Kabla ya mchezo huo kuanza kulitokea vurugu za mashabiki baada ya
mashabiki wanaodhaniwa kuwa ni wa Mbeya City kulipiga mawe basi la Yanga
wakati linaingia uwanjani pamoja na gari dogo aina ya Noah lililokuwa
limebeba viongozi wa Yanga nalo lilipigwa mawe na kioo cha nyuma cha
gari kuvunjika.
Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga wamekata rufaa kwa
kamati ya Ligi kutaka mchezo wao dhidi ya Mbeya City uliofanyika
Jumamosi iliyopita urudiwe kwenye uwanja huru.
Katika mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa
Sokoine ulimalizika kwa sare ya 1-1 na kufanikiwa kuingiza Sh100 milioni
baada ya mashabiki 20,000 kushuhudia mechi hiyo.
Kabla ya mchezo huo kuanza kulitokea vurugu za
mashabiki baada ya mashabiki wanaodhaniwa kuwa ni wa Mbeya City kulipiga
mawe basi la Yanga wakati linaingia uwanjani pamoja na gari dogo aina
ya Noah lililokuwa limebeba viongozi wa Yanga nalo lilipigwa mawe na
kioo cha nyuma cha gari kuvunjika.
Wakizungumza jijini Mbeya, Ofisa habari wa Yanga,
Baraka Kizuguto akisaidiana na mjumbe wa kamati ya sekretarieti ya
Yanga, Patrick Naggi walisema, “Tunachohitaji mechi irudiwe na ichezwe
kwenye uwanja huru.”