Wanafunzi Albino wakiwa wamepumzika nje ya eneo la shule.
Shinyanga. Shule ya Msingi Maalumu Buhangija iliyopo Manispaa ya Shinyanga ililenga kuwasaidia watoto wasioona.
Lakini kutokana na kuzuka kwa wimbi la mauaji ya
walemavu wa ngozi (albino), mwaka 2009 shule hiyo iliamua kuwahifadhi
hapo ili kulinda usalama wao pamoja na kuwapatia elimu.
Shule hiyo kwa sasa inalea watoto mchanganyiko
wakiwemo wasiiona 37, viziwi 46 na walemavu wa ngozi (albino) 164,
ambapo licha ya kuwa chini ya Serikali kupitia halmashauri husika, kwa
kiasi kikubwa inategemea msaada kutoka kwa wafadhili ambao ni mashirika,
wahisani pamoja na watu binafsi kutokana na Serikali kuitelekeza.
Watoto wanaosoma Buhangija Maalumu, wamekuwa
wakiishi kwa dhiki kubwa kutokana na uhaba wa fedha za kuwahudumia,
mahitaji muhimu kama vile chakula, malazi