Magaidi wateka watu dukani Nairobi
Watu waliokuwa na silaha wamefyatua risasi mjini Nairobi, Kenya, kwenye eneo la maduka katika mtaa wa Westlands.
Walioshuhudia tukio hilo, wanasema kuwa maguruneti piya yalitumika.
Inaarifiwa watu watano wamekufa.
Mwandishi wetu mjini Nairobi anaeleza kuwa
washambuliaji inaarifiwa walivaa vilemba kama vya al-Shabaab, lakini
haikuthibitishwa kama wapiganaji hao wamehusika.
Polisi waliojihami kwa silaha wamezingira jengo
la maduka liitwalo Westgate, katika mtaa wa Westlands, na kuna taarifa
ya watu waliojeruhiwa wakitolewa hapo kwa machera.
Inaarifiwa kuwa watu wengi wamenasa ndani ya jengo.
Magari yaliyoegeshwa nje ya maduka yameharibika