Alhamisi, 23 Januari 2014

UKREINE YAGEUKA UWANJA WA VITA....SIASA MCHEZO MCHAFU

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145158_kiev-protest-1.jpg 
Angalau watu wawili wameuawa katika ghasia kati ya polisi na waandamanaji katika mji mkuu wa Ukraine Kiev.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145200_kiev-protest-2.jpg
Makabiliano hayo ya Jumatano, yalianza baada ya polisi kuanza kuvunja maandamano ya moja ya makundi ya wanaharati 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145202_body-bbc.jpg
Viongozi wa mashitaka walithibitisha kuwa watu wawili walifariki kutokana na majeraha ya risasi. Ni watu wa kwanza kufariki kutokana na vurugu tangu kuanza Novemba mwaka jana kutokana na mapendekezo ya serikali kujiunga na muungano wa Ulaya
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145204_kiev-protest-4.jpg
Makabiliano hayo yanakuja baada ya siku moja ya kubuniwa sheria mpya za kuharamisha maandamano wiki jana. Bunge liliidhinisha sheria hizo wiki jana na kusababisha vurugu mpya
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145206_kiev-protest-5.jpg
Mamia ya watu wamejeruhiwa ingawa baadhi ya vurugu zimelaumiwa kwa kundi moja linalounga siasa kali
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145208_kiev-protest-6.jpg
Ghasia za Jumatano, zilianzia katika sehemu ndogo ya barabara kuelekea katika majengo ya bunge .
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145210_kiev-protest-7.jpg
Muda mfupi baada ya saa mbili asubuhi, baada ya usiku wa amani, polisi walivamia sehemu ambako waandamanaji hao walikuwa wamekita kambi
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145212_kiev-protest-8.jpg
Polisi baadaye walichukua hatua zao, baada ya makabiliano makali na waandamanaji lakini ilipofika mchana na kuvunja vuzuizi
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145213_kiev-protest-9.jpg
Waandamanaji walianza, kuwatupia mabomu ya petroli na mawe wakati polisi wa kupambana na ghasia nao waliwatupia magurunedi na risasi za mipira
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/22/140122145215_kiev-protest-10.jpg
Moshi mweusi ulifuka kutokana na magurudumu kuteketezwa wakati wa vurugu hizo mjini Kiev, huku picha za magari ya kivita yakitumiwa kupambana na waandamanaji hao.