itakuwa pigo kubwa kwa vuguvugu la Muslim Brotherhood
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/14/140114105247_egypt_vote_pic_gal_976x549_ap.jpg
Misri pia imekuwa ikikumbwa na hali mbaya ya usalama. Mashambulizi ya kulipiza kisasi na ya kuvizia yakiwa jambo la kawaida. Chini ya katiba hii waziri wa ulinzi sharti awe mwanajeshi kama hali ilivyo sasa.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/14/140114104533_egypt_vote_pic_gal_976x549_ap.jpg
Usalama ulidhibitiwa kote nchini humo kwa hofu ya mashambulizi
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/14/140114111950_egypt_vote_pic_gal_976x549_ap.jpg
Wake kwa waume, wazee kwa vijana wote walijitokeza kwa hamu ya kuipatia Misri mustakabali mwema wa kisiasa