Hayo yalisemwa jana na Kwesigabo akizitaja bidhaa za vyakula zilizochangiwa kupungua kwa
mfumuko wa bei na kiwango cha punguzo kwa asilimia katika mabano kuwa ni
pamoja na mikate na nafaka (2.2), vitafunwa (3.8), mahindi ( 1.6), unga
wa ngano (2.5), unga wa muhogo ( 0.6) na unga wa mtama (3.4).
Mfumuko wa bei nchini umezidi kupungua na sasa umefikia asilimia
6.7 kwa mwezi Agosti, 2013, kutoka asilimia 7.5, Ofisi ya Takwimu ya
Taifa (NBS) imebainisha, katika taarifa yake ya matokeo ya mfumuko wa
bei kwa mwezi Agosti.
Akizungumza na waandishi wa habari jana,
Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii wa NBS, Ephrahim Kwesigabo
alisema kupungua kwa mfumko huo wa bei kunamaanisha kuwa kasi ya
upandaji wa bei za bidhaa na huduma kwa mwezi Agosti imepungua
kulinganisha na mwezi Julai.
“Kwa kiasi kikubwa kupungua kwa mfumuko wa bei
nchini kumechangiwa na kupungua kwa