Hapa ni Stesheni ya Shirika la Reli la Tanzania na Zambia Mbeya
Hawa ni Baadhi ya Wafanyakazi wa Stesheni mbalimbali wakiwa kwenye mshikamano kushinikiza uongozi wa shirika hilo kuwapa mishahara yao ya miezi minne sasa
Kwa nyuso za huzuni kabisa wanyakazi wa shirika la reli ya Tanzania na Zambia-Mbeya
Kushoto kwako ni mimi Alex Mwalyego nikijaribu kupata habari kadhaa kutoka kwa baadhi ya wafanyakazi wa shirika hilo
Hapa wafanyakazi wakiondoka kwa huzuni bila kupata jibu lolote nini hatima ya mishahara yao
Polisi nchini Kenya wanachunguza
kisa ambacho kichwa cha mtu aliyeuawa kilipatikana kimewekwa nje ya
afisi ya mwenyekiti wa tume ya kitaifa ya polisi Johnston Kavuludi
jijini Nairobi.
Kifurushi hichi kilichokuwa kimefungwa kwa karatasi ya plastiki, vilevile kilikuwa na mikono miwli ya binadamy iliyojaa damu.kando ya kifurishi hicho kulikuwa na ilaani iliyoandiskwa ''Kavuludi wewe ndiye utakayefuata''.
Tangu uteuzi wake, kamishna huyo ameongoza harakati za kujaribu kuifanyia marekebisho idara ya polisi ambayo inadaiwa kuwa fisadi zaidi Afrika Mashariki.
Kwa mujibu wa idara ya polisi, hakuna mshukiwa aliyekamatwa kauhusiana na tukio hilo na kuwa bado wangali wanachunguza mwili huo ulikuwa wa nani.
Katika miezi ya hivi karibuni kumekuwa na uhasama kati ya tume hiyo inayoongozwa na Kavuludi na ofisi ya mkuu wa polisi, huku zikilumbana kuhusu nani ana madaraka ya kuliendesha idara hiyo.
Chanzo na BBC Swahili