ONA WALINZI KADHAA WAUAWA MPAKANI MWA IRAQ
Shirika la habari la taifa la Iran, IRNA, limearifu kuwa walinzi 17 wa
mpaka wameuwawa katika mapambano na watu waliokuwa na silaha, kwenye
mpaka wa Iran na Pakistan.
IRNA imeeleza kuwa baada ya shambulio hilo watu 16 wamenyongwa - watu wenye uhusiano na makundi yenye uhasama na serikali.Kisa hicho cha mpakani kimetokea kwenye eneo la milima nje ya mji wa Saravan.
Washambuliaji hawajulikani, lakini mjumbe mmoja wa bunge la Saravan, Hedayatollah Mirmoradzehi, aliwaeleza hao kuwa magaidi wanaopinga mapinduzi.
Mpaka wa Iran na Pakistan huwa na machafuko na eneo hilo ni njia inayotumiwa na wafanya magendo ya mihadarati.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni