Jumamosi, 7 Septemba 2013

Wasichana watakiwa kuvaa makoti India

Maandamano dhidi ya ubakaji India

Chama cha upinzani cha India, BJP, kimeiomba serikali ya mji wa Pondicherry, kusini mwa nchi, kuwapatia watoto wa shule makoti wavae ili wasinyanyaswe kijinsia.
Katibu wa chama alitoa taarifa kusema kuwa unyanyasaji ni tatizo hasa katika shule za serikali, na kwamba wasichana wote wapewe makoti na piya wapate fursa ya kueleza malalamiko yao bila ya kujitambulisha.
Visa vya ubakaji vimezidi kuripotiwa nchini India na kupelekea sheria mpya kupitishwa.
Lakini baadhi ya viongozi wamelaumiwa kwa kutazama maisha ya wanawake tu, badala ya kubadilisha tabia za wanaume.

Wanafunzi albino watelekezwa shuleni Bughangija


 Wanafunzi Albino wakiwa wamepumzika nje ya eneo la shule.

Shinyanga. Shule ya Msingi Maalumu Buhangija iliyopo Manispaa ya Shinyanga ililenga kuwasaidia watoto wasioona.
Lakini kutokana na kuzuka kwa wimbi la mauaji ya walemavu wa ngozi (albino), mwaka 2009 shule hiyo iliamua kuwahifadhi hapo ili kulinda usalama wao pamoja na kuwapatia elimu.
Shule hiyo kwa sasa inalea watoto mchanganyiko wakiwemo wasiiona 37, viziwi 46 na walemavu wa ngozi (albino) 164, ambapo licha ya kuwa chini ya Serikali kupitia halmashauri husika, kwa kiasi kikubwa inategemea msaada kutoka kwa wafadhili ambao ni mashirika, wahisani pamoja na watu binafsi kutokana na Serikali kuitelekeza.
Watoto wanaosoma Buhangija Maalumu, wamekuwa wakiishi kwa dhiki kubwa kutokana na uhaba wa fedha za kuwahudumia, mahitaji muhimu kama vile chakula, malazi

WAREMBO WA REDD'S MISS TANZANIA 2013 WAKIWA ARUSHA KWENYE HOTEL YA CORRIDO










Hizi ni baadhi tu ya nyuso zao za furaha

MWANMZIKI MAARUFU WA BONGO FLEVA REHEMA CHALAMILA "RAY C" AFUNGUKA



Mwanadada  anayejipanga kurejea kwenye gemu la Bongo Fleva kwa kishindo, Rehema Chalamila ‘Ray C’ amefunguka ya moyoni tena  akisema kuwa anamshukuru Mungu kwa kupona madhara ya madawa ya kulevya bila kupata matatizo mengine ya kiafya huku akifafanua suala la

Kenya na Nigeria kushirikiana kibiashara


Ziara ya Godluck ni ya kwanza rasmi nchini Kenya
Kenya na Nigeria zimetia saini mkataba utakaoimarisha ushirikiano wa kibiashara kati ya nchi hizo mbili.

Katika taarifa ya pamoja , Rais Kenyatta na mwenzake wa Nigeria Goodluck Jonathan pia walikubaliana kufanya kazi pamoja katika sekta ya kilimo na uvuvi na mifugo.
Serikali hizo mbili zimesaini makubaliano ya pamoja kuhusu uhamiaji ambapo huenda visa zikaondolewa kwa wanigeria na wakenya , swala la uhalifu, biashara haramu ya mihadarati na kuimarisha biashara kati ya nchi hizo mbili.

WAAUSTRALIA WAMALIZA KUPIGA KURA

Wapihaji kura wa Australia wasubiri kwenye foleni
Raia wa Australia wamemaliza kupiga kura katika uchaguzi mkuu ambapo waziri mkuu wa chama cha Labor, Kevin Rudd, anakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa Tonny Abbott.

Kura za maoni za hivi karibuni zinaonesha Bwana Abbot na chama chake cha Liberal-National akiongoza, lakini wanasiasa wote wawili wanasema matokeo hayatabiriki na waliwaomba wafuasi wao wapige kura.
Foleni zilikuwa ndefu katika vituo vya kupiga kura - katika sheria ya

MICHUANO YA KOPA COCA COLA NYANDA ZA JUU KUSINI YAINGIA DOSARI

Iringa yasusia Mashindano baada ya kulazimishwa kucheza na kufungwa na Mbeya City

Iringa FC Kopa Coca Cola wakitoka uwanjani wakiwa hawaamini kilichotendeka dhidi yao

Mbeya City FC chini ya umri wa miaka 15 Kopa Coca Cola

Mbeya City FC chini ya miaka 15 kopa Coca Cola wakiwa katika nyuso za furaha baada ya kuichabanga Iringa Fc katika viwanja vya Iyunga Mbeya

Baadhi ya wapenzi wa mpira wa miguu waliofurika kuangalia michuano ya Kopa Coca Cola viwanja vya Iyunga Mbeya

Kumekucha Madawa ya Kulevya: Kina 'Masogange' wawataja waliowatuma!


 Staa muuza nyago kwenye video za wasanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu za Kibongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ na shosti wake, Mellisa Edward kabla ya kupandishwa kizimbani kwa msala wa dawa za kulevya ‘unga’ Afrika Kusini waliingizwa kwenye chumba cha mateso kwa saa 24 ili kutaja waliowatuma.

Habari kutoka kwa chanzo chetu kilichopo jijini Johannesburg nchini humo zilidai kuwa baada ya kukamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo, walipelekwa polisi ambapo walichukuliwa maelezo.