Kabla ya mchezo huo kuanza kulitokea vurugu za mashabiki baada ya
mashabiki wanaodhaniwa kuwa ni wa Mbeya City kulipiga mawe basi la Yanga
wakati linaingia uwanjani pamoja na gari dogo aina ya Noah lililokuwa
limebeba viongozi wa Yanga nalo lilipigwa mawe na kioo cha nyuma cha
gari kuvunjika.
Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga wamekata rufaa kwa
kamati ya Ligi kutaka mchezo wao dhidi ya Mbeya City uliofanyika
Jumamosi iliyopita urudiwe kwenye uwanja huru.
Katika mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa
Sokoine ulimalizika kwa sare ya 1-1 na kufanikiwa kuingiza Sh100 milioni
baada ya mashabiki 20,000 kushuhudia mechi hiyo.
Kabla ya mchezo huo kuanza kulitokea vurugu za
mashabiki baada ya mashabiki wanaodhaniwa kuwa ni wa Mbeya City kulipiga
mawe basi la Yanga wakati linaingia uwanjani pamoja na gari dogo aina
ya Noah lililokuwa limebeba viongozi wa Yanga nalo lilipigwa mawe na
kioo cha nyuma cha gari kuvunjika.
Wakizungumza jijini Mbeya, Ofisa habari wa Yanga,
Baraka Kizuguto akisaidiana na mjumbe wa kamati ya sekretarieti ya
Yanga, Patrick Naggi walisema, “Tunachohitaji mechi irudiwe na ichezwe
kwenye uwanja huru.”
“Tunataka mechi ichezwe kwenye uwanja huru kwa sababu ya matukio yaliyotokea katika mechi yetu dhidi ya Mbeya City ambayo yaliifanya timu kucheza bila amani kutokana na vurugu zilizokuwa zinafanywa na mashabiki wa Mbeya,” alisema Kizuguto.
“Basi la timu pamoja na Noah yaliyokuwa yamebeba
wachezaji na viongozi yalishambuliwa na vioo kuvunjwa, pia dereva wa
basi, Maulid Kihula na beki Nadir Haroub walijeruhiwa,” alisema Kizuguto
na kusisitiza wanataka uangalizi zaidi mechi yao ijayo dhidi ya
Prisons.
Naye Naggi alisema, “Tukio lile halikuwa la kimichezo, kila mtu aliyekuwa uwanjani aliona.”
Kutokana na madai hayo ya Yanga, msemaji wa
Coastal Union, Edo Kumwembe ambao basi la wachezaji wao lilipigwa mawe
na mashabiki wa Yanga jijini Dar es Salaam ametaka mechi yao pia
irudiwe.
Wakati huohuo; Kocha mkuu wa Mbeya City, Juma
Mwambusi amesema waliingia uwanjani kwa lengo la kuhakikisha
washambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu na Jerry Tegete hawafurukuti.
“Unajua tulijiandaa kwa mambo mengi, kama
unavyojua Yanga ni timu kubwa na ndiyo mabingwa watetezi kama tungefanya
mchezo wangetudhalilisha,” alisema Mwambusi. Naye kocha wa Yanga,
Ernest Brandts alisema wamepata matokeo hayo kutokana na sababu
mbalimbali moja ni uwanja mbovu.
“Staili ya mchezo ni kubutuabutua tu kama Ragbi wakati Yanga tunapenda kucheza mpira,” alisema Brandts.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni