Jumamosi, 31 Agosti 2013

TAZARA yagawanyika

Hapa ni Stesheni ya Shirika la Reli la Tanzania na Zambia Mbeya
Hawa ni Baadhi ya Wafanyakazi wa Stesheni mbalimbali wakiwa kwenye mshikamano kushinikiza uongozi wa shirika hilo kuwapa mishahara yao ya miezi minne sasa
Kwa nyuso za huzuni kabisa wanyakazi wa shirika la reli ya Tanzania na Zambia-Mbeya
Kushoto kwako ni mimi Alex Mwalyego nikijaribu kupata habari kadhaa kutoka kwa baadhi ya wafanyakazi wa shirika hilo
Hapa wafanyakazi wakiondoka kwa huzuni bila kupata jibu lolote nini hatima ya mishahara yao

IGP Mwema ameibiwa upanga wa dhahabu wa kilo tatu




Jeshi la Polisi limeingia katika kashfa nzito baada ya mkuu wake, Inspekta Jenerali Said Mwema, kuibiwa upanga wa dhahabu ambao ni mali ya Shirikisho la Wakuu wa Majeshi ya Polisi wa nchi za Kusini mwa Afrika (SARPCCO).

Upanga huo wenye uzito wa takriban kilo tatu na wenye thamani ya zaidi ya fedha za Tanzania Sh600 milioni, ni kielelezo kwa nchi inayokabidhiwa uongozi wa SARPCCO.

Mwaka jana Tanzania ilikuwa mwenyekiti wa SARPCCO, ambapo upanga huo ulikabidhiwa kwa IGP Mwema na Jenerali Magwashi Victoria ‘Riah’ Phiyega, ambaye ni Kamishna wa Taifa wa Polisi wa Afrika Kusini aliyekuwa amemaliza muda wake kwa wakati huo.

Hilo ni tukio la pili la wizi la mali zinazohusu ofisi ya IGP, ambapo mwaka jana ndani ya ofisi hiyo kuliibwa kompyuta ndogo (laptop), ikiwa na taarifa muhimu za kipolisi. Hadi sasa hakuna taarifa za kupatikana kwa kompyuta hiyo.

IGP Mwema alikabidhiwa upanga huo Septemba 5, 2012, katika mkutano saba wa SARPCCO uliofanyika Zanzibar na kuhudhuriwa na wakuu wa majeshi ya Polisi kutoka nchi 13, pamoja na mashirika ya kimataifa.

Upanga huo ambao unakwenda sambamba na bendera ya SARPCCO, ni moja ya vielelezo vya nchi iliyochaguliwa kuwa Mwenyekiti wa shirikisho hilo, ambaye moja kwa moja anakuwa ni Mkuu wa Jeshi la Polisi katika nchi husika.

Kwa mujibu wa taratibu za SARPCCO, vielelezo hivyo hutakiwa kuwekwa ofisini kwa kiongozi husika, ikiwa ni alama ya kila mgeni atakayeingia ofisini hapo kutambua uwepo wa wadhifa huo wa kimataifa.

Uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kuwa IGP aligundua kutoweka kwa upanga huo wiki iliyopita, wakati akijiandaa kwenda kuukabidhi kwa mwenyekiti mpya wa SARPCCO, ambaye ni IGP wa Namibia.

Taarifa za ndani ya jeshi hilo zilibaini kuwa, IGP alilazimika kuondoka bila upanga huo alipokwenda Namibia wiki iliyopita kuhudhuria mkutano wa nane wa SARPCCO, uliofanyika Jumapili iliyopita mjini Windhoek.

Kwa mujibu wa uchunguzi, IGP Mwema alikabidhi upanga unaofanana na huo ambao siyo wa dhahabu, alioazimwa kutoka kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi la Namibia, Inspekta Jenerali, Luteni Jenerali Sebastian Ndeitunga, na kukabidhiwa kama ishara ya kukabidhiwa uenyekiti wa SARPCCO kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Uchunguzi ulibaini kuwa IGP Mwema alitoa ahadi ya kurejesha upanga halisi ndani ya kipindi cha mwezi mmoja, au Serikali ya Tanzania italazimika kutengeneza mwingine kulipa uliopotea.

Uchunguzi wa gazeti hili unaonyesha kuwa kashfa hiyo ametupiwa Mkuu wa Polisi Zanzibar, Kamishna Mussa Ali Mussa pamoja na dereva wake, ikidaiwa kuwa upanga huo baada ya kupokewa na IGP Mwema, Septemba mwaka jana uliwekwa kwenye gari la kamishna huyo.

Kichwa cha binadamu chapatikana katika ofisi ya mkuu wa polisi

Polisi nchini Kenya
Polisi nchini Kenya wanachunguza kisa ambacho kichwa cha mtu aliyeuawa kilipatikana kimewekwa nje ya afisi ya mwenyekiti wa tume ya kitaifa ya polisi Johnston Kavuludi jijini Nairobi.
Kifurushi hichi kilichokuwa kimefungwa kwa karatasi ya plastiki, vilevile kilikuwa na mikono miwli ya binadamy iliyojaa damu.
kando ya kifurishi hicho kulikuwa na ilaani iliyoandiskwa ''Kavuludi wewe ndiye utakayefuata''.
Tangu uteuzi wake, kamishna huyo ameongoza harakati za kujaribu kuifanyia marekebisho idara ya polisi ambayo inadaiwa kuwa fisadi zaidi Afrika Mashariki.
Kwa mujibu wa idara ya polisi, hakuna mshukiwa aliyekamatwa kauhusiana na tukio hilo na kuwa bado wangali wanachunguza mwili huo ulikuwa wa nani.
Katika miezi ya hivi karibuni kumekuwa na uhasama kati ya tume hiyo inayoongozwa na Kavuludi na ofisi ya mkuu wa polisi, huku zikilumbana kuhusu nani ana madaraka ya kuliendesha idara hiyo.

Chanzo na BBC Swahili

Chelsea yashindwa kutamba mbele ya Bayern URFA Super CUP



Hivi ndivyo ilivyokuwa kwenye mechi ya jana...Ndani ya Dak 90 timu hizo zilikuwa (2-2)

Wachezaji wa Bayern wakifurahia ushindi wao baada ya kuiondosha Chelsea kwa Penalty (5-4) baada ya Rumelo Lukaku kukosa Penalty ya mwisho

Ijumaa, 30 Agosti 2013

Maandamano kufanyika Misri licha ya kitisho cha serikali

Matukio ya Kisiasa

Maandamano kufanyika Misri licha ya kitisho cha serikali

Chama cha Udugu wa Kiislamu kimepanga kuandamana baada ya sala ya Ijumaa dhidi ya serikali ya mpito nchini humo. Maandamano hayo yameitishwa licha ya serikali kutishia kutumia nguvu kupambana na waandamanaji.
Maandamano haya ya leo yanatarajiwa kupima ni kwa kiwango gani vikosi vya usalama vimelidhoofisha kundi hilo na hii itajulikana tu kwa namna watu watakavyojitokeza katika maandamano hayo.
Kulingana na wakaazi huko, maandamano ya leo yanahofiwa kuzua machafuko zaidi katika nchi hiyo iliyokumbwa na msukosuko wa kisiasa.
Maandamano Misri Maandamano Misri
Umwagikaji mkubwa wa damu ulishuhudiwa wiki mbili zilizopita baada ya polisi kushambulia kambi za waandamanaji waliokuwa wanapinga hatua iliyochukuliwa Julai 3 ya kumuondoa madarakani kiongozi wao Mohammed Mursi kwa njia ya mapindzi ya kijeshi.
Hali hiyo ilisababisha vurugu ya wiki nzima zilizowauwa watu takriban 1,000, wengi wao wakiwa wafuasi wa Mursi. Inadaiwa kuwa baadhi ya wafuasi hao walijibu mashambulizi kwa kuchoma makanisa, majengo ya serikali na pia kushambulia vituo vya polisi.
Pande zote mbili zaombwa kusuluhisha tofauti zao
Katika mahojiano na shirika la habari la Associated Press, kiongozi wa kundi lililokuwa la waasi la Gamaa Islamiya, Abboud el-Zommor, alizihimiza pande zote mbili serikali na upinzani kukaa pamoja na kutatua tofauti zao ili kusimamisha umwagikaji wa damu nchini humo.
Huku hayo yakiarifiwa serikali imeongeza majeshi yake katika maeneo tofauti nchini humo huku ikilishutumu kundi la Udugu wa Kiislamu kuitisha maandamano na kuzua ghasia.
Kiongozi wa Udugu wa Kiislamu Mohamed El-Beltagi Kiongozi wa Udugu wa Kiislamu Mohamed El-Beltagi
Wakati huo huo utawala wa Misri umeendelea kuwakamata viongozi wa kundi hilo kwa madai ya kuchochea ghasia. Tayari viongozi wawili, Mohammed el-Beltagy na Khaled el-Azhari, walikamatwa hapo jana.
Polisi wanasema waliwakamata kwa sababu ya kuchochea maandamano na kuteswa kwa polisi aliyekamatwa na waandamanaji mjini Cairo.
Kwa upande wake. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Misri imesema itapambana vikali na watu ambao wanajaribu kuyumbisha usalama wa nchi na kwamba polisi wamepewa amri ya kutumia nguvu katika kulinda mali ya umma na ile ya watu binafsi nchini humo.
Wizara hiyo imesema pia kuwa maandamano ya leo yana lengo la kusababisha vurugu.
Mwandishi: Amina Abubakar/Reuters/AP
Mhariri: Mohammed Khelef

DIAMOND AFANYA MAKUBWA KATIKA UZINDUZI WA VIDEO YAKE, AMKABIDHI GARI MUHIDIN GURUMO

1 1Mwanamuziki Diamond Platnum akimkabidhi funguo ya gari aina ya Toyota Funcargo mwanamuziki mkongwe nchini mzee Muhidin Gurumo kama zawadi yake kwa mkongwe huyo wa muziki baada ya kustaafu rasmi kuimba muziki, Diamond alitoa zawadi hiyo kwa Gurumo katika hafla yake ya uzinduzi wa video yake mpya ya wimbo Nomber One aliyoirekodi huko Afrika Kusini ikigharimu kiasi cha dola elfu 30.000 zaidi ya milioni arobaini za Tanzania, Video hiyo imetengenezwa kwa viwango vya kimataifa na itaweza kumtangaza vyema kijana huyo wa kitanzania katika ulimwengu wa muziki hasa kimataifa, Hafla hiyo imefanyika kwenye hoteli ya Serena Dar es salaam na imehudhuriwa na wasanii pamoja na waigizaji wa filamu na watu maarufu mbalimbali
Mzee  Muhidin Gurumo akimshukuru Diamond kwa kumzawadia gari jambo ambalo kwake ni kama ndoto kwakuwa amestaafu akiwa hana usafiri “Yaani sijui hata mke wangu nikimwambia atanielewaje manake ni jambo la kushangaza kwangu” Alisema mzee Gurumo 3Diamond akimuongoza mzee Gurumo kwenda kumuonyesha gari 5Diamond akimuonyesha Mzee Gurumo gari 6Akimuelekeza jambo baada ya mzee Gurumo kuingia kwenye gari 7 
Diamond akizungumza machache kushukuru mashabiki wake na watu mbalimbali waliomsaidia kufikia hapo alipo



Diamond na madansa wake wakitumbuiza katika hafla hiyo 10Wasanii mbalimbali pamoja na MaDJ walikuwepo katika hafla hiyo hapa ni Dully Sykes na MawanaFA wakiwa na baadhi ya MaDJ 11Maurice Njowoka kutoka Cocacola wa pili kutoka kushoto na Mwanamuziki AY wa tatu kutoka kushoto pamoja na wadau wengine wakiwa katika hafla hiyo 12 
Mwigizaji Jaquiline Wolper naye alitia timu  13Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka akiwa na mama yake Diamond 15Wadau mbalimbali wakiwa katika hafla hiyo 16 17Mzee Gurumo akihojiwa na waandishi wa habari 18Hawa marafiki zangu wakakumbushia miaka kadhaa waliyofunga ndoa kwa kulishana mishikaki ilipendeza katikati ni Nancy Sumari akishuhudia 19Kulia ni Irene Uwoya kushoto Salma Msangi  20Kushoto AY na Salama Jabir wakipiga story na wadau mbalimbali 21 22Kutoka kulia ni Raymond Kigosi, Irene Uwoya na JB wakiwa katika hafla hiyo.
9

Zitto Kabwe: Msiwaamini wanasiasa, chama tawala wala wapinzani

Photo: Zitto Kabwe: Watanzania, msiwaamini sana wanasiasa; wawe wa chama tawala au wapinzani (Kuhusu uwajibikaji)

Soma zaidi hapa => http://bit.ly/12S5U8A Kauli hii ameitoa leo katika kongamano la ufuatiliaji wa uwajibikaji Jamii ambapo yeye alikuwa akiongelea majukumu ya bunge katika kusimamia uwajibikaji. Mambo mengi aliyoongea yalikuwa ni yenye mwelekeo chanya isipokuwa hili la kutupa tahadhari ya kutowaamini wanasiasa, akisisitiza hata wa upinzani. Nyuma ya kauli hii kumejificha nadharia nyingi kutegemea na mtu atakavyoipokea. Kwa maana nyingine, kauli hii inaleta hisia kwamba, hata wale wa chama chake tusiwaamini pia. Kwa kuwa mheshimiwa ni miongoni mwa members hapa, najua ujumbe huu utamfikia. Nilitaka atoe ufafanuzi alikuwa anamaanisha nini kwa kauli yake hii.

Waanza kupigiana debe wao kwa wao

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais, asiyekuwa na wizara maalumu, Profesa Mark Mwandosya, amempigia debe Spika wa Bunge, Anne Makinda, akisema kuwa anafaa kuwa rais kutokana na sifa zake. Profesa Mwandosya alimwaga sifa hizo bungeni jana, wakati akiunga mkono Azimio la Bunge la kumpongeza Makinda, kutokana na kuchaguliwa kwake kuwa Rais wa Chama cha Mabunge ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola (CPA). Profesa Mwandosya, ambaye miaka ya nyuma alijitosa katika kinyang’anyiro cha urais, alisema Spika Makinda ana sifa zaidi ya kumi ambazo zinamtosheleza kuwa rais na kwamba ni watu wachache wenye sifa kama hizo. Akitaja sifa hizo, Profesa Mwandosya alisema Makinda ni mtu anayejiamini, mtenda haki, mchapakazi, mzoefu, msikivu, mbunifu, mwelewa, mvumilivu, mnyenyekevu na pia ni mtu mwenye msimamo. Alisema kutokana na sifa hizo, Makinda anafaa kuwa kiongozi wa ngazi ya juu katika nchi, huku akimtazama kuwa ni mwanamke tishio katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015. “Kwa namna ninavyomfahamu Spika Makinda ni tishio kwa uchaguzi wa rais mwaka 2015, kutokana na jinsi alivyokuwa na uwezo na mambo aliyowahi kulifanyia taifa hili. “Kuchaguliwa kwake kuwa rais wa CPA ni hatua muhimu na nzuri kwa wanawake wengi kuongezeka katika Bunge la mwaka 2015 kwa kufikia asilimia 55, kutokana na utendaji kazi wake uliotukuka,” alisema Profesa Mwandosya. Profesa Mwandosya, ambaye amekuwa serikalini kwa muda mrefu, mwaka 2005 alikuwa miongoni mwa wanachama wa CCM waliojitokeza kuwania urais.Hata hivyo, kutokana na mchujo, Mwandosya alifanikiwa kuingia katika tatu bora. Wengine walikuwa ni Dk. Salim Ahmed Salim, Rais Jakaya Kikwete. Naye Mbunge wa Viti Maalum, Anna Abdallah (CCM), alimwaga sifa kwa kiongozi huyo wa Bunge na kusema kuwa ni mwanamke shupavu atakayekuwa tishio katika uchaguzi mkuu ujao. Akichangia mjadala huo wa kumpongeza Spika, Anna Abdallah, alisema Makinda ni mwanamke mwenye uwezo wa kuongoza nafasi yoyote ya juu, ikiwemo urais wa nchi. Alisema kutokana na uzoefu wake katika uongozi hapa nchini, ameweza kuaminika hata nje ya nchi, jambo ambalo limemfanya kuchaguliwa kuwa Rais wa CPA. “Kwa muda mrefu nchi yetu imekuwa ikihubiri juu ya mwanamke kupewa fursa na hasa kama ana uwezo, sasa wenzetu CPA wameweza kuliona hili wamemchagua,” alisema. Mbunge huyo aliwataka wanawake kutojali maneno ya pembeni na sasa ni lazima jamii ikubali kumuamini mwanamke kwa kumpa nafasi ya juu ya uongozi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015. Awali akisoma Azimio hilo la Bunge, Mwenyekiti wa CPA-Tanzania, Mussa Azzan Zungu, alisema Spika Makinda alishika wadhifa huo baada ya kufanyika kwa mkutano wa 44 wa chama hicho. Zungu, ambaye ni Mbunge wa Ilala, alisema katika mkutano huo Bunge la Tanzania liliwakilishwa na wabunge wanane, akiwemo Spika Makinda na baadaye ulifanyika uchaguzi huo. Chanzo:Mtanzania

Ulaya:Arsenal na Man City wataweza?

Timu ya Arsenal wakati mgumu katika kombe la Klabu Bingwa
Timu ya Arsenal huenda ikawa na kibarua kigumu katika mechi za kutafuta nafasi ya kujitosa katika duru ya muondoano ya kombe la klabu bingwa bara ulaya.
Katika mechi za makundi vijana wa Arsene Wenger wamepangwa kundi moja na Borussia Dortmund ya Ujerumani, Olympic Marseille ya Ufaransa na Napoli kutoka Italy.
Arsenal waliingia katika duru ya makundi baada ya kuibandua timu ya Fenerbahce 5-0 katika mechi za mchujo zilizochezwa ugenini na nyumbani.
Timu nyegine ya Uingereza itakayo kuwa na wakati mgumu katika mechi hizo za makundi ni Celtic ya Scotland kwani imepangwa kucheza na mibabe ya soka Barcelona, AC Milan ya Italy na Ajax ya Uholanzi.
Jee Man City wataweza safari hii
Manchester City nao watalazimika kupepetana na bingwa wa kombe hilo la klabu bingwa ,Ulaya Bayern Munich, CSKA Moscow na Viktoria Plzen. Wapenzi wengi wa soka wanajiuliza je safari hii baada ya kupata kocha mpya mwenye uzoefu katika michuano hiyo ya kombe la klabu bingwa Manuel Pellegrini,Man City wataweza kupiga hatua na kuingia katika mechi za muondoano?
Kwa upande mwengine Kocha mpya wa Manchester United ,David Moyes hatakuwa na kazi kubwa sana kwani watapepetana na Shakhtar Donetsk, Bayer Leverkusen ya Ujerumani na Real Sociedad ya Uhispania.
Miongoni mwa timu za Uingereza ni Chelsea peke yake ndio yenye kazi nyepesi kwani katika kundi lao watamenyana na Schalke ya Ujerumani, FC Basel na Steaua Bucharest.
Mechi za kwanza za makundi zinapaswa kugaragawa kati ya Septemba17-18 mwaka huu.

Orodha kamili ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya

Group A: Manchester United, Shakhtar Donetsk, Bayer Leverkusen, Real Sociedad
Group B: Real Madrid, Juventus, Galatasaray, FC Copenhagen
Group C: Benfica, Paris St-Germain, Olympiakos, Anderlecht
Group D: Bayern Munich, CSKA Moscow, Manchester City, Viktoria Plzen
Group E: Chelsea, Schalke, FC Basel, Steaua Bucharest
Group F: Arsenal, Marseille, Borussia Dortmund, Napoli
Group G: Porto, Atletico Madrid, Zenit St Petersburg, Austria Vienna
Group H: Barcelona, AC Milan, Ajax, Celtic

Alhamisi, 29 Agosti 2013

Uingereza inaweza kushambulia Syria bila idhini ya UN

29 Agosti, 2013 - Saa 13:53 GMT

Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron
Uingereza huenda ikaanzisha mashambulio dhidi ya utawala wa Syria, bila kuungwa mkono na Umoja wa Mataifa.
Hayo ni kwa mujibu wa ushauri wa wataalamu wake wa masuala ya kisheria.
Ushauri huo unasema, mashambulio hayo yatahitajika ikiwa yatatekelezwa ili kuzuia raia kuuawa, hata ikiwa wanachama wa kudumu wa baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Urussi na Uchina zikitumia kura zao za turufu kupinga mikakati za kijeshi dhidi ya utawala wa Syria.
Maafisa wa ujasusi nchini Uingereza wamemueleza Waziri Mkuu, David Cameron kuwa, kuna uwezekano mkubwa kuwa serikali ya Syria ilihusika na shambulio la kemikali wiki iliyopita mjini Damascus.
Wabunge wa Uingereza wanatarajiwa kujadili suala hilo katika kikao chao cha leo jioni.
Serikali ya Syria imekana madai ya kutumia silaha za kemikali katika shambulio mjini Damascus tarehe 21 mwezi huu, ambapo mamia ya watu waliuawa.
Lakini Bwana Cameron anaamini kuwa kuna ushahidi wa kutosha kutoka wa maafisa wake wa ujasusi na pia kutoka kwa wanainchi kuhusu ukatili unaofanywa na utawala wa sasa wa Syria.
Ofisi ya Waziri mkuu wa Uingereza, imechapisha ripoti hiyo, kuambatana na ushauri wa mkuu wake wa sheria Dominic Grieve, inayotoa idhini ya mashambulio ya kijeshi ili kuzuia utumiaji wa silaha za kemikali siku zijazo, kuambatana na sheria za kimataifa.

Umoja wa Mataifa


Ban Ki-Moon
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon amesema atapokea ripoti kutoka kwa wachunguzi wake wa silaha, wanaochunguza ikiwa silaha za kemikali zilitumika nchini Syria.
Mamia ya watu wanaripotiwa kuuawa kwenye shambulio hilo, lililofanyika karibu na mji mkuu wa Damascus wiki iliyopita.
Rais wa Marekani Barack Obama, amesema hajaamua kuhusu mpango wa kuishambulia Syria kijeshi.
Mataifa mengine pia yanajadili hatua watakayo chukua na Uingereza imekuwa ikishinikiza baraza la Usalama la Usalama la Umoja wa Mataifa kuidhinisha azimio litakalihakisha raia wamelindwa nchini Syria.
Rais wa Syria Bashar al-Assad amesema taifa lake litajilinda kutokana na shambulio lolote kutoka kwa mataifa ya kigeni.

Syria kujilinda asema Assad


Ed Miliband
Awali Kiongozi wa chama cha Upinzani cha Labour, nchini Uingereza, Ed Miliband, amesema bunge la nchi hiyo halipaswi kuamua ikiwa itaidhinisha mzozo wa Syria kutatuliwa Kijeshi.
Milliband ameyasema hayo muda mfupi kabla ya bunge la Uingereza kupiga kura ikiwa Uingereza itaishambulia Syria, kufuatia madai ya kutumia silaha za kemikali mjini Damascus.
Waandishi wa habari wanasems serikali ya Uingereza inahofia huenda ikapoteza kura hiyo na hivyo kukosa idhini ya kuingilia mzozo huo wa Syria.
Milliband amesema wamejifunza mengi kutokana na maamuzi yaliyochukuliwa miaka ya zamani kama ule wa kuivamia Iraq.
Amesema jamii ya kimataifa inapaswa kuipa jopo maalum na wachunguzi wa Umoja wa Mataifa nafasi ya kufanya kazi yao.
Serikali ya Uingereza imesema ina habari za kujasusi kuhusu Syria na itachapisha ripoti hiyo na ushauri wa kisheria kabla ya mjadala huo kuanza bungeni.

RATIBA YA LIGI KUU BARA 2013/2014



 24.08.2013 1 YOUNG AFRICANS VS ASHANTI UNITED NATIONAL STADIUM DAR
 24.08.2013 2 MTIBWA SUGAR VS AZAM FC MANUNGU MOROGORO
 24.08.2013 3 JKT OLJORO VS COASTAL UNION SH. AMRI ABEID ARUSHA
 24.08.2013 4 MGAMBO JKT VS JKT RUVU  MKWAKWANI TANGA
 24.08.2013 5 RHINO RANGERS VS  SIMBA SC A.H. MWINYI TABORA
 24.08.2013 6 MBEYA CITY VS KAGERA SUGAR SOKOINE MBEYA
 24.08.2013 7 RUVU SHOOTINGS VS TANZANIA PRISONS MABATINI PWANI
  
 28.08.2013 8 MTIBWA SUGAR VS KAGERA SUGAR MANUNGU MOROGORO
 28.08.2013 9 RHINO RANGERS VS AZAM FC A.H. MWINYI TABORA
 28.08.2013 10 JKT RUVU VS TANZANIA PRISONS MABATINI PWANI
 28.08.2013 11 MBEYA CITY VS RUVU SHOOTINGS SOKOINE MBEYA
 28.08.2013 12 MGAMBO JKT VS ASHANTI UNITED MKWAKWANI TANGA
 28.08.2013 13 JKT OLJORO VS SIMBA SC SH. AMRI ABEID ARUSHA
 28.08.2013 14 YOUNG AFRICANS VS COASTAL UNION NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
(29.August-09.Sept. National Team Camp for WCQ against Gambia away)  
14.09.2013 15 SIMBA SC VS MTIBWA SUGAR NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
14.09.2013 16 COASTAL UNION VS TANZANIA PRISONS MKWAKWANI TANGA
14.09.2013 17 RUVU SHOOTINGS VS MGAMBO JKT MABATINI  PWANI
14.09.2013 18 JKT OLJORO VS RHINO RANGERS SH. AMRI ABEID ARUSHA
14.09.2013 19 MBEYA CITY VS YOUNG AFRICANS SOKOINE MBEYA
14.09.2013 20 KAGERA SUGAR VS AZAM FC KAITABA KAGERA
14.09.2013 21 ASHANTI UNITED VS JKT RUVU AZAM COMPLEX DAR ES SALAAM
  
18.09.2013 22 TANZANIA PRISONS VS YOUNG AFRICANS SOKOINE MBEYA
18.09.2013 23 SIMBA SC VS MGAMBO JKT NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
18.09.2013 24 KAGERA SUGAR VS  JKT OLJORO KAITABA KAGERA
18.09.2013 25 AZAM FC VS ASHANTI UNITED AZAM COMPLEX DAR ES SALAAM
18.09.2013 26 COASTAL UNION VS RHINO RANGERS MKWAKWANI TANGA
18.09.2013 27 MTIBWA SUGAR VS MBEYA CITY MANUNGU MOROGORO
18.09.2013 28 RUVU SHOOTINGS VS JKT RUVU MABATINI PWANI
  
21.09.2013 29 MGAMBO JKT VS RHINO RANGERS MKWAKWANI  TANGA
21.09.2013 30 TANZANIA PRISONS VS MTIBWA SUGAR SOKOINE MBEYA
22.09.2013 31 JKT RUVU VS JKT OLJORO AZAM COMPLEX DAR ES SALAAM
21.09.2013 32 SIMBA SC VS MBEYA CITY NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
22.09.2013 33 AZAM FC VS YOUNG AFRICANS NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
21.09.2013 34 KAGERA SUGAR VS ASHANTI UNITED KAITABA KAGERA
22.09.2013 35 COASTAL UNION VS RUVU SHOOTINGS MKWAKWANI  TANGA
  
 28.09.2013 36 YOUNG AFRICANS VS RUVU SHOOTINGS NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
 28.09.2013 37 RHINO RANGERS VS KAGERA SUGAR A. H. MWINYI TABORA
 29.09.2013 38 ASHANTI UNITED VS MTIBWA SUGAR AZAM COMPLEX DAR ES SALAAM
 28.09.2013 39 MBEYA CITY VS COASTAL UNION SOKOINE MBEYA
 28.09.2013 40 MGAMBO JKT VS JKT OLJORO MKWAKWANI TANGA
 29.09.2013 41 JKT RUVU VS SIMBA SC NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
 29.09.2013 42 TANZANIA PRISONS VS AZAM FC SOKOINE MBEYA
  
 05.10.2013 43 RUVU SHOOTINGS VS SIMBA SC NATIONAL STADIUM DAR ES  SALAAM
 05.10.2013 44 JKT RUVU VS KAGERA SUGAR AZAM COMPLEX DAR ES  SALAAM
 05.10.2013 45 COASTAL UNION VS AZAM FC MKWAKWANI TANGA
 05.10.2013 46 JKT OLJORO VS MBEYA CITY SH. AMRI ABEID ARUSHA
 25.09.2013 47 RHINO RANGERS VS ASHANTI UNITED A. H. MWINYI TABORA
 06.10.2013 48 MGAMBO JKT  VS TANZANIA PRISONS MKWAKWANI TANGA
 06.10.2013 49 YOUNG AFRICANS VS MTIBWA SUGAR NATIONAL STADIUM DAR ES  SALAAM
  
09.10.2013 50 RHINO RANGERS VS MBEYA CITY A. H. MWINYI TABORA
09.10.2013 51 JKT OLJORO VS RUVU SHOOTINGS SH. AMRI ABEID ARUSHA
09.10.2013 52 AZAM FC VS MGAMBO JKT AZAM COMPLEX DAR ES SALAAM
09.10.2013 53 MTIBWA SUGAR VS JKT RUVU MANUNGU MOROGORO
12.10.2013 54 KAGERA SUGAR VS YOUNG AFRICANS KAITABA KAGERA
12.10.2013 55 SIMBA SC VS TANZANIA PRISONS NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
13.10.2013 56 ASHANTI UNITED VS COASTAL UNION AZAM COMPLEX DAR ES SALAAM
  
 13.10.2013 57 RUVU SHOOTINGS VS RHINO RANGERS MABATINI PWANI
 13.10.2013 58 MGAMBO JKT VS MBEYA CITY MKWAKWANI TANGA
 13.10.2013 59 AZAM FC VS JKT RUVU AZAM COMPLEX DAR ES SALAAM
 13.10.2013 60 MTIBWA SUGAR VS JKT OLJORO MANUNGU MOROGORO
 16.10.2013 61 ASHANTI UNITED VS TANZANIA PRISONS AZAM COMPLEX DAR ES SALAAM
 19.10.2013 62 KAGERA SUGAR VS COASTAL UNION KAITABA KAGERA
 20.10.2013 63 SIMBA SC  VS YOUNG AFRICANS NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
  
 19.10.2013 64 JKT OLJORO  VS AZAM FC SH. AMRI ABEID ARUSHA
 19.10.2013 65 MTIBWA SUGAR VS MGAMBO JKT MANUNGU MOROGORO
 19.10.2013 66 MBEYA CITY VS JKT RUVU SOKOINE MBEYA
 19.10.2013 67 ASHANTI UNITED VS RUVU SHOOTINGS AZAM COMPLEX DAR ES SALAAM
 23.10.2013 68 COASTAL UNION VS SIMBA SC MKWAKWANI TANGA
 23.10.2013 69 TANZANIA PRISONS VS KAGERA SUGAR SOKOINE MBEYA
 23.10.2013 70 YOUNG AFRICANS VS RHINO RANGERS NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
  
 26.10.2013 71 TANZANIA PRISONS VS MBEYA CITY SOKOINE MBEYA
 26.10.2013 72 COASTAL UNION VS MTIBWA SUGAR MKWAKWANI TANGA
 26.10.2013 73 JKT OLJORO VS ASHANTI UNITED SH. AMRI ABEID ARUSHA
 26.10.2013 74 YOUNG AFRICANS VS MGAMBO JKT NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
 27.10.2013 75 RUVU SHOOTINGS VS KAGERA SUGAR MABATINI PWANI
 27.10.2013 76 SIMBA SC VS AZAM FC NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
 27.10.2013 77 RHINO RANGERS VS JKT RUVU A. H. MWINYI TABORA
  
 30.10.2013 78 MGAMBO JKT  VS COASTAL UNION MKWAKWANI TANGA
 30.10.2013 79 TANZANIA PRISONS VS JKT OLJORO SOKOINE  MBEYA
 30.10.2013 80 AZAM FC VS RUVU SHOOTINGS AZAM COMPLEX DAR ES SALAAM
 30.10.2013 81 SIMBA SC VS KAGERA SUGAR NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
 30.10.2013 82 MTIBWA SUGAR VS RHINO RANGERS MANUNGU MOROGORO
 30.10.2013 83 MBEYA CITY VS ASHANTI UNITED SOKOINE  MBEYA
 31.10.2013 84 JKT RUVU VS YOUNG AFRICANS NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
  
 02.11.2013 85 JKT RUVU VS COASTAL UNION AZAM COMPLEX DAR ES SALAAM
 02.11.2013 86 ASHANTI UNITED VS SIMBA SC NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM
 03.11.2013 87 KAGERA SUGAR VS MGAMBO JKT KAITABA KAGERA
 03.11.2013 88 AZAM FC VS MBEYA CITY AZAM COMPLEX DAR ES SALAAM
 03.11.2013 89 RHINO RANGERS VS TANZANIA PRISONS A. H. MWINYI TABORA
 03.11.2013 90 RUVU SHOOTINGS VS MTIBWA SUGAR MABATINI PWANI
 03.11.2013 91 YOUNG AFRICANS VS JKT OLJORO NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM

Ijumaa, 23 Agosti 2013

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

 

Dar es Salaam. Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge.
Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012.
Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni.
“Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. Tunajua kwamba fedha hizi zilipunguzwa kiasi cha Sh95 bilioni na kupelekwa Wizara ya Uchukuzi, zilibakia Sh252.975bilioni katika kifungu hicho lakini kuna bilioni 100 zimetumika visivyo,” alisema Zitto, ambaye pia ni Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini (Chadema).
Alisema katika majumuisho ya Bajeti ya wizara hiyo, Dk Magufuli na Dk Mwakyembe wakati huo akiwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Lukuvi walitoa maelezo yasiyo ya kweli bungeni kuhusu fedha.
Alikariri maneno yaliyorekodiwa kwenye Hansard ya Bunge yaliyosemwa na viongozi hao watatu.
“Tunaomba fedha Sh252 bilioni kwa ajili ya kuanzia kazi za ujenzi wa barabara,” Zitto alisema akikariri maneno ya Dk Magufuli wakati anawasilisha bajeti.
“Fedha hizi zitachangia miradi ya wafadhili,” haya yalikuwa maneno ya Dk Mwakyembe wakati akifanya majumuisho.
“Hizi ni fedha kwa ajili ya counterpart fund,” alimkariri Lukuvi wakati akichangia hotuba ya wizara hiyo.
Zitto alisema CAG alihoji mwaka huu kuhusu matumizi ya fedha hizo na alitoa taarifa akidai kuwa fedha hizo zilikuwa miradi hewa na kasma kivuli.
Zitto alisema kuwa Dk Magufuli na Katibu Mkuu wake walipohojiwa walidai kutumia fedha hizo kulipa madeni.
“Kwa nini mlidanganya Bunge? Mliomba fedha za kuanza miradi maalumu. Hamkuomba fedha za madeni. Kwa nini mliunda kasma kivuli na kuifuta baada ya pesa kulipwa?” Zitto alimhoji Balozi Mrango.
Katika majibu yake, Balozi Mrango alisema kwa nia njema, fedha hizo zilitumika kuwalipa makandarasi waliokuwa wamechachamaa, huku baadhi yao wakisisitiza kusitisha kuendelea na miradi. Hivyo wakalazimika kuomba fedha kwa njia hiyo ili miradi kuendelea katika maeneo mbalimbali ya nchi.
Zitto hakuridhishwa na majibu hayo akisema hapakuwa na haja ya kutumia fedha hizo kuwalipa makandarasi wakati kulikuwa na kasma yao ya awali. Alisema kama kulikuwa na haja hiyo, wizara isingeita mradi rasmi.
“Jambo hili siyo sahihi hata kidogo kulidanganya Bunge na hadi sasa wewe na waziri wako hamuonyeshi kukubali kosa hili, hata Waziri Lukuvi naye alisisitiza bungeni kwamba fedha hizo zinaombwa ili kutekeleza mradi maalumu lakini sasa imebainika sivyo, kwa mujibu wa Kanuni za Bunge tutawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ili wahojiwe nao wajieleze kwa kulidanganya,” alisema Zitto.
Pia kamati hiyo imeitaka wizara hiyo kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu matumizi ya Sh100 bilioni zilizotumika kinyume na maombi yaliyowasilishwa kwenye Bajeti ya mwaka huo wa fedha.
CAG ameshauri madeni yote ambayo Wizara ya Ujenzi inadaiwa yaorodheshwe ili yawe wazi kuepuka migongano katika matumizi ya fedha.
Alipoulizwa kuhusu madai hayo, Lukuvi alisema haelewi chochote na kusisitiza kuwa akipata taarifa rasmi za Kamati ya PAC, atatoa ufafanuzi.
Halmashauri zinavyotafuna mabilioni
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAACc), imeeleza namna mamilioni ya fedha za Serikali zinavyoibwa kutoka Hazina kupitia halmashauri za wilaya huku Ilala ikitajwa kuongoza kwa ufisadi huo.
Mwenyekiti wa LAAC, Rajab Mbarouk Mohammed aliwaambia waandishi wa habari jana kwamba Hazina imekuwa ikipeleka fedha kwenye halmashauri zikiwa zimezidi na kwamba kiasi kinachozidi hakirudishwi badala yake huliwa.
Alisema kamati hiyo imefanya uchunguzi kwenye halmashauri 43 na kubaini kwamba mtindo huo ndiyo unaotumika kuiba fedha za Serikali.
“Mwaka 2011/12 kiasi cha Sh1.5 bilioni zilipelekwa zikiwa zimezidi kwenye halmashauri hizo lakini hazikurudishwa Hazina kama inavyoonyesha kwenye ripoti ya CAG.
Alisema kati ya kiasi hicho, Halmashauri ya Manispaa ya Ilala ilipewa ziada ya Sh213 milioni ikifuatiwa na Geita iliyopewa Sh129 milioni.
“Fedha hizo za mishahara zilipelekwa kwenye halmashauri hizo na Hazina kimakosa zikiwa zimezidi lakini watendaji wa hawakuzirudisha kama wanavyotakiwa kisheria badala yake zikayeyuka,” alisema.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa uchunguzi huo pia ulibaini kwamba katika halmashauri hizo 43 kiasi cha Sh693 milioni hulipwa mishahara hewa ambayo wafanyakazi wake walishakufa na wengine kustaafu.
Alisema Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ililipa mishahara hewa yenye thamani ya Sh79.4 milioni ikifuatiwa na Ukerewe iliyolipa Sh57.5 milioni.
Kwa upande wa fedha za miradi ya maendeleo, mwaka 2011/12, Hazina ilipeleka katika Halmashauri ya Mbarali, Mbeya Sh724 milioni kwa ajili ya Mradi wa Maendeleo ya Elimu Sekondari wakati mradi huo ulikuwa ukihitaji Sh70 milioni tu.
“Kiasi cha Sh654 milioni zilipelekwa kimakosa na Hazina lakini badala ya kurudishwa zilitumiwa katika mazingira ya kutatanisha,” alisema.
Alisema Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe ilipelekewa ziada ya Sh500 milioni na Mvomero ilipewa Sh85 milioni. “Kuna mtandao mkubwa wa Hazina na halmashauri ambao ukiachwa utaendelea kupoteza fedha nyingi za walipakodi,”

Ijumaa, 9 Agosti 2013

Wanyarwanda 520 watii agizo la Kikwete kuondoka nchini

Bukoba. Ngara. Zikiwa zimesalia saa 48 kabla ya kumalizika kwa muda uliotolewa na Rais Jakaya Kikwete kwa wahamiaji haramu kuondoka nchini au kuhalalisha ukaazi wao na wenye silaha kuzisalimisha, makundi ya wahamiaji hao, yameanza kuondoka kwa hiari.
Wastani wa wahamiaji haramu 150 wanaendelea kujiandikisha kuvuka mpaka katika Kituo cha Rusumo, Ngara mkoani Kagera kutekeleza agizo hilo.
Ofisa Uhamiaji wa Kituo cha Rusumo, Samweli Mahirane alisema mpaka sasa Wanyarwanda 520 wameshaondoka katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya Ngara na kurejea makwao huku Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Fabian Massawe akisema silaha 17 za aina mbalimbali zimesalimishwa.
Mahirane alisema wahamiaji hao wanatokea katika vijiji vya Wilaya za Ngara, Karagwe, Kyerwa, Biharamulo na Geita pamoja na Runzewe na wamekuwa wakiishi katika maeneo hayo bila vibali halali.
“Kuondoka kwa hiari kwa wahamiaji haramu, kutahitimishwa Jumatatu Agosti 12 na baada ya tarehe hiyo, vyombo vya dola vitaanza kufanya kazi kama agizo la Rais Kikwete lilivyoelekeza katika Mikoa ya Kagera na Kigoma,” alisema.
Aliwahakikishia wahamiaji hao usalama katika mataifa yao kwani hivi karibuni Serikali ya Rwanda ilikubali kuwapokea hata walio na mifugo kwa masharti kuwa ndani ya kipindi kifupi wataipunguza kwa kuiuza na kuboresha maisha yao.
“Rwanda wanahitaji mifugo michache, hivyo walio na mingi wanatakiwa kuipunguza kwa kuuza na kujenga makazi bora ikiwa ni pamoja na kuhifadhi ama kulinda mazingira ya nchi hiyo,” alisema Mahirane.