Jumanne, 28 Julai 2015

MATUKIO KATIKA PICHA...SIASA SIYO UGOMVI NI KUZIDIANA KETE TU










Dkt Magufuli akiwa na mbowe hii inaonyesha kuwa mbowe anakubali mziki wa magufuli mpaka kashindwa kujizuia kapanda gali moja na Dkt Magufuli.

Endelea kufuatilia kupitia blog ya kijanja

MZIMU WA AJALI ZA BARABARANI UNAENDELEA KUTUMALIZA...EEE MUNGU TUSAIDIE




Watu wanne wanasadikiwa kufariki dunia baada ya Basi la Kampuni ya Sabuni Express linalofanya safari zake kati ya Karagwe na Mwanza kugongana uso kwa uso na Gari ndogo aina ya Toyota Land Cruiser iliyokuwa imebeba Masister eneo la Bugorora,ikitokea Bukoba mjini kuelekea Mutukura.

Chanzo na mwandishi wa ITV na Radio One

SIASA NI MCHEZO MCHAFU....UKISEMA WA NINI WENZIO WANASEMA WATAMPATA LINI?


Edward Lowassa anajiunga na CHADEMA na atakuwa mgombea urais wa CHADEMA na wa UKAWA. Lowassa is perhaps the most controversial and divisive political figure in the country right now. 
Na amekuwa hivyo kwa muda mrefu. Sisi CHADEMA tulimweka kwenye Orodha ya Mafisadi kutokana na kuhusika kwake na Kashfa ya Richmond mwaka 2007. Kwa hiyo swali halali kabisa ambalo lazima tulijibu kwa ufasaha ni hili: k
wa nini tumekubali, sio tu kumpokea kama mwanachama, bali kumpa heshima ya kuwa mgombea wetu wa urais. Na kwa nini washirika wetu wa UKAWA nao wamemkubali kuwa mgombea wao wa urais??? 
Jibu ni kwamba tupo katika kipindi na mazingira ya kipekee ya kisiasa katika nchi yetu. Kwa mara ya kwanza katika historia yetu kama taifa, tunaona mfumo tawala ukipasuka vipande vipande. Kwa mara ya kwanza tunaona CCM ikipasuka katikati. Na mtu aliyeipasua CCM na mfumo tawala ni Edward Lowassa. Sisi CHADEMA tumefanya kazi kubwa ya kujenga chama tangu 2010.
 Tuna wagombea wengi na bora katika majimbo mengi ya uchaguzi na ngazi ya madiwani kuliko ambavyo tumewahi kuwa nao kwa miaka yote ya nyuma. 
Hata hivyo, ni ukweli pia kwamba kuna maeneo mengi ya nchi ambako tuko dhaifu sana. Kwa kuingia kwake CHADEMA na UKAWA, Lowassa anayaingiza maeneo hayo kwenye ulingo wa kisiasa and very much within our reach.
Na Lowassa ataiporomosha CCM kwa sababu ana nguvu kubwa ndani ya chama hicho kuliko mwanasiasa mwingine yeyote. Katika mazingira ya sasa ya kipekee, tunahitaji kuamua nani ni adui mkubwa zaidi wa nchi yetu na ustawi wake: Edward Lowassa mtuhumiwa wa ufisadi au CCM na mfumo tawala ambao unajenga mazingira yanayostawisha na kulinda ufisadi. Sisi Chadema na UKAWA tumeamua kuwa adui yetu mkubwa wa sasa na siku zote ni CCM na mfumo tawala. Tumemkaribisha Edward Lowassa kwa sababu kuwepo kwake kutaharakisha kuiangamiza CCM na mfumo tawala. Tunaomba wananchi mtuelewe na kutuunga mkono.

endelea kufuatilia

Jumapili, 12 Julai 2015

Urais CCM........Magufuli Apata Ushindi wa Kishindo

Chama  cha  mapinduzi, CCM kimemteua  Dr .Magufuli  kuwa  mgombea  wa  Urais  2015. Uteuzi wa  Dr. Magufuli  umetokana na  ushindi  wa  kishindo  alioupata  baada  ya  mkutano  mkuu  kukutana jana   usiku  kwa  ajili  ya  kupiga  kura  ili  kupata  jina...oja  kati  ya  matatu  yaliyokuwa  yamependekezwa  na  Halmashauri  kuu  ya  CCM.

 Matokeo  ni  kama  ifuatavyo
1.Magufuli.....87%
2. Amina.......10%
3.Migiro......3%

Endelea kufuatilia kupitia hapa hapa kwenye blog yako ya kijamii

Jumamosi, 11 Julai 2015

CHAMA CHA AKIBA NA MIKOPO TAZARA MBEYA SACCOS LTD KIMETOA MIKOPO KWA WANACHAMA WAKE YENYE THAMANI YA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 60

WAFUATAO NI BAADHI YA WANACHAMA WALIONUFAIKA NA MIKOPO HIYO.
Bwana Yusto Barnabas (kushoto)

Bi.Teddy Ndimbo

Bwana Luka Mahenge (kushoto)

 Bi. Bupe Kalinga

Bwana. Godfrey Mwakalindile (Kulia)

Bi. Rose Mwandiwa (Kulia)

Bi. Erikanali Nyari..(Kulia) akiwa badala ya Deborah Nyari

Bi. Salome Magwaza (katikati)

Endelea kutembelea blog hii kwa habari zaidi

HABARI KUBWA LEO-CCM KUMFIA KIKWETE WIKI HII?.MIPANGO YA KUASI CCM YAVUJA NI YAWASAKA URAIS,SOMA HAPO KUJUA


Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiongoza kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichofanyika hivi karibuni picha na maktaba.
HATMA ya Chama cha Mapinduzi CCM kuendelea salama au kufikia tamati na kuingia kwenye mpasuko mkubwa kutokana na Makada wake wanaotaka Urais ndani ya Chama hicho ni itabianika wiki hii.(Mtandao huu unaripoti) anandika KAROLI VINSENT endelea nayo
              Baada ya Kamati kuu ya chama hicho CC  kinachotarajiwa kukutana Alhamisi ya Terehe 9 ya wiki hii ambapo kwa mujibu ya Ratiba ya chama hicho inaonyesha pamoja na mambo mengine kamati itakuwa na jukumu moja tu la  “Kufyeka” majina ya takribani 38 ya makada walioomba ridhaa ya kutaka urais kwenye Chama hicho na kubakisha majina matano.
        Taarifa kutoka ndani ya CCM zinasema kwa sasa chama hicho kipo kwenye presha kubwa kutoka kwa makada wake ambao wamejiapiza kwa udi na Uvumba lazima wapite na kuwa Mgombea wa Urais ambao taarifa zinasema Makada hao wanaojiapiza  ni wale wanakubwa na Kashfa za ufisadi pamoja na kukiuka kanuni za chama.
        Makada hao wakiongozwa na Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa Ufisadi wa Kampuni ya tata ya kufua Umeme ya Richmound Edward Lowassa ambaye mara kwa mara kupitia Kambi zake kwamba akisema “hakuna wakulita jina lake ndani ya CC”
          Mbali na Lowassa Kada mwengine wa CCM ambaye amekuwa akijiipiza pia hakuna wakulikata jina lake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimatifa Benard Membe  ambapo naye amekuwa ajisifu kuwa lazima apite na kuwa Rais.
       Kwa Mujibu wa Vyanzo vyetu vilivyopo ndani ya CCM zinasema kwa sasa chama hicho,kimekuwa na Presha kubwa ambapo kwa sasa wanatafakari ni njia gani watatumia kuwachagua wagombe ambapo watakiaacha chama hicho  salama,
   “Yaani wiki hii ndio chama chetu  kitakuwa salama au ndio kitameguka maana kwa sasa chama kimekuwa na makundi makubwa sana ambayo kusema kweli hata kamati kuu sijui itakuja na jibu gani,ukitazama kuna makada wengi wamekubwa na kashfa kubwa za ufisadi wamekuwa ana nguvu tena wamepanga hata kufanya uasi endapo majina yao yatakatwa”
   Taarifa zanasema Kada ambaye amekuwa akiogopesha Chama hicho ni Edward Lowassa ambapo  kwa sasa amekuwa na Nguvu kubwa sana ndani ya chama hicho kutokana na mipango ambaye ameiandaa,
        “Huyu bwana kusema kweli basi tena hawamuwezi,maana amekuwa na makundi makubwa ndani ya chama chetu amewanunua wajumbe wa Mkutano mkuu kwa pesa nyingi sana,yaani amevunja kanuni ya wazi za chama,amejigeuza kama kiongozi mkuu wa chama,yaani mapaka sasa chama kinamwogopa sana”
     Kwa mujibu taarifa kutoka kambi ya Lowassa zinasema kwa sasa wamepanga hata kufanya “uasi”endapo kamati kuu ya CCM wakimkata mgombea wao.
        “Sisi tunangojea kwa hamu siku hiyo ya tarehe 9 ndugu,ndio utaona makubwa hapa nchini,yaani tunajua kwenye kamati ya CC  kunawatu hawamtaki Lowassa na wamepanga kumkata jina lake,nakuhakikishia hatukubali na ukitaka kuamini ngojea uone”
              Kwa mujibu wa ratiba ya CCM inaonyesha baada ya kamati kuu ya ccm kupendekeza majina matano,kinachofuata ni Halmashauri kuu ya chama cha Mapinduzi CCM nayo itayakata majina mawili kati ya matano na kubakiza majina matatu ambayo yanapigiwa kura siku ya tarehe 11 na 12 ya jumamosi na jumapili na kupatikana mgombea Mmoja wa Urais pamoja na Makamu wake.
     Taarifa za kiuchunguzi kutoka ndani ya Kambi ya Lowassa zinasema endapo Lowassa akipitishwa na Kamati kuu CC kinachofuata ni kutafuta kura za wajumbe 175 wa NEC kwa udi na Uvumba.

“Ujue sisi tunajua kabisa Lowassa akipita tu CC tayari Safari ya Matumaini imefanikiwa maana tumeshapata kura 175 za wajumbe wa NEC basi tumefanikiwa nakuhakishishi tutazipata kura hizo,tatizo ni kamati kuu ndugu,”

Jumatatu, 1 Juni 2015

NDOA ZA JINSIA MOJA ZAPATA KIBARI...SHERIA MPYA YAANZISHWA

Kinara mkuu wa chama cha upinzani cha Labour nchini Australia, ameanzisha sheria inayokubalia ndoa ya wapenzi wa jinsia moja, sheria ambayo inapingwa na Waziri mkuu wa nchi hiyo, Tony Abbott.
Kiongozi huyo, Bill Shorten, amemtaka Bwana Abbott kuwakubalia wanachama wa serikali wawe na uhuru wa kupiga kura kuhusiana na swala hilo.
Abbot ambaye ni mfuasi wa kanisa katoliki alikataa kura ya uhuru wa ndoa za jinsia moja na kusema kuwa lengo lake kuu ni kuimarisha uchumi na usalama wa taifa.
***chanzo na BBC Swahili***

KAZI YA KUTANGAZA NIA NDANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) BADO INAENDELEA...NI ZAMU YA MWANDOSYA MBEYA


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (Kazi Maalum), Profesa Mark Mwandosya.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (Kazi Maalum), Profesa Mark Mwandosya, anatarajia kutangaza nia ya kugombea urais leo Juni Mosi na kuchukua fomu Juni tatu mwaka huu
.

Jumatano, 25 Februari 2015

HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA JANA KATIKA MJI MDOGO WA ILULA NJE KIDOGO YA MJI WA IRINGA


WANANCHI WALIAMUA KUCHOMA KITUO CHA POLISI NA KUZIBA BARABARA KUU YA IRINGA-DSM KWA KUCHUKIZWA NA POLISI KUMUUA MAMA MMOJA MFANYABIASHARA KATIKA MJI HUO!

Alhamisi, 22 Januari 2015

ROSE MUHANDO JELA MIAKA SABA KWA TUHUMA ZA KUTOA MIMBA YA MIEZI SABA.





Rose Muhando.

KITENDO cha mwimbaji nyota wa muziki wa Injili, Rose Muhando (pichani) kudaiwa kutoa mimba ya miezi saba, endapo kitathibitishwa na mamlaka zinazohusika, kinaweza kusababisha kupewa adhabu ya kifungo cha miaka 7 jela, Risasi Jumatano lina mkanda kamili.

Mwimbaji nyota wa muziki wa Injili, Rose Muhando akiimba wakati akiwa mjamzito.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, ilidaiwa kuwa Rose, mwimbaji mwenye maskani yake mjini Dodoma, alikuwa ameitoa mimba aliyokuwa nayo, ambayo anadaiwa kupewa na mcheza shoo wake. Kama ingeenda salama na kujifungua, ingempatia mtoto wake wa nne.


Kufuatia madai hayo, gazeti hili lilifanya mawasiliano na wadau kadhaa, miongoni mwao wakiwa ni wanasheria, wanamuziki wenzake na viongozi juu ya ishu hiyo iliyoushtua ulimwengu wa Injili.

Mwanasheria mmoja maarufu nchini, ambaye aliomba hifadhi ya jina lake kwa sababu alizodai ni za kimaslahi, alisema kutoa mimba ni kosa kisheria na wahusika, akiwemo mama na daktari aliyeshiriki kukamilisha tukio hilo, wanapaswa kushtakiwa na kuhukumiwa.


“Inategemea, kama alitoa mimba kwa sababu za kimatibabu, yaani ili afya yake iwe sawa ni lazima atoe ujauzito alionao, hilo siyo kosa, lakini kama alitoa kwa sababu nyinginezo nje ya hapo, ni kosa la jinai linalostahili adhabu.

“Kwa mujibu wa Sheria za Kanuni ya Adhabu sura ya 16, kifungu cha 150, daktari anayehusika na kosa hilo adhabu yake ni kifungo cha miaka 14 jela na mama aliyetolewa ujauzito huo, kwa mujibu wa kifungu cha 151, anastahili kifungo cha miaka saba jela,” alisema mwanasheria huyo.

Kuhusu sababu za kumfunga kwa miaka mingi daktari badala ya mama aliyetaka kutolewa, ‘lawyer’ huyo alisema hii inatokana na kiapo ambacho madaktari huapa ambacho kinawataka kulinda uhai wa mtu na pia ni kukiuka maadili ya kazi yao.


“Mahakama itakuwa kali zaidi kwa madaktari kwa sababu ya dhamana ya kiapo chao. Huu unakuwa ni mfano kwa madaktari wengine ili wasimamie maadili na viapo vyao,” alisema mwanasheria huyo.

Katibu wa Chama Cha waimba Injili, Stella Joel, alipoulizwa kuhusu maoni yake juu ya kadhia hiyo, alisema chama chao hakina taarifa za tukio hilo, lakini wanaweza kuchukua hatua kama Polisi watalifanyia kazi jambo hilo kwa vile ni kosa la kijinai.


“Kutoa mimba ni kosa la Jinai, kwa hiyo kama Polisi watalifanyia kazi, sisi tutatoa tamko na kuchukua hatua, kwa sasa hatuna la kufanya, tunasikia katika vyombo vya habari na mitandao, tukimuuliza anakataa,” alisema.

Waimbaji wenzake, Bahati Bukuku na Christina Shusho walionyesha kushangazwa na tukio hilo, wakidai limewashtua na halikutarajiwa.


“Rose ni mtu mzima, kama kweli tukio hili lipo, basi huo ni uamuzi wake na Mungu wake, inategemea na mapatano yao, kila mtu ana maamuzi yake ila nimeshtushwa sana,” alisema Bahati Bukuku.

Shusho alisema jambo hilo ni baya na kosa kisheria, lakini hata hivyo ni suala binafsi linalomhusu mhusika. 

Rose Mhando mwenyewe alitafutwa katika simu yake ya mkononi ili kusikia kauli yake juu ya suala hilo, lakini zaidi ya mara nne, simu yake iliita hadi kukatika pasipo kupokelewa.