Jumatatu, 7 Oktoba 2013

AFRIKA KATIKA PICHA

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/07/131007084609_kenya_marathoner_976x549_bbc_nocredit.jpg
Mshindi wa mbio za Marathon mjini Berlin, Ujerumani mkenya Wilson Kipsang mwenye umri wa miaka 31. Hapa anasherehekea ushindi wake. Alivunja rekodi ya mbio hizo kwa sekunde kumi na tano. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/07/131007084707_lagos_boys_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Wachezaji wa mchezo wa Roller Skating mjini Lagos Nigeria wanasherehekea miaka 53 ya uhuru wa Nigeria. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/07/131007085024_school_kid__976x549_bbc_nocredit.jpg 
Watoto wa shule pia walisherehekea uhuru wa Nigeria kote nchini humo siku ya Jumanne wiki jana 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/07/131007085937_somalia_qauarry_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Wafanyakazi wakibeba mchanga kutoka machimboni mjini Mogadishu,siku ya Jumanne. Kuna machimbo mengi kama hay ambayo yamekuwa na shughuli nyingi katika miaka miwili iliyopita tangu al-Shabab kufurushwa na kusababisha ujenzi mkubwa.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/07/131007085218_kenya_maombi_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Msichana huyu alikuwa miongoni mwa waliohudhuria maombi maalum kwa watu waliofariki kutokana na shambulizi la kigaidi dhidi ya jumba la Westgate mjini Nairobi, Kenya 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/07/131007085320_ghana_uk_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Raia hawa wa Ghana walihudhuria kongamano la kila mwaka la chama cha Conservative katika mtaa wa Manchester nchini Uingereza 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/07/131007090118_miss_world_976x549_b_nocredit.jpg 
Carranzar Naa Okailey Shooter, (kushoto) aliwakilisha Ghana katika mashindano ya mwanamke mrembo zaidi duniani. Hapa amesimama na mshindi wa mashindano hayo (katikati) kutoka Ufilipino. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/07/131007085408_boats_lights_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Wamiliki wa boti za usafiri wanawasubiri abiria kwenye fuo za mto Nile mjini Cairo. Safari za boti ni jambo la kawaida sana na watu husafiri kwa boti zaidi nyakati za jioni kujivinjari  
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/07/131007085642_tz_fishing_976x549_bbc_nocredit.jpg
Pindi wanapowasili, wavuvi hukimbia sokoni na samaki wao waliowavua kwa siku hiyo kuelekea kuwauza katika soko la Kivukoni
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/07/131007085748_octopizo_tz_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Si Samaki pekee wanaovuliwa bali pia Pweza hawa wanaoaminika kuongeza nguvu za kiume mwilini
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/10/07/131007090028_senegal_water_976x549_bbc_nocredit.jpg 
Uhaba wa maji nchini Senegal ni tatizo sugu na hii ndiyo dalili yake watu kupanga foleni kununua maji 

Hakuna maoni: