Jumatatu, 23 Desemba 2013

HII NDIYO AJALI YA TRENI ILIYOTOKEA KIBERA HUKO NAIROBI KENYA

Vibanda vya Kibera vimejengwa karibu sana na njia ya reli
Waokozi wana wasiwasi kuwa pengine watu kadha wamenasa chini ya treni iliyopinduka katika mitaa ya Kibera, Nairobi - eneo la watu maskini.
Watu kama kumi walijeruhiwa wakati mabehewa mane ya mizigo yalipopinduka juu ya vibanda kando ya njia ya reli.
Waokozi wanajaribu kutafuta nafasi katika mtaa wenye nyumba zilizogandana sana, ili kuleta mashini ya kunyanyua mabehewa ili kuwafikia wale walionasa.
Mabehewa yalianguka juu ya vibanda vilivyo karibu na njia ya reli.
Magazeti yanaarifu kuwa kazi za uokozi zimezingika kwa sababu watu wengi wamezonga eneo hilo.