Chama cha Udugu wa Kiislamu kimepanga kuandamana baada ya sala ya Ijumaa
dhidi ya serikali ya mpito nchini humo. Maandamano hayo yameitishwa
licha ya serikali kutishia kutumia nguvu kupambana na waandamanaji.
Maandamano haya ya leo yanatarajiwa kupima ni kwa kiwango gani vikosi
vya usalama vimelidhoofisha kundi hilo na hii itajulikana tu kwa namna
watu watakavyojitokeza katika maandamano hayo.
Kulingana na wakaazi huko, maandamano ya leo yanahofiwa kuzua machafuko zaidi katika nchi hiyo iliyokumbwa na msukosuko wa kisiasa.
Umwagikaji mkubwa wa damu ulishuhudiwa wiki mbili zilizopita baada ya polisi kushambulia kambi za waandamanaji waliokuwa wanapinga hatua iliyochukuliwa Julai 3 ya kumuondoa madarakani kiongozi wao Mohammed Mursi kwa njia ya mapindzi ya kijeshi.
Hali hiyo ilisababisha vurugu ya wiki nzima zilizowauwa watu takriban 1,000, wengi wao wakiwa wafuasi wa Mursi. Inadaiwa kuwa baadhi ya wafuasi hao walijibu mashambulizi kwa kuchoma makanisa, majengo ya serikali na pia kushambulia vituo vya polisi.
Pande zote mbili zaombwa kusuluhisha tofauti zao
Katika mahojiano na shirika la habari la Associated Press, kiongozi wa kundi lililokuwa la waasi la Gamaa Islamiya, Abboud el-Zommor, alizihimiza pande zote mbili serikali na upinzani kukaa pamoja na kutatua tofauti zao ili kusimamisha umwagikaji wa damu nchini humo.
Huku hayo yakiarifiwa serikali imeongeza majeshi yake katika maeneo tofauti nchini humo huku ikilishutumu kundi la Udugu wa Kiislamu kuitisha maandamano na kuzua ghasia.
Wakati huo huo utawala wa Misri umeendelea kuwakamata viongozi wa kundi hilo kwa madai ya kuchochea ghasia. Tayari viongozi wawili, Mohammed el-Beltagy na Khaled el-Azhari, walikamatwa hapo jana.
Polisi wanasema waliwakamata kwa sababu ya kuchochea maandamano na kuteswa kwa polisi aliyekamatwa na waandamanaji mjini Cairo.
Kwa upande wake. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Misri imesema itapambana vikali na watu ambao wanajaribu kuyumbisha usalama wa nchi na kwamba polisi wamepewa amri ya kutumia nguvu katika kulinda mali ya umma na ile ya watu binafsi nchini humo.
Wizara hiyo imesema pia kuwa maandamano ya leo yana lengo la kusababisha vurugu.
Mwandishi: Amina Abubakar/Reuters/AP
Mhariri: Mohammed Khelef
Kulingana na wakaazi huko, maandamano ya leo yanahofiwa kuzua machafuko zaidi katika nchi hiyo iliyokumbwa na msukosuko wa kisiasa.
Umwagikaji mkubwa wa damu ulishuhudiwa wiki mbili zilizopita baada ya polisi kushambulia kambi za waandamanaji waliokuwa wanapinga hatua iliyochukuliwa Julai 3 ya kumuondoa madarakani kiongozi wao Mohammed Mursi kwa njia ya mapindzi ya kijeshi.
Hali hiyo ilisababisha vurugu ya wiki nzima zilizowauwa watu takriban 1,000, wengi wao wakiwa wafuasi wa Mursi. Inadaiwa kuwa baadhi ya wafuasi hao walijibu mashambulizi kwa kuchoma makanisa, majengo ya serikali na pia kushambulia vituo vya polisi.
Pande zote mbili zaombwa kusuluhisha tofauti zao
Katika mahojiano na shirika la habari la Associated Press, kiongozi wa kundi lililokuwa la waasi la Gamaa Islamiya, Abboud el-Zommor, alizihimiza pande zote mbili serikali na upinzani kukaa pamoja na kutatua tofauti zao ili kusimamisha umwagikaji wa damu nchini humo.
Huku hayo yakiarifiwa serikali imeongeza majeshi yake katika maeneo tofauti nchini humo huku ikilishutumu kundi la Udugu wa Kiislamu kuitisha maandamano na kuzua ghasia.
Wakati huo huo utawala wa Misri umeendelea kuwakamata viongozi wa kundi hilo kwa madai ya kuchochea ghasia. Tayari viongozi wawili, Mohammed el-Beltagy na Khaled el-Azhari, walikamatwa hapo jana.
Polisi wanasema waliwakamata kwa sababu ya kuchochea maandamano na kuteswa kwa polisi aliyekamatwa na waandamanaji mjini Cairo.
Kwa upande wake. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Misri imesema itapambana vikali na watu ambao wanajaribu kuyumbisha usalama wa nchi na kwamba polisi wamepewa amri ya kutumia nguvu katika kulinda mali ya umma na ile ya watu binafsi nchini humo.
Wizara hiyo imesema pia kuwa maandamano ya leo yana lengo la kusababisha vurugu.
Mwandishi: Amina Abubakar/Reuters/AP
Mhariri: Mohammed Khelef
1Mwanamuziki Diamond Platnum akimkabidhi funguo ya gari aina ya Toyota Funcargo mwanamuziki mkongwe nchini mzee Muhidin Gurumo kama zawadi yake kwa mkongwe huyo wa muziki baada ya kustaafu rasmi kuimba muziki, Diamond alitoa zawadi hiyo kwa Gurumo katika hafla yake ya uzinduzi wa video yake mpya ya wimbo Nomber One aliyoirekodi huko Afrika Kusini ikigharimu kiasi cha dola elfu 30.000 zaidi ya milioni arobaini za Tanzania, Video hiyo imetengenezwa kwa viwango vya kimataifa na itaweza kumtangaza vyema kijana huyo wa kitanzania katika ulimwengu wa muziki hasa kimataifa, Hafla hiyo imefanyika kwenye hoteli ya Serena Dar es salaam na imehudhuriwa na wasanii pamoja na waigizaji wa filamu na watu maarufu mbalimbali
Diamond akimuongoza mzee Gurumo kwenda kumuonyesha gari
Diamond akimuonyesha Mzee Gurumo gari
Akimuelekeza jambo baada ya mzee Gurumo kuingia kwenye gari
Wasanii mbalimbali pamoja na MaDJ walikuwepo katika hafla hiyo hapa ni Dully Sykes na MawanaFA wakiwa na baadhi ya MaDJ
Maurice
Njowoka kutoka Cocacola wa pili kutoka kushoto na Mwanamuziki AY wa
tatu kutoka kushoto pamoja na wadau wengine wakiwa katika hafla hiyo
Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka akiwa na mama yake Diamond
Wadau mbalimbali wakiwa katika hafla hiyo
Mzee Gurumo akihojiwa na waandishi wa habari
Hawa
marafiki zangu wakakumbushia miaka kadhaa waliyofunga ndoa kwa
kulishana mishikaki ilipendeza katikati ni Nancy Sumari akishuhudia
Kulia ni Irene Uwoya kushoto Salma Msangi
Kushoto AY na Salama Jabir wakipiga story na wadau mbalimbali


Kauli hii ameitoa leo katika kongamano la ufuatiliaji wa uwajibikaji Jamii ambapo yeye alikuwa akiongelea majukumu ya bunge katika kusimamia uwajibikaji.
Mambo mengi aliyoongea yalikuwa ni yenye mwelekeo chanya isipokuwa hili la kutupa tahadhari ya kutowaamini wanasiasa, akisisitiza hata wa upinzani.
Nyuma ya kauli hii kumejificha nadharia nyingi kutegemea na mtu atakavyoipokea.
Kwa maana nyingine, kauli hii inaleta hisia kwamba, hata wale wa chama chake tusiwaamini pia.
Kwa kuwa mheshimiwa ni miongoni mwa members hapa, najua ujumbe huu utamfikia. Nilitaka atoe ufafanuzi alikuwa anamaanisha nini kwa kauli yake hii.


