Alhamisi, 5 Septemba 2013

NI KIAMA: ATAFUNWA USO NA MWAJIRI WAKE NYUMBANI

KABLA ALIANZA KUNG'ATA ULIMI WA MBWA 


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida mkazi wa Kijiji cha Nyabibuye Kakongo katika Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma, Susuluka (16) anadaiwa kujeruhiwa vibaya usoni na bosi wake, Imani Paulo (36) kwa kung’atwa ng’atwa usoni na kisha kunyofolewa macho, pua na meno kubaki nje, kama ambavyo anaonekana pichani ukurasa wa mbele.

Tukio hilo ambalo tunaweza kulifananisha na dunia kuelekea kufika mwisho, limegusa hisia za watu wengi hasa wakazi wa Kibondo, huku wengine wakitokwa na machozi kutokana na kuguswa na ukatili ambao amefanyiwa kijana huyo.Tunaweza kufikiria kuwa tukio hilo ni sinema, lakini Mkuu wa Wilaya ya Kibondo, Venance Mwamotto, ameliambia Majira kuwa tukio hilo limetokea miezi miwili iliyopita.
Akizungumza na Majira katika mahojiano maalumu, Mwamotto, alisema kuwa kabla ya kijana huyo kujeruhiwa na bosi wake, alimtuma dukani ili akamnunulie soda.Aliliambia Majira kuwa baada ya kufika nyumbani alimkuta bosi wake akiwa amemkaba koo mbwa na kutokana na maumivu aliyokuwa akiyapata mbwa huyo, alianza kuhema akitoa ulimi nje.
DC Mwamotto alisema kuwa mtuhumiwa huyo ghafla alianza kuung’ata ulimi wa mbwa na kisha kumeza vipande jambo lililosababisha mbwa huyo kupiga kelele kutokana na maumivu.Aliongeza kuwa aliendelea kula vipande vya ulimi huo wa mbwa hadi alipoumaliza.
“Unaweza kusema kuwa ni uongo, lakini ni tukio la kweli kabisa kwani mshtakiwa huyo aliendelea kula ulimi wote wa mbwa, huku kijana huyo akiendelea kumshangaa bosi wake kutokana na kitendo hicho kilichosababisha mbwa huyo kufa,”Wakati akiendelea kumshangaa bosi wake ghafla alimrukia na kumkamata kwa nguvu na kuanza kumng’ata kama mtu anayetafuna hindi la kuchoma.
“Mshtakiwa huyo alianza kumtafuna jicho moja na kufuatia jicho la pili na kisha kumeza vipande vya macho huku akiendelea kumshika kwa nguvu,” alisema DC Mwamotto wakati wa mahojiano na Majira.
Baada ya kumaliza kitendo hicho alisema kuwa mshtakiwa huyo alianza kumng’ata pua na kisha kumeza na vipande.
Alisema kuwa wakati anaendelea na kitendo hicho majeruhi huyo alikuwa akipiga kelele za kuomba msaada, lakini mshtakiwa huyo alianza kumng’ata tena kipande cha mdomo wa chini na kisha kusababisha meno kubaki nje.“Kutokana na kelele hizo wananchi waliamua kusogea karibu, lakini walikuta tayari, Susuluka amejeruhiwa vibaya usoni huku damu zikimtoka kwa wingi,” alisema.
Mwamotto alisema kuwa kutokana na hali hiyo wananchi walimvamia na kumpiga na kumpeleka katika Kituo cha Polisi cha Kibondo na majeruhi walimkimbiza katika Hospitali ya Wilaya ya Kibondo.
Majira iliendelea na mahojiano hayo ambapo, mshtakiwa huyo alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya na kufunguliwa mashtaka ya kudhulu mwili.“Hivi sasa mshtakiwa yupo katika Gereza la Nyamisivi Kibondo, lakini cha kusikitisha tena akiwa huko alimng’ata na kula vipande vya nyama vya mguu mshtakiwa mwenzake,” alisema.
Alisema kuwa mshtakiwa mwenzake alimjeruhi vibaya na kupelekwa hospitalini hali iliyosababisha mshtakiwa huyo kutengwa na washtakiwa wenzake.“Mimi nimelazimika kwenda hadi gerezani na kufanya mahojiano na mshtakiwa huyu, kwani hili tukio linasikitisha sana lakini cha ajabu alitaka kufahamu je ameshtakiwa kwa makosa gani ya kuua mbwa au kumng’ata mtu,” alisema.
Alisema kuwa pia amelazimika kwenda kumjulia hali majeruhi huyo ambapo madaktari katika hospitali hiyo walishindwa kumtibia.“Nimeomba msaada kutoka Wizara ya Afya ili mgonjwa huyu akatibiwe India na tayari maandalizi yameanza kufanyika kwa kushirikiana na Hospitali ya Kibondo,” alisema.
Mwamotto alisema kuwa mgonjwa huyo hana pua, macho yamefumba, mdomo kwa kujeruhiwa vibaya usoni hali ambayo anahitaji matibabu zaidi....!

Chanzo: majira gazeti huru

Kiongozi wa kambi rasmi ya Upinzani Bungeni Mh Mbowe ametolewa nje ya Bunge

 Mh. Philemon Mbowe
Kiongozi wa kambi rasmi ya Upinzani Bungeni Mh Mbowe ametolewa nje ya Bunge, baada ya kukaidi amri ya Naibu spika Mh Ndugai alipomwamuru akae na Mh Mbowe kutokutii amri hiyo. Mh ngudai aliamuru askari wa Bunge kumtoa nje, hata hivyo baadaye wabunge karibu wote wa upinzani walitoka pia isipokuwa Mh. Augustin Mrema wa TLP. Upinzani Bungeni unadai muswada wa katiba 2013 unamapungufu.

Rooney awajibu wakosoaji wake

Jeraha alilopata Rooney
Wayne Rooney amechapisha picha ya jeraha alilopata kichwani baada ya wakosoaji wake kuhoji kujitolea kwake kuchezea timu ya taifa.

Rooney alijeruhiwa na mchezaji mwenzake wa Manchester United Phil Jones,kwa kumkanyaga kichwani na hivyo kumlazimisha kukaa nje ya mechi za England kufuzu kushiriki kombe la dunia zitakazochezwa Uijumaa na Jumanne.
Alisema kuwa baadhi ya watu wanaonekana kuhoji kujitolea kwake na kusema kuwa amejiondoa kwenye miuchuano ya kufuzu kwa kombe la dunia.

"nina uhakika watu wataona kwa nini sitaweza kucheza.''
Rooney, mwenye umri wa miaka 27, aliongeza kuwa hakuna sababu inayoweza kumzuia kuwasaidia wachezaji wenzake kuweza kufuzu kwa kombe la dunia.

Kocha mkuu wa Man United David Moyes alisema kuwa Rooney huenda asicheze kwa wiki tatu kutokana na jeraha alilopata Jumamosi kabla ya timu hiyo kushindwa na Liverpool, mechi ambayo Rooney hakuweza kucheza kutokana na jeraha.

Mchezaji mwenzake wa timu ya taifa Theo Walcott ameelezea kutishwa na picha hiyo akisema inafanana na picha zinazoonekana tu kwenye filamu.
Rooney ni mmoja wa wachezaji watatu ambao wamejiondoa kutoka kwenye kikosi cha timu ya taifa kwa sababu ya jeraha alilopata.
Wengine ni Glen Johnson na Jones.

Wabunge wa Chadema, NCCR-Mageuzi na CUF watoka nje

 
 Wabunge wa Vyama vya CUF, NCCR-Mageuzi, na Chadema wakitoka nje ya ukumbi wa Bunge kupinga muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba bungeni dodoma jana.

Dodoma.Wabunge wa Kambi ya Upinzani Bungeni jana jioni walitoka ndani ya Ukumbi wa Bunge, baada ya kupuuzwa kwa mwongozo wao wa kutaka kuahirishwa kujadiliwa kwa Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, hadi hapo Zanzibar itakaposhirikishwa.
Wabunge waliotoka bungeni jana yapata saa 12.15 ni kutoka vyama vya Chadema, CUF na NCCR-
 Mageuzi huku Mbunge wa Vunjo na Mwenyekiti wa Taifa wa Tanzania Labour Party (TLP, Augustine Mrema akiendelea kubaki ukumbini.
Kitendo cha wabunge hao wa upinzani kilionekana kuwakera baadhi ya wabunge wa CCM, ambao walisikika wakiwakejeli kwa kupiga meza huku wakisema: “Kwendeni zenu, tumewazoea.”
Wakati wabunge hao wakiondoka, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, alikuwa akiwasisitiza wabunge wanaobakia wawe watulivu, maana kuna usalama wa kutosha ndani ya ukumbi huo.

“Mnaotoka nimewaona wote na mnanijua,” alisikika Naibu Spika Ndugai akiwatahadharisha wabunge wa upinzani waliosusa mjadala huo.
Wabunge wa CCM waliendeleza vituko ambapo baada ya wapinzani kutoka, wabunge Juma Nkamia (Kondoa Kusini), Hilary Aeshi ( Sumbawanga Mjini) na Murtaza Mangungu (Kilwa Kaskazini) walikwenda kukaa katika viti vya kambi ya upinzani.

Kabla ya kutoka kwa wabunge hao wabunge wawili kutoka CUF waliomba mwongozo wa Spika, wakitaka muswada huo kuondolewa ili kuwapa nafasi Wanzanzibar kutoa maoni yao.
Mbunge wa Mkanyageni, Habib Mohamed Mnyaa (CUF) aliomba mwongozo akitaka muswada huo uondolewe, hadi hapo Wazanzibar watakaposikilizwa.
Alisema kuwa kwa maoni ya Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala wamesikiliza maoni ya wadau wengi, lakini Zanzibar hawakwenda kuwasikiliza wadau wa eneo hilo.

“Na hili suala zima katika masuala ya katiba linahitaji usawa wa washirika, tunazungumza kitu kinachohusiana na Zanzibar na Tanzania Bara, ili kupata maoni ya nchi nzima kuna uhalali gani wa Bunge hili kuendelea na mjadala huu?” alihoji.
Hata hivyo, alikatizwa na kelele za Mbunge wa Viti Maalumu, Pindi Chana (CCM), ambaye alitoa taarifa kuwa Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala ilialika wajumbe mbalimbali ikiwamo Zanzibar.

“Miongoni wa wajumbe walioalikwa ni pamoja na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Zanzibar pamoja na wadau mbalimbali ambao walikuja mbele ya Katiba,” alisema Pindi ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati hiyo........habari zaidi na Mwananchi Com.LTD

MICHUANO YA KOPA COCA COLA NYANDA ZA JUU KUSINI VIWANJA VYA IYUNGA -MBEYA

Iringa FC kopa Coca Cola Cup

Mwalimu wa Timu ya Iringa FC kopa Coca Cola akitoa maelekezo kwa vijana wake

 Mwalimu wa michezo timu ya Iringa FC Kopa Coca Cola

Timu Iringa Fc Kopa Coca Cola chini ya umri wa miaka 15

Vijana wa Iringa FC kopa Coca Cola wakifanya mazoezi katika viwanja vya Iyunga-Mbeya

MICHUANA YA KOPA COCA COLA CHINI YA MIAKA 15 IKIENDELEA KATIKA VIWANJA VYA IYUNGA-MBEYA

Timu ya Sumbawanga ikijinoa kwa mazoezi katika viwanja vya Iyunga-Mbeya
Sumbawanga FC Kopa Coca Cola

Nahodha wa timu ya Sumbawanga akiongoza mazoezi

Mwalimu wa michezo timu ya Sumbawanga FC kopa Coca Cola

Waalimu wa timu ya Sumbawanga wakitoa Mazoezi kwa vijana wao

Sumbawanga FC kopa Coca Cola

Wajua kwa nini unahitaji kulala?

Usingizi unasaidia kukuza celi za ubongo wako

Wanasayansi wanaamini kuwa wamepata sababu moja mpya ya kwa nini tunahitaji usingizi.
Wanasema kuwa kulala kunasaidia katika kujenga celi mpya za ubongo.
Usingizi unasaidia kuzalisha upya celi za ubongo ambazo nazo hujenga kemikali inayojulikana kama Myelin ambayo ni muhimu katika kulinda ubongo wetu kwa ambavyo unafanya kazi.

Matokeo ya utafiti huu ambayo yalijitokeza katika panya wa mahabara, huenda yakachochea maelezo zaidi kuhusu umuhimu wa usingizi katika kukabarabati celi za ubongo na kukuza celi mpya pamoja na kuulinda kutokana na magonjwa.
Daktari Chiara Cirelli na wenzake kutoka chuo kikuu cha Wisconsin waligundua kuwa Panya hao walipokuwa wanalala, ndipo kemilaki hiyo ilikuwa inatengezwa kwa wingi na celi za mwili.
Ongezeko la kemikali pia ilitegemea aina ya usingizi ambao Panya walilala hasa uliohusishwa na ndoto.

Kinyume na hilo, celi zilionekana kufariki wakati Panya walipokuwa wako macho wazi.

Na hii ndio maana usingizi ni muhimu jambo ambalo wamekuwa wakilihoji wanasayansi kwa miaka mingi. Yaani nini umuhimu wa usingizi?
Ni wazi kuwa tunahitaji kulala ili kupumzika na ili ubongo wetu ufanye kazi vyema....lakini mambo ya kibayolojia yanayofanyika tunapokuwa tumelala ndio yameanza tu kugunduliwa.

Daktari Cirelli alisema kuwa : "kwa muda mrefu, watafiti wa usingizi wamekuwa wakilenga tofauti iliyopo kati ya celi za neva wakati wanyama wanakuwa hawajalala na wakti wamelala. Kwa sasa ni bayana kuwa celi zengine kwenye mfumo wa neva hubadilika kutokana na usingizi.''
Watafiti hao wanasema kuwa matokeo yao yanapendekeza kuwa ukosefu wa usingizi,unaweza kusababisha maradhi ya ubongo yanayoathiri celi zake.

Watafiti hao pia wanataka kuchunguza ikiwa vijana kukosa usingizi wakati wanapokuwa huenda ikaathiri ubongo wao katika siku za usoni.
Usingizi ni muhimu kwa mfumo wa neva mwilini ili uweze kufanya kazi vyema.
Usingizi pia husaidia katika uzalishaji wa homoni zinazowafanya watoto na vijana kukuwa.