HATUA
ya Serikali ya Tanzania kuyafungia magazeti mawili ya kila siku,
Mtanzania (kwa siku 90) na Mwananchi (siku 14), imesababisha mjadala wa
hali ya juu katika maeneo mbalimbali barani Afrika.
Gazeti
la Mail&Guardian la Afrika Kusini, liliandika kuwa hatua hiyo ni
kusambaratisha uhuru wa vyombo vya habari na kuwanyima wananchi haki ya
kupata habari.
Gazeti
hilo liliendelea kudai kuwa hatua ya kufungia vyombo vya habari ni
kuvunja maana ya upashanaji habari, ambayo inatakiwa kuwafikia
wananchi.
Chombo
hicho cha habari kimeifananisha adhabu hiyo ya kuyafungia magazeti hayo
mawili kama ile iliyochukuliwa na Serikali ya Uganda, mwanzoni mwa
mwaka huu ya kulifungia gazeti jingine la NMG, la Daily Monitor, kwa
madai lilichapisha habari ya uchochezi.
Tangazo
la Serikali ya Tanzania kupitia Gazeti la Serikali namba 333 Septemba
27 mwaka huu lilitangaza magazeti ya Mwananchi na Mtanzania yamefungiwa.
Katika
hatua nyingine, gazeti la Mail&Guardian lilimkariri Mbunge wa
Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, akisema kuwa “Kufungia magazeti
hakutazuia haki ya wananchi kutoa maoni yao na kupambana mpaka
kupatikana utawala bora.
“Kwanza
kufungiwa kwa magazeti hayo kutawaimarisha waandishi kwa kiwango cha
juu. Unalifungia gazeti kwa kutoa taarifa za mishahara? Tatizo liko
wapi, je, watu hawatakiwi kujua mishahara ya watumishi wa umma?”
Ikitumia
Sheria ya Magazeti ya Mwaka 1976, Serikali kupitia kwa Mkurugenzi wa
Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene, iliyafungia magazeti hayo kwa
madai ya kuchapisha habari zenye mwelekeo wa uchochezi na uvunjifu wa
amani. Serikali ilitangaza kulifungia Mwananchi kwa siku 14 na Mtanzania
siku 90, kuaNzia Septemba 27, mwaka huu.
Uamuzi
huo ulichukuliwa na serikali kwa madai kwamba, magazeti hayo yaliandika
habari na makala za uchochezi na uhasama kwa nia ya kusababisha
wananchi wakose imani kwa vyombo vya dola. Uamuzi huo, ambao ulikuwa
ghafla, ulipokewa kwa mshituko mkubwa na wadau mbalimbali, huku wengi
wakihoji mwelekeo wa demokrasia nchini. Wadau hao wa kada mbalimbali,
wakiwamo wanasheria, wanataaluma, wanahabari, wanaharakati, wanasiasa na
watetezi wa haki za binadamu, wote wamekuwa na kauli moja ya kufanana.
SOURCE:http://www.udakuspecially.com/2013/10/afrika-kusini-yaguswa-kufungiwa-kwa.html
|
HALI ya amani katika mji wa Mombasa
imezidi kuwa tete kutokana na makundi ya vijana wenye hasira kali
kuendeleza machafuko katika sehemu mbalimbali vya mji huo.Kwa
mujibu wa taarifa iliyotolewa na BBC, jumla ya watu wanne wamepoteza
maisha katika machafuko hayo, baada ya makundi ya vijana hao kupambana
na askari wa kutuliza ghasia.Habari
kutoka nchini humo zinaeleza kuwa machafuko hayo yametokea siku moja
baada ya kifo cha Sheikh Ibrahim Omar ‘Rogo’, aliyeuawa kwa kushambuliwa
kwa risasi na watu wasiojulikana.Katika
shambulizi hilo, pia washirika watatu wa Sheikh Rogo nao wamepoteza
maisha papo hapo, huku Salim Adbi akinusurika katika shambulizi hilo.Kwa mujibu wa taarifa zaidi kutoka mjini Mombasa, vijana wenye hasira kali wameteketeza kanisa moja katika ghasia za juzi. Sheikh
Ibrahim Rogo alikuwa mhubiri katika msikiti ambao ulikuwa unatumiwa kwa
mahubiri na marehemu Sheikh Aboud Rogo, ambaye pia aliuawa kwa kupigwa
risasi na watu wasiojulikana mwaka jana.Sheikh
Aboud Rogo alishutumiwa kutoa mafunzo yenye itikadi kali
yaliyowashawishi vijana kujiunga na kikundi cha kigaidi cha Al Shabaab.Kabla ya kifo chake, marehemu Aboud Rogo alidaiwa kuwa na uhusiano na kundi la kigaidi la Al Shabaab.Tukio
la kifo cha Sheikh Ibrahim Omar ‘Rogo’ limetokea ndani ya kipindi cha
wiki mbili baada ya shambulizi la kigaidi la Westgate Mall, ambapo jumla
ya watu 67 walipoteza maisha.Ibrahim Rogo alionekana kama mrithi wa marehemu Aboud Rogo, alipohutubu katika msikiti huo.Imeandikwa na Mtanzania
|
SULUHU
ya bila kufungana kati ya Coastal Union na Azam FC katika uwanja wa
Mkwakwani mjini Tanga imezidi kuwaongezea idadi ya suluhu Wagosi wa kaya
katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Mchezo
huo uliokuwa na presha kubwa kwa mashabiki na wachezaji ulimuweka
katika wakati mgumu mwamuzi Andrew Shamba kutoka Pwani, kutokana na
kushutumiwa kuwapendelea Azam FC.
Kipindi
cha kwanza timu zote zilicheza kwa nguvu zikihakikisha zinapata mabao
ya mapema na kujihakikishia ushindi lakini hakuna hata timu moja
iliyofanikiwa kuona lango la mwenzake.
Kipindi
cha pili kilianza kwa Azam FC kushambulia kwa kasi huku wakimiliki
mpira hali iliyowachanganya wachezaji wa Coastal Union wakaanza
kupoteana na kucheza bila kufuata mfumo. Hali hiyo ilizidi kuwachanganya
Wagosi wa Kaya hasa baada ya mwamuzi kuanza kutoa maamuzi ya utata,
kwani katika dakika ya sabini alitoa kona kwa Azam wakati ilikuwa ni
goal kick.
Mashabiki
wakaanza kuhamaki na kutaka kuvuruga mchezo baada ya mwamuzi kuzidisha
kutoa maamuzi ya utata kama faulo zisizoeleweka na kona za utata. Hali
hiyo ilimtisha mwamuzi na kusimamisha mchezo mara kwa mara ili kuwataka
wasimamizi wa mchezo huo kuwatuliza mashabiki.
Tukio
lililotokea kipindi cha kwanza ambapo mwamuzi wa pembeni alipigwa na
kitu kisichojulikana kutoka jukwaa la 'Rasha' lilitaka kujirudia kipindi
cha pili baada ya chupa na mawe kutupwa uwanjani baada ya mwamuzi kutoa
faulo nje kidogo ya 18 upande wa Coastal Union.
Dakika
ya 65 mwalimu Hemed Moroco alifanya mabadiliko na kumtoa Pius Kisambale
akaingia Suleiman Kassim 'Selembe'. Mabadiliko hayo yaliongeza uhai kwa
Wagosi hasa kutokana na aina ya uchezaji wa Selembe kutumia mipira ya
kasi.
Azam
FC walianza kuelemewa kutokana na Mganda, Yayo Kato kutumia vema mwili
wake mfupi na wenye nguvu kuwashambulia mabeki wa Azam, hali hiyo
iliwafanya Azam kubadilika na kucheza mpira wa hovyo uliowapa nafasi
Coastal Union kupiga mipira mirefu ambapo ilipofika dakika ya 75 kipindi
cha pili katika jukwaa la African Sports, Wagosi walikosa bao la wazi
baada ya Selembe kupiga krosi iliyopenya ngome ya Azam akiwemo mlinda
mlango Mwadini Ally na kugonga mwamba.
Kutokana
na piga nikupige ya lala salama kufika dakika ya 74 mwamuzi
alimnyooshea mlinzi wa kulia wa Coastal Union, kinda Hamadi Juma
'Basmat', kadi nyekundu baada ya kubadilishiana maneno na mchezaji wa
Azam, Kipre Tchetche.
Tukio
hilo lilianzia kwa Kipre kumpiga Hamadi kiwiko cha shingo hali
iliyomfanya kinda huyo kumfuata kwa jazaba huku akimuuliza kwanini
amemfanyia hivyo. Mwamuzi baada ya kuona Hamadi amemuelekezea kichwa
Kipre akadhani kinda huyo anapigana ndipo akatoa kadi ya moja kwa moja.
Baada
ya kadi hiyo hali ya uwanja ilichafuka ambapo mashabiki walikuwa
wakipiga kelele huku wachezaji wakitaka kupigana, ndipo mchezaji
mwingine wa Coastal Union beki wa kushoto Othman Tamim akapewa kadi ya
njano papo hapo.
Baadaye
mchezo ulirudi katika hali yake lakini ngome ya Coastal Union ilikuwa
imepwaya hali iliyomfanya Juma Said 'Nyoso' kuwa na kazi kubwa ya
kuhakikisha ngome yao inakuwa imara.
Ilipofika
dakika ya 84 mwlimu Moroco alifanya mabadiliko kwa kumtoa Uhuru
Suleiman na kumuingiza Yusuf Chuma. Ambapo kinda huyo alionyesha uwezo
mkubwa na kurudisha uhai wa safu ya ulinzi.
Mpaka
mwamuzi wa leo anapuliza kipyenga cha mwisho matokeo yaliendelea
kusomeka hivyo hivyohivyo 0-0, na kuendelea kuibakisha Coastal Union
katika nafasi ya nne ikiwa na point 11 nyuma ya Azam iliyo nafasi ya
tatu yenye point 11 lakini ikiwa na mabao mengi ya kufunga.
Baada
ya mechi ya leo Coastal Union itashuka dimbani wiki ijayo katika uwanja
wa Chamazi dhidi ya Ashanti United wanaoshika mkia katika ligi.
|
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni